Geza Ulole
JF-Expert Member
- Oct 31, 2009
- 58,783
- 78,452
Malasusa: Chagueni mtu makini si chama
Fidelis Butahe na Fredy Azzah
MKUU wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Dk Alex Malasusa amewataka Watanzania kuchagua kiongozi makini badala ya chama. Askofu Malasusa ambaye pia ndiye Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani, alisema hayo jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia jana katika harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa la KKKT Usharika wa Kitunda Relini, iliyofanyika katika ukumbi wa Msimbazi.
Katika halfa hiyo ambayo Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye alikuwa mgeni rasmi, Askofu Malasusa alitumia dakika nane kuwaeleza watu waliofika kwenye harambee hiyo aina ya kiongozi anayefaa kuchaguliwa. Dk Malasusa alisema Watanzania wamechoka kudanganywa na akawataka kuamka na kuchagua kiongozi mwenye sifa bila kujali anatokea chama gani.
Mkuu huyo wa KKKT hilo alikuwa akirudia kusema maneno hayo mara kwa mara wakati akiongoza mnada wa kuuza vitu mbalimbali, ikiwemo picha yake, ya Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, saa na khanga. Kabla ya kumkaribisha Sumaye kuzungumza na umati uliokusanyika kwenye harambee hiyo, Dk Malasusa alisema, "Kipindi hiki ni cha kutulia na kufanya lile ambalo Mungu ametuelekeza. Taifa hili ni la Mungu, tumlilie atatuonyesha kiongozi bora." Aliendelea: "Huu sio wakati wa kuchagua chama. Ni wakati wa kuchagua mtu ambaye ni kiongozi bora.
Tumedanganywa vya kutosha miaka mingi, na kuchagua chama. "Tunahitaji kutulia na kumuomba Mungu ili atuelekeze njia ya kupata na kuchagua kiongozi bora na atakuwa nasi katika Uchaguzi Mkuu". Kauli ya Dk Malasusa inakuja siku chache baada ya viongozi wa makanisa Katoliki, KKKT na Pentekoste mkoani Kilimanjaro, kutoa waraka unaowataka waumini wao kuchagua mgombea anyafaa kuwaletea maendeleo badala ya chama cha siasa.
Wakati akipiga mnada wa khanga, ambayo ilikuwa na rangi ya njano, Askofu Malasusa alimtazama mmoja wa watu waliotaka kununua khanga hiyo na kumuuliza: "Vipi hii inakufaa? Inaonekana inafanana sana na rangi ya kile chama chako. Lakini sasa hivi ni kuchagua mtu siyo mambo ya chama".
Kauli hiyo iliwafanya watu waliokusanyika ukumbini humo kuangua kicheko huku wakipiga makofi. Dk Malasusa aliwataka waumini wa KKKT kutumia muda mrefu kutafakari na kumwomba Mungu, ili nchi iweze kupata viongozi bora na uchaguzi ufanyike kwa amani na utulivu. "Hiki ni kipindi kizuri na sisi kama sehemu ya raia wa nchi hii, tunapaswa kutulia. Tumuombe Mungu atupe kiongozi mzuri," alisema Askofu Malasusa na kuongeza: "Mkristo wa kweli hafanyi mambo kwa kukurupuka, hutulia na kumua kwa kumsikiliza Rohom Mtakatifu ".
Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Kanisa alimfagilia Sumaye akisema katika nafasi mbalimbali za uongozi wa nchi alizoshika, aliitumikia serikali na kanisa kwa uaminifu. "Katika nafasi mbalimbali alizoshika, Mheshimiwa Sumaye aliitumikia nchi hii kwa uaminifu, pia alilitumikia Kanisa," alieleza. Hivi karibuni Mkuu wa Kanisa la Anglikana nchini, Askofu Dk Valentino Mokiwa aliwataka wananchi kupokea hela za wagombea wanaotoa rushwa lakini wasiwapigie kura. Akizungumzia ujenzi wa kanisa hilo linalotajiriwa kugharimu takribani Sh900 milioni, Askofu alisema makanisa ni sehemu muhimu ya kubadili mienendo ya watu. "Watu wasipomrudia Mungu, tutaendelea kujenga magereza na kuongeza sheria bila mafanikio.
Jengo hilo ni muhimu sana, naomba tujenge nyumba ya Mungu," alisisitiza. Hata hivyo, Sumaye hakutaka kuzungumza chochote kwenye harambee hiyo zaidi ya kuiongoza hafla hiyo kama mgeni rasmi. "Katika shughuli kama hizi huwa sitoi hotuba. Waliponiletea kadi ya mwaliko, niliwauliza nani mwingine atakayehudhuria hafla hii? "Waliponiambia ni Mkuu wa Kanisa Baba Askofu Malasusa, nikawaambia mimi nitakuja lakini, Askofu naomba ndiye awe mgeni rasmi," alieleza Sumaye mara baada ya kukaribishwa.
"Kwa hiyo mimi nitakuwa MC (msemaji), kama yupo mliyemwandaa basi nitakuwa msaidizi wake," alieleza na kuendelea kuongoza harambee hiyo. Waumini wa KKKT nchini na Watanzania kwa ujumla, waliombwa kutoa michango yao ya hali na mali ili kuifanikisha ujenzi wa kanisa hilo, litakalo kuwa na uwezo wa kuchukua waumini 3,000 kwa wakati mmoja. Kanisa la sasa linalotumika na usharika huo, lina uwezo wa kuchukua waumini 800. mwishio
Malasusa: Chagueni mtu makini si chama
MY TAKE:
Haki ya Mungu Kikwete ukishinda safari hii ni kwa wizi tu! Hamna sababu nyingine watu wamekuchoka waliokuiita Chaguo la Mungu sasa wamekuchoka nathani marafiki wako ni mafisadi na wale unaoweza kuwarubuni tu!
Fidelis Butahe na Fredy Azzah
MKUU wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Dk Alex Malasusa amewataka Watanzania kuchagua kiongozi makini badala ya chama. Askofu Malasusa ambaye pia ndiye Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani, alisema hayo jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia jana katika harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa la KKKT Usharika wa Kitunda Relini, iliyofanyika katika ukumbi wa Msimbazi.
Katika halfa hiyo ambayo Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye alikuwa mgeni rasmi, Askofu Malasusa alitumia dakika nane kuwaeleza watu waliofika kwenye harambee hiyo aina ya kiongozi anayefaa kuchaguliwa. Dk Malasusa alisema Watanzania wamechoka kudanganywa na akawataka kuamka na kuchagua kiongozi mwenye sifa bila kujali anatokea chama gani.
Mkuu huyo wa KKKT hilo alikuwa akirudia kusema maneno hayo mara kwa mara wakati akiongoza mnada wa kuuza vitu mbalimbali, ikiwemo picha yake, ya Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, saa na khanga. Kabla ya kumkaribisha Sumaye kuzungumza na umati uliokusanyika kwenye harambee hiyo, Dk Malasusa alisema, "Kipindi hiki ni cha kutulia na kufanya lile ambalo Mungu ametuelekeza. Taifa hili ni la Mungu, tumlilie atatuonyesha kiongozi bora." Aliendelea: "Huu sio wakati wa kuchagua chama. Ni wakati wa kuchagua mtu ambaye ni kiongozi bora.
Tumedanganywa vya kutosha miaka mingi, na kuchagua chama. "Tunahitaji kutulia na kumuomba Mungu ili atuelekeze njia ya kupata na kuchagua kiongozi bora na atakuwa nasi katika Uchaguzi Mkuu". Kauli ya Dk Malasusa inakuja siku chache baada ya viongozi wa makanisa Katoliki, KKKT na Pentekoste mkoani Kilimanjaro, kutoa waraka unaowataka waumini wao kuchagua mgombea anyafaa kuwaletea maendeleo badala ya chama cha siasa.
Wakati akipiga mnada wa khanga, ambayo ilikuwa na rangi ya njano, Askofu Malasusa alimtazama mmoja wa watu waliotaka kununua khanga hiyo na kumuuliza: "Vipi hii inakufaa? Inaonekana inafanana sana na rangi ya kile chama chako. Lakini sasa hivi ni kuchagua mtu siyo mambo ya chama".
Kauli hiyo iliwafanya watu waliokusanyika ukumbini humo kuangua kicheko huku wakipiga makofi. Dk Malasusa aliwataka waumini wa KKKT kutumia muda mrefu kutafakari na kumwomba Mungu, ili nchi iweze kupata viongozi bora na uchaguzi ufanyike kwa amani na utulivu. "Hiki ni kipindi kizuri na sisi kama sehemu ya raia wa nchi hii, tunapaswa kutulia. Tumuombe Mungu atupe kiongozi mzuri," alisema Askofu Malasusa na kuongeza: "Mkristo wa kweli hafanyi mambo kwa kukurupuka, hutulia na kumua kwa kumsikiliza Rohom Mtakatifu ".
Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Kanisa alimfagilia Sumaye akisema katika nafasi mbalimbali za uongozi wa nchi alizoshika, aliitumikia serikali na kanisa kwa uaminifu. "Katika nafasi mbalimbali alizoshika, Mheshimiwa Sumaye aliitumikia nchi hii kwa uaminifu, pia alilitumikia Kanisa," alieleza. Hivi karibuni Mkuu wa Kanisa la Anglikana nchini, Askofu Dk Valentino Mokiwa aliwataka wananchi kupokea hela za wagombea wanaotoa rushwa lakini wasiwapigie kura. Akizungumzia ujenzi wa kanisa hilo linalotajiriwa kugharimu takribani Sh900 milioni, Askofu alisema makanisa ni sehemu muhimu ya kubadili mienendo ya watu. "Watu wasipomrudia Mungu, tutaendelea kujenga magereza na kuongeza sheria bila mafanikio.
Jengo hilo ni muhimu sana, naomba tujenge nyumba ya Mungu," alisisitiza. Hata hivyo, Sumaye hakutaka kuzungumza chochote kwenye harambee hiyo zaidi ya kuiongoza hafla hiyo kama mgeni rasmi. "Katika shughuli kama hizi huwa sitoi hotuba. Waliponiletea kadi ya mwaliko, niliwauliza nani mwingine atakayehudhuria hafla hii? "Waliponiambia ni Mkuu wa Kanisa Baba Askofu Malasusa, nikawaambia mimi nitakuja lakini, Askofu naomba ndiye awe mgeni rasmi," alieleza Sumaye mara baada ya kukaribishwa.
"Kwa hiyo mimi nitakuwa MC (msemaji), kama yupo mliyemwandaa basi nitakuwa msaidizi wake," alieleza na kuendelea kuongoza harambee hiyo. Waumini wa KKKT nchini na Watanzania kwa ujumla, waliombwa kutoa michango yao ya hali na mali ili kuifanikisha ujenzi wa kanisa hilo, litakalo kuwa na uwezo wa kuchukua waumini 3,000 kwa wakati mmoja. Kanisa la sasa linalotumika na usharika huo, lina uwezo wa kuchukua waumini 800. mwishio
Malasusa: Chagueni mtu makini si chama
MY TAKE:
Haki ya Mungu Kikwete ukishinda safari hii ni kwa wizi tu! Hamna sababu nyingine watu wamekuchoka waliokuiita Chaguo la Mungu sasa wamekuchoka nathani marafiki wako ni mafisadi na wale unaoweza kuwarubuni tu!