Makosa makubwa ya kiitifaki katika suala la tuzo za miaka 50; je Ikulu watakiri??

nderingosha

JF-Expert Member
Mar 20, 2011
4,281
3,243
Katika utawala huu wa awamu ya nne imekuwa si jambo la ajabu tena kwa watanzania kusikia kuwa taasisi ya ikulu wamefanya makosa ya kiutendaji......kilichobaki kuwa kigumu sana kwao ikulu kwasasa ni kukiri kuwa kuna wakati wanafanya makosa ya kiutendaji.....hili tumeliona na tunazidi kuliona kila kukicha.......

Tujikumbushe kidogo......

  • Kuna wakati ikulu(kwa kupitia rais)walitoa gari ya Longido kwenda Loliondo......na baadae kukiri kuwa kweli makosa yalifanyika.
  • Hivi majuzi Jairo na washirika wake kafuja hela ndefu ya umma(na nashangaa kimya juu ya hatma yao!!)........haohao ikulu(kwa kupitia Luanjo)wakatoka mbele ya watanzania na kumsafisha Jairo........mpaka ikaundwa kamati teule ya bunge iliyofichua uharo tele wa Jairo.......pamoja na kuwa rais alimzuia kurudi kazini mpaka kamati imalize kazi......lakini ikulu (kwa kupitia Luanjo) haikuwahi kukiri kuwa walikosea....
Nimeanza hivi ili kukaribisha mjadala juu ya taasisi ya ikulu kushindwa kuwa tayari kukiri makosa ya kiutendaji mara yanapotokea....hivi majuzi tumeona jinsi ambavyo itifaki imeshindwa kuzingatiwa ipasavyo kwenye suala la utoaji tuzo za heshima ya miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika yetu isiyokuwepo......

  • Ebu tujiulize.....hivi kweli (hata kwa logic ndogo) inawezekanaje pasiwepo hata kiongozi mmojawapo(majaji wakuu wastaafu) wa muhimili wa mahakama kwenye tuzo???,mengi yamesemwa juu ya kina Malecela,Lowasa na Sitta kutopewa.....hili linaweza kueleweka ......kwani kwenye mihimili yao kuna waliopata tuzo........hili la majaji wakuu kukosa tuzo kwa kweli linaonekana kabisa kuwa kosa la kiitifaki........hapa ikulu wanatakiwa waje na maelezo kwa kweli...........

Angalizo: Issue hii ya tuzo watu wanaibeza lakini inaweza kuwa mojawapo ya indicator kubwa sana ya matatizo makubwa ya kiutendaji yaliyopo katika taasisi ya ikulu......ikumbukwe kuwa issue hii ime mark anti climax kubwa sana katika maadhimisho haya ya miaka 50 ya uhuru pamoja na kuandaliwa kwa mbwembwe tele na watawala......
 
hoja zako ni nzuri kama ungekuwa umefanya utafiti kidogo kujua kama unayoongea ni kweli maana kuna sehemu unakili kuwa HUKUSIKILIZA (kwa maana nyingine huna uhakika na unachokiandika), sasa kama hivyo ndivyo mbona unaanza kulaumu kabla ya kujua ukweli ulivyo! mm nafikiri kwa kuwa ili jukwaa ni chombo muhimu cha kuelimisha jamii ni vyema post zifanyiwe kazi kwanza ili kuondoa maswali mengi yasiyo na msingi!
 
hivi huu ni utawala wa awamu ya pili au ya nne?? nipeni jibu tafadhali!!
 
Tuzo anayopewa Anna Makinda hastahili kupewa mtu wa maana. Huu ni muendelezo wa ufisadi na ubinafsi unaowapumbaza wakuu wetu wa nchi. Hawana la kujivunia wanabakia kupeana matuzo feki.
 
Kwa namna ile ile Mh.Dokta alivyopata nishani ya Udaktari ndio ametoa nishani hizi kwa wenzake ambao na yeye anaona wana vigezo kama vile yeye alivyokuwa navyo mpk leo hii amekuwa Mh. Dokta. Sidhani kama zinahusiana na competency ya mtu, and that is why hata Mh. Mama asiyejua kuwa Dodoma hawaishi wabunge peke yao amepewa moja.
 
Angalizo: Issue hii ya tuzo watu wanaibeza lakini inaweza kuwa mojawapo ya indicator kubwa sana ya matatizo makubwa ya kiutendaji yaliyopo katika taasisi ya ikulu......ikumbukwe kuwa issue hii ime mark anti climax kubwa sana katika maadhimisho haya ya miaka 50 ya uhuru pamoja na kuandaliwa kwa mbwembwe tele na watawala......
Mkuu, hii nchi sasa inaendeshwa kisegemnege, si katika suala hili la tuzo tu, bali uongozi wa nchi kwa ujumla wake, hali ni mbaya sana
 
hoja zako ni nzuri kama ungekuwa umefanya utafiti kidogo kujua kama unayoongea ni kweli maana kuna sehemu unakili kuwa HUKUSIKILIZA (kwa maana nyingine huna uhakika na unachokiandika), sasa kama hivyo ndivyo mbona unaanza kulaumu kabla ya kujua ukweli ulivyo! mm nafikiri kwa kuwa ili jukwaa ni chombo muhimu cha kuelimisha jamii ni vyema post zifanyiwe kazi kwanza ili kuondoa maswali mengi yasiyo na msingi!
With no research, you have no right to speak.... naungana na wewe, mleta mada akajipange upya.
 
Katika utawala huu wa awamu ya pili imekuwa si jambo la ajabu tena kwa watanzania kusikia kuwa taasisi ya ikulu wamefanya makosa ya kiutendaji......kilichobaki kuwa kigumu sana kwao ikulu kwasasa ni kukiri kuwa kuna wakati wanafanya makosa ya kiutendaji.....hili tumeliona na tunazidi kuliona kila kukicha.......

Tujikumbushe kidogo......

  • Kuna wakati ikulu(kwa kupitia rais)walitoa gari ya Longido kwenda Loliondo......na baadae kukiri kuwa kweli makosa yalifanyika.
  • Hivi majuzi Jairo na washirika wake kafuja hela ndefu ya umma(na nashangaa kimya juu ya hatma yao!!)........haohao ikulu(kwa kupitia Luanjo)wakatoka mbele ya watanzania na kumsafisha Jairo........mpaka ikaundwa kamati teule ya bunge iliyofichua uharo tele wa Jairo.......pamoja na kuwa rais alimzuia kurudi kazini mpaka kamati imalize kazi......lakini ikulu (kwa kupitia Luanjo) haikuwahi kukiri kuwa walikosea....
Nimeanza hivi ili kukaribisha mjadala juu ya taasisi ya ikulu kushindwa kuwa tayari kukiri makosa ya kiutendaji mara yanapotokea....hivi majuzi tumeona jinsi ambavyo itifaki imeshindwa kuzingatiwa ipasavyo kwenye suala la utoaji tuzo za heshima ya miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika yetu isiyokuwepo......

  • Ebu tujiulize.....hivi kweli (hata kwa logic ndogo) inawezekanaje pasiwepo hata kiongozi mmojawapo(majaji wakuu wastaafu) wa muhimili wa mahakama kwenye tuzo???,mengi yamesemwa juu ya kina Malecela,Lowasa na Sitta kutopewa.....hili linaweza kueleweka ......kwani kwenye mihimili yao kuna waliopata tuzo........hili la majaji wakuu kukosa tuzo kwa kweli linaonekana kabisa kuwa kosa la kiitifaki........hapa ikulu wanatakiwa waje na maelezo kwa kweli...........
  • Kama hiyo haitoshi..........leo nimekumbuka.......nchi hii rais ni amiri jeshi mkuu wa majeshi ya Tanzania.....walio karibu nae kabisa kwenye hili ni wakuu wa majeshi..........tujiulize........hivi kweli wakuu wa majeshi(wastaafu)hawakustahili kupata tuzo????,tukumbuke kuwa rais akipata balaa mtu wa karibu kuchukua nchi ni mkuu wa majeshi.......hata wale wakuu wa majeshi waliotuongoza kwenye vita dhidi ya nduli Idd amin hivi hawakustahili tuzo za heshima za miaka 50????(au walipewa??maana mi sikusikiliza)......kama ndivyo hivi basi hakika makosa haya ya kiitifaki yatahitaji maelezo ya ikulu..................
Angalizo: Issue hii ya tuzo watu wanaibeza lakini inaweza kuwa mojawapo ya indicator kubwa sana ya matatizo makubwa ya kiutendaji yaliyopo katika taasisi ya ikulu......ikumbukwe kuwa issue hii ime mark anti climax kubwa sana katika maadhimisho haya ya miaka 50 ya uhuru pamoja na kuandaliwa kwa mbwembwe tele na watawala......
Anazungumzia awamu ya pili ..... hii ilikuwa ni ya mzee ruksa. Lakini mbona mambo yaliyomo ni ya juzi.... japo nazo hazikuwa tuzo... zilikuwa nishani. Nina mashaka na uelewa wako NDERI - NGOSHA. Hebu rekebisha bana ili tutoe michango ya kukuelimisha.
 
Wakuu wa JWTZ wastaafu walipewa isipokuwa George Waitara pekee. Sababu zinaeleweka hata kabla ya kunyimwa. Wale wazee 17 waliotajwa ndio walionishangaza zaidi. Walipaswa kukumbukwa tarehe 7 mwezi wa 7 mwaka 2004 ambapo TANU ilitimiza miaka 50.
 
Anazungumzia awamu ya pili ..... hii ilikuwa ni ya mzee ruksa. Lakini mbona mambo yaliyomo ni ya juzi.... japo nazo hazikuwa tuzo... zilikuwa nishani. Nina mashaka na uelewa wako NDERI - NGOSHA. Hebu rekebisha bana ili tutoe michango ya kukuelimisha.
One of a big problems with tanzanians like you,OSOKONI,Rutasinibwa and VGL.. is that....you always give simple answers to big issues.(just like your president).....that's why the only problem you see is a petty issue of time difference in tz leadership and 'tuzo not nishani issue' in this thread.....only these are of concern to you as tanzanians......(ignoring the bigger picture..)......what a bunch of ignorants you are eh!!!........
 
Speaker Ana Makinda Samamba aka mama kiroborobo anaweza kufua dafu kwa Chifu Adam Sapi Mkwawa aliyekuwa speaker wa bunge letu kwa miongo kadhaa hadi alipostaafu? Kwa nini Kikwete anakumbatia sana mama kiroborobo? Hayati Adam Sapi hakustahiili tuzo? Edwin Mtei aliyetetea mfumo wa kiuchumi tulio nao sasa enzi za Nyerere hakustahili? Licha ya majaji hao kuna wengine wengi tu waliostahili na badala yake amewapa tuzo waliohujumu nchi kama akina Nzee Nkapa.
 
Kwanza tujiulize kwanini walifanya kisirisiri?

Tuzo hilo lilitakiwa litolewe pale uwanjani mbele ya kadamnasi ya watanzania wote.
 
Tuzo anayopewa Anna Makinda hastahili kupewa mtu wa maana. Huu ni muendelezo wa ufisadi na ubinafsi unaowapumbaza wakuu wetu wa nchi. Hawana la kujivunia wanabakia kupeana matuzo feki.

Sio ili awe mpole kwenye hoja kali zenye kuidhalilisha serikali? Aitetee bungeni.
 
Swala la tuzo ya kutukuka kltaifa lilitakiwa liwe la kitaifa na lishirikishe wananchi katika mchahakato wake sio watu wachache wajifungie maliwatoni na kuchaguana kwa sifa za nani ana sushuzi wenye harufu mbaya zaidi na nani mwenye kikwapa kinachochefua zaidi. Kigezo cka utukuka wao kilitakiwa kiwe utumishi wao kwa wananchi na ilitakiwa iangalie nyanja zote hata ikiwa na viongozi wa dini na hata watu wa kawaida wa mtaani. Wapo watu wa kawaida kabisa mitaani na vijijini ambao wamefanyia mengi kwa taifa hili ambao wanastahili kukumbukwa kwa nini wachaguane wao tu?
 
Unategemea nini kama orodha ya wapewa tuzo iilitayarishwa na Salva Rweyemamu na Premy Kibanga?
 
Katika utawala huu wa awamu ya nne imekuwa si jambo la ajabu tena kwa watanzania kusikia kuwa taasisi ya ikulu wamefanya makosa ya kiutendaji......kilichobaki kuwa kigumu sana kwao ikulu kwasasa ni kukiri kuwa kuna wakati wanafanya makosa ya kiutendaji.....hili tumeliona na tunazidi kuliona kila kukicha.......

Tujikumbushe kidogo......

  • Kuna wakati ikulu(kwa kupitia rais)walitoa gari ya Longido kwenda Loliondo......na baadae kukiri kuwa kweli makosa yalifanyika.
  • Hivi majuzi Jairo na washirika wake kafuja hela ndefu ya umma(na nashangaa kimya juu ya hatma yao!!)........haohao ikulu(kwa kupitia Luanjo)wakatoka mbele ya watanzania na kumsafisha Jairo........mpaka ikaundwa kamati teule ya bunge iliyofichua uharo tele wa Jairo.......pamoja na kuwa rais alimzuia kurudi kazini mpaka kamati imalize kazi......lakini ikulu (kwa kupitia Luanjo) haikuwahi kukiri kuwa walikosea....
Nimeanza hivi ili kukaribisha mjadala juu ya taasisi ya ikulu kushindwa kuwa tayari kukiri makosa ya kiutendaji mara yanapotokea....hivi majuzi tumeona jinsi ambavyo itifaki imeshindwa kuzingatiwa ipasavyo kwenye suala la utoaji tuzo za heshima ya miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika yetu isiyokuwepo......

  • Ebu tujiulize.....hivi kweli (hata kwa logic ndogo) inawezekanaje pasiwepo hata kiongozi mmojawapo(majaji wakuu wastaafu) wa muhimili wa mahakama kwenye tuzo???,mengi yamesemwa juu ya kina Malecela,Lowasa na Sitta kutopewa.....hili linaweza kueleweka ......kwani kwenye mihimili yao kuna waliopata tuzo........hili la majaji wakuu kukosa tuzo kwa kweli linaonekana kabisa kuwa kosa la kiitifaki........hapa ikulu wanatakiwa waje na maelezo kwa kweli...........

Angalizo: Issue hii ya tuzo watu wanaibeza lakini inaweza kuwa mojawapo ya indicator kubwa sana ya matatizo makubwa ya kiutendaji yaliyopo katika taasisi ya ikulu......ikumbukwe kuwa issue hii ime mark anti climax kubwa sana katika maadhimisho haya ya miaka 50 ya uhuru pamoja na kuandaliwa kwa mbwembwe tele na watawala......
Pumba.
 
Katika utawala huu wa awamu ya nne imekuwa si jambo la ajabu tena kwa watanzania kusikia kuwa taasisi ya ikulu wamefanya makosa ya kiutendaji......kilichobaki kuwa kigumu sana kwao ikulu kwasasa ni kukiri kuwa kuna wakati wanafanya makosa ya kiutendaji.....hili tumeliona na tunazidi kuliona kila kukicha.......

Tujikumbushe kidogo......

  • Kuna wakati ikulu(kwa kupitia rais)walitoa gari ya Longido kwenda Loliondo......na baadae kukiri kuwa kweli makosa yalifanyika.
  • Hivi majuzi Jairo na washirika wake kafuja hela ndefu ya umma(na nashangaa kimya juu ya hatma yao!!)........haohao ikulu(kwa kupitia Luanjo)wakatoka mbele ya watanzania na kumsafisha Jairo........mpaka ikaundwa kamati teule ya bunge iliyofichua uharo tele wa Jairo.......pamoja na kuwa rais alimzuia kurudi kazini mpaka kamati imalize kazi......lakini ikulu (kwa kupitia Luanjo) haikuwahi kukiri kuwa walikosea....
Nimeanza hivi ili kukaribisha mjadala juu ya taasisi ya ikulu kushindwa kuwa tayari kukiri makosa ya kiutendaji mara yanapotokea....hivi majuzi tumeona jinsi ambavyo itifaki imeshindwa kuzingatiwa ipasavyo kwenye suala la utoaji tuzo za heshima ya miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika yetu isiyokuwepo......

  • Ebu tujiulize.....hivi kweli (hata kwa logic ndogo) inawezekanaje pasiwepo hata kiongozi mmojawapo(majaji wakuu wastaafu) wa muhimili wa mahakama kwenye tuzo???,mengi yamesemwa juu ya kina Malecela,Lowasa na Sitta kutopewa.....hili linaweza kueleweka ......kwani kwenye mihimili yao kuna waliopata tuzo........hili la majaji wakuu kukosa tuzo kwa kweli linaonekana kabisa kuwa kosa la kiitifaki........hapa ikulu wanatakiwa waje na maelezo kwa kweli...........

Angalizo: Issue hii ya tuzo watu wanaibeza lakini inaweza kuwa mojawapo ya indicator kubwa sana ya matatizo makubwa ya kiutendaji yaliyopo katika taasisi ya ikulu......ikumbukwe kuwa issue hii ime mark anti climax kubwa sana katika maadhimisho haya ya miaka 50 ya uhuru pamoja na kuandaliwa kwa mbwembwe tele na watawala......

Napata taabu kuelewa unapoandika kwenye Ttle "Makosa makubwa ya kiitifaki..." Halafu ndani ya uzi ukaeleza vitu tofauti. Hebu anza kwa kufafanua maana ya neno Itifaki kama ulivyolitumia hapo. Au limekupendeza tu?
 
Back
Top Bottom