samirnasri
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 1,388
- 213
Malaika beach resort (MBR) ni hoteli ya kisasa kabisa iliyoko eneo la ilemela jijini mwanza. Hotel hii imejengwa juu ya miamba ya mwanza lakini pia imejengwa pembezoni kabisa mwa ziwa victoria. Kuna sehemu ya hoteli hiyo iko juu ya maji ya ziwa. Mahala ilipojengwa hoteli hiyo imezua gumzo miongoni mwa wakazi wa mwanza kwani hoteli hiyo imeshikana kabisa na maji ya ziwa na haijulikani sewage system yake inaelekea wapi. Watu wengi wamekuwa wakihoji kama hotel hiyo inamilikiwa na mtu baki au kuna kigogo wa serikali ametia mkono. Ukifika mwanza tembelea malaika beach resort ujionee mwenyewe..