Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 71,257
- 105,389
Hivi maandishi yote niliyoandika umeyasoma au umeruka tu?Yaani swali linajibiwa na swali linafuatiwa na swali alafu tena swalii...... yaani mpaka nimechokaa.
Mkuu nimeuliza swali jepesi tu lakini jibu ulilotoa ni irrelevant na nilichokuuliza na ukarukia fasta kwenye conclusion wakati hata wewe mwenyewe bado hujathibitisha unachosimamia.
It is like you've miscontrued what exactly i have asked, i find hard to extend this argumentation with you anymore.. you derail my questions to your own way you want it to be and you ain't reaady to answer as it originally is.
Mimi hata sijauliza kama unaamini uwepo wa wanachama wa freemasonry kama ulekeo wa majibu yako unavyoonyesha, mimi nimeuliza je unaamini hiyo dini ya freemasonry ipo!!?
Kama ipo niambie who are those religion worshippers worshipping for if not the devil..!!?
Ni hivi, kuwapo kwa hao Freemasons ni kama kuwapo kwa watu wanaoamini mlima Kilimanjaro upo Kenya.
Ukweli kwamba nakubali kwamba kuna watu wanaamini mlima Kilimanjaro upo Kenya haufanyi mlima Kilimanjaro uwepo Kenya.
Vivyo hivyo, ukweli kwamba nakubali kuna watu wanaamini u Freemason, wanaamini kuwapo kwa shetani (wanamuamini/ muabudu shetani kwa mujibu wako) haufanyi shetani huyo awepo. Wanaweza kuamini kuwapo kwa shetani ambaye hayupo!
Imani yao inaweza kuwa potofu tu.
Sawasawa na watu wanaoamini kwamba mlima Kilimanjaro upo Kenya.
Kuamini mlima Kilimanjaro upo Kenya hakufanyi mlima Kilimanjaro uwepo Kenya.
Unachoniambia mimi hapa ni hiki.
"Wewe Kiranga umekubali kwamba kuna watu wanaamini mlima Kilimanjaro upo Kenya. Hivyo ni lazima mlima Kilimanjaro upo Kenya. Na wewe unaamini mlima Kilimanjaro upo Kenya. Kama mlima Kilimanjaro haupo Kenya hao wanaoamini mlima Kilimanjaro upo Kenya wataaminije mlima Kilimanjaro upo Kenya?"
Huoni kwamba inawezekana watu wakawa na imani potofu wakaamini mlima Kilimanjaro upo Kenya wakati kwa kweli upo Tanzania?
It is the same argument as.
"Wewe Kiranga umekubali kuna watu wanaamini u Freemason (lets say u Freemason ni kumuabudu shetani kwa mujibu wako). Hivyo ni lazima imani ya u Freemason ni ya kweli (this is a logical non sequitur, you draw a connection where there is none). Na wewe unamuamini shetani. Na shetani yupo. Kama shetani hayupo hao Freemason wanaomuamini shetani wangemuaminije?
Hivi ni lazima kitu kiwepo ili watu wakiamini?
Kama hivyo ni kweli, vipi watu wawili wakiwa na imani tofauti, hiyu anaamini kipo na huyu anaamini hakipo. Kitu kitakuwa kipo au hakipo?
Kama mtu hawezi kuamini meza ipo ndani ya chumba mpaka meza iwepo, wakitokea watu wawili, mmoja anaamini na mwi gine haamini hilo lina maana gani? Meza ipo au haipo?
Unaposema u Freemason unaonesha kwamba shetani yupo, kwa zababu asingekuwepo hao Freemason wasingemuamini, vipi kuhusu mimi na ma atheist wenzangu ambao hatuamini kwamba kuna mungu wala shetani? Imewezekanaje tusiamini jama shetani yupo na kuwepo kwake kunafanya watu waamini kuwa yupo?