Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Kwa karibu miaka kadhaa sasa kuna mlolongo wa matukio ambayo yangetokea nchi nyingine yoyote yangetoa nafasi ya pekee kwa vyama vya upinzani. Mlolongo huo kwa Tanzania hata hivyo haujatoa nafasi hiyo kwa upinzani kiasi kwamba kama taifa badala ya kuangalia upinzani kutoa uongozi katika saa na wakati huu bado wananchi wanaangalia CCM pamoja na madudu yake kutoa uongozi kwa taifa.
Hili lawezekana ni kutokana na makosa ya upinzani na vyama vikubwa vya upinzani nchini. Makosa ambayo kimsingi kabisa yamechangia kudhoofisha demokrasia na hivyo kuufanya upinzani wa Tanzania ulivyo sasa kuwa kikwako cha mabadiliko tunayoyataka na kwamba umejenga ukuta wa kuzuia mabadiliko ya kweli kuja kwani wananchi wachache wameweka matumaini katika upinzani huo ingawa ukweli ni ulivyo sasa upinzani wa Tanzania hauwezi kuthaminiwa kuongoza taifa letu.
Kama chama chenye muundo, historia, watu na raslimali nyingi kama CCM kimeshindwa kuongoza mabadiliko ya kweli kwa Mtanzania itakuwaje kwa chama kama CUF au Chadema? Kama CCM imeshindwa kufanya hivyo ndani ya miaka 45 hivi itachukua muda gani kwa upinzani dhaifu kama wa kwetu kufanya hivyo?
Ni makosa gani ambayo upinzani usipoyarekebisha haraka (ndani ya hii miezi 12) hawatastahili kuaminiwa na uongozi wa taifa hata wakiomba kwa machozi?
Au upinzani wetu unasubiri kuombewa na kupepewa ili Mungu hatimaye awaangushie masanduku ya kura kama alivyofanya kwenye masimulizi ya safari ya wana Israeli alipowaangushia mana na kuwapeperushia kware!?
Je yawezekana upinzani wetu umekuwa hauna maana na wananchi wajitahidi kuokoa merikebu inayozama wakijua ina watu wanaoweza kuifikisha mbele kuliko kurukia mtumbwi ambao hauna uwezo wa kukabili mawimbi ya bahari!?
Hili lawezekana ni kutokana na makosa ya upinzani na vyama vikubwa vya upinzani nchini. Makosa ambayo kimsingi kabisa yamechangia kudhoofisha demokrasia na hivyo kuufanya upinzani wa Tanzania ulivyo sasa kuwa kikwako cha mabadiliko tunayoyataka na kwamba umejenga ukuta wa kuzuia mabadiliko ya kweli kuja kwani wananchi wachache wameweka matumaini katika upinzani huo ingawa ukweli ni ulivyo sasa upinzani wa Tanzania hauwezi kuthaminiwa kuongoza taifa letu.
Kama chama chenye muundo, historia, watu na raslimali nyingi kama CCM kimeshindwa kuongoza mabadiliko ya kweli kwa Mtanzania itakuwaje kwa chama kama CUF au Chadema? Kama CCM imeshindwa kufanya hivyo ndani ya miaka 45 hivi itachukua muda gani kwa upinzani dhaifu kama wa kwetu kufanya hivyo?
Ni makosa gani ambayo upinzani usipoyarekebisha haraka (ndani ya hii miezi 12) hawatastahili kuaminiwa na uongozi wa taifa hata wakiomba kwa machozi?
Au upinzani wetu unasubiri kuombewa na kupepewa ili Mungu hatimaye awaangushie masanduku ya kura kama alivyofanya kwenye masimulizi ya safari ya wana Israeli alipowaangushia mana na kuwapeperushia kware!?
Je yawezekana upinzani wetu umekuwa hauna maana na wananchi wajitahidi kuokoa merikebu inayozama wakijua ina watu wanaoweza kuifikisha mbele kuliko kurukia mtumbwi ambao hauna uwezo wa kukabili mawimbi ya bahari!?