Makutano Show: Exclusive Interview na Mhe. John Mnyika - Oct 06, 2012

Mkurugenzi wa Habari na Uenezi-CDM John Mnyika amesema hana mpango wa kugombea urais hivi karibuni wala katika kipindi cha miaka kumi ijayo na zaidi.Amesema Urais kamwe si kipaumbele chake.
Akihojiwa wiki iliyopita Mnyika ambaye pia ni Mbunge wa Ubungo alisema kwa sasa anayo majukumu makubwa mawili ambayo ameyaweka kama kipaumbele chake.
Mnyika amesema kipaumbele cha kwanza ni kukitumikia chama chake cha CDM kwa moyo mmoja na kuwaunganisha wanachama wote ili kujiandaa kuchukua dola 2015.
Mnyika amesema kipaumbele cha pili ni kuwatumikia wananchi wa ubungo kwa uwezo wake wote.Alisema wananchi wa Ubungo walimuamini yeye na chama chake na kamwe hatawaangusha.

urais wa nini aweke wazi maana kuna rais wa masharobaro,vyuo vikuu nk.
 
mtangazaji aliyehoji naye sifuri mnyika ana sifa zipi za kuthubutu kugombea urais.
 
HAWEZI KUWAZIA URAIS KWANI 2015 NDIO MWISHO WAKE,HILO LINAFAHAMIKA VIZURI TUH
AACHE ZAKE HASHUO HUYOO....!!
:target::msela:
 
Haya mambo ya urais waachie wenye tamaa. kwa muda mrefu sasa wakazi wa Morogoro Rd tuna matatizo makubwa ya maji kutokana na mabomba kutotoa maji kabisa. Tafadahali fanya ufuatailiaji kama ilivyo kawaida yako kabla hatujaathirika zaidi.
 
Haya mambo ya urais waachie wenye tamaa. kwa muda mrefu sasa wakazi wa Morogoro Rd tuna matatizo makubwa ya maji kutokana na mabomba kutotoa maji kabisa. Tafadahali fanya ufuatailiaji kama ilivyo kawaida yako kabla hatujaathirika zaidi.

Na kweli moja ya kipaumbele chake ni kuwatumikia wananchi wa Ubungo.
 
Haya mambo ya urais waachie wenye tamaa. kwa muda mrefu sasa wakazi wa Morogoro Rd tuna matatizo makubwa ya maji kutokana na mabomba kutotoa maji kabisa. Tafadahali fanya ufuatailiaji kama ilivyo kawaida yako kabla hatujaathirika zaidi.

Nimependa bandiko lako.
 
Back
Top Bottom