nderingosha
JF-Expert Member
- Mar 20, 2011
- 4,281
- 3,243
Katika utawala huu wa awamu ya nne imekuwa si jambo la ajabu tena kwa watanzania kusikia kuwa taasisi ya ikulu wamefanya makosa ya kiutendaji......kilichobaki kuwa kigumu sana kwao ikulu kwasasa ni kukiri kuwa kuna wakati wanafanya makosa ya kiutendaji.....hili tumeliona na tunazidi kuliona kila kukicha.......
Tujikumbushe kidogo......
Tujikumbushe kidogo......
- Kuna wakati ikulu(kwa kupitia rais)walitoa gari ya Longido kwenda Loliondo......na baadae kukiri kuwa kweli makosa yalifanyika.
- Hivi majuzi Jairo na washirika wake kafuja hela ndefu ya umma(na nashangaa kimya juu ya hatma yao!!)........haohao ikulu(kwa kupitia Luanjo)wakatoka mbele ya watanzania na kumsafisha Jairo........mpaka ikaundwa kamati teule ya bunge iliyofichua uharo tele wa Jairo.......pamoja na kuwa rais alimzuia kurudi kazini mpaka kamati imalize kazi......lakini ikulu (kwa kupitia Luanjo) haikuwahi kukiri kuwa walikosea....
- Ebu tujiulize.....hivi kweli (hata kwa logic ndogo) inawezekanaje pasiwepo hata kiongozi mmojawapo(majaji wakuu wastaafu) wa muhimili wa mahakama kwenye tuzo???,mengi yamesemwa juu ya kina Malecela,Lowasa na Sitta kutopewa.....hili linaweza kueleweka ......kwani kwenye mihimili yao kuna waliopata tuzo........hili la majaji wakuu kukosa tuzo kwa kweli linaonekana kabisa kuwa kosa la kiitifaki........hapa ikulu wanatakiwa waje na maelezo kwa kweli...........