Makongoro Nyerere ampasulia JK!

Hapana mkuu!bado naendelea kukataa kwamba 'Nyerere alituletea fisadi Mkapa'!By that time mkapa hakuwa fisadi.Nyerere hakuwa Mungu wa kumtambua Mkapa kuwa atakuwa fisadi baadae.Unafahamu kuwa Mkapa aliingia ikulu akiitwa aka 'Mr.Clean'?Sasa hilo la kutuletea fisadi limetoka wapi?Ndomana nimekuuliza hayo mabaya ya Mkapa wakati akinadiwa na mwl Nyerere ni yapi ili tupate uhakika kuwa Nyerere aliyafumbia macho?Otherwise nakubaliana na wewe kuwa Nyerere hakuwa malaika,kuna makosa alifanya kama alivyokiri mwenyewe lakini hili la "kutuletea fisadi Mkapa"bado nalikataa.Huwezi kulinganisha hilo na Kikwete kuwapigia kampeni akina Mramba,Chenge,Lowasa na Rostam kwakuwa hawa tayari walikuwa ni sehemu ya mijadala ya ufisadi popote nchini na nje ya nchi.Sasa Mkapa as CCM presidential candidate by that time alikuwa na image ipi mbaya kuhusu utendaji wake?

Ufisadi wa Mkapa haukuanza baada ya kuwa rais kwani kiti cha urais hakimfanyi mtu kuwa fisadi.Ufisadi ni hulka ya mtu, hivyo Mkapa alikuwa fisadi tangu anazaliwa ila tu alikuwa ameficha makucha yake, sasa Mwalimu hakulijua hilo, fine,lakini kutokujua ufisadi wa Mkapa hakumuondolei lawama ya kuwa ni yeye aliyemuingiza ikulu.
 
hapana mkuu!bado naendelea kukataa kwamba 'nyerere alituletea fisadi mkapa'!by that time mkapa hakuwa fisadi.nyerere hakuwa mungu wa kumtambua mkapa kuwa atakuwa fisadi baadae.unafahamu kuwa mkapa aliingia ikulu akiitwa aka 'mr.clean'?sasa hilo la kutuletea fisadi limetoka wapi?ndomana nimekuuliza hayo mabaya ya mkapa wakati akinadiwa na mwl nyerere ni yapi ili tupate uhakika kuwa nyerere aliyafumbia macho?otherwise nakubaliana na wewe kuwa nyerere hakuwa malaika,kuna makosa alifanya kama alivyokiri mwenyewe lakini hili la "kutuletea fisadi mkapa"bado nalikataa.huwezi kulinganisha hilo na kikwete kuwapigia kampeni akina mramba,chenge,lowasa na rostam kwakuwa hawa tayari walikuwa ni sehemu ya mijadala ya ufisadi popote nchini na nje ya nchi.sasa mkapa as ccm presidential candidate by that time alikuwa na image ipi mbaya kuhusu utendaji wake?
basi nadhani kwa maelezo yako mnyakatari, natumai labda hayati mwl. Nyerere angezingatia kutojiingiza katika kushauri au kudominate power wakati wa kupitisha jina la mgombea uraisi ktk kipindi icho, kwani binadamu kigeugeu na anabadilika, yani jinsi unavyoniona nichukulie kama napretend, wajua mabenka wana utaratibu unaokuwa moyoni na si hadharani kuwa "lazima awe makini dhidi ya mteja yeyote atakaye tokea mbele kwani kama ukimuongezea ela hatorudisha, pia aweza kukuchomekea ela feki ukimshtukia atajidai nae hakufahamu au ni bahati mbaya" so aya ma kina ben ni majanja janja sana lakini na maovu yake bado anathaminiwa sana na ccm, log off
 
ufisadi wa mkapa haukuanza baada ya kuwa rais kwani kiti cha urais hakimfanyi mtu kuwa fisadi.ufisadi ni hulka ya mtu, hivyo mkapa alikuwa fisadi tangu anazaliwa ila tu alikuwa ameficha makucha yake, sasa mwalimu hakulijua hilo, fine,lakini kutokujua ufisadi wa mkapa hakumuondolei lawama ya kuwa ni yeye aliyemuingiza ikulu.
nimeipenda na imesomeka, iko very true
 
Rejea posti yangu vizuri, mimi nimemkumbusha kuwa hata Baba yake alishatutia chaka la Simba na kutuaminisha kuwa Mkapa anafaa.
Usikurupuke kureply usichokielewa.
Shifta, naona uko kwenye payroll ya watu, au? Nashangaa umeshikilia wazo lako hili kila thread hadi unaonya watu wasikurupuke wakati wewe mwenyewe unakurupuka hapo. Acha kusafisha watu kwa kuchafua watu wanaoheshimika na jamii ya Tz na dunia. Baba wa Taifa alipompigia debe rais wa awamu ya tatu, Mkapa alikuwa kada safi bila tuhuma yoyote, hakuwa na makundi, wala backround ya ufisadi, bali alikuwa mjamaa kwelikweli. Kama siyo hivyo wewe utueleze kwa uthibitisho...

EL wako huwezi ukamlinganisha na Mkapa wakati anapigiwa debe na baba wa taifa. EL na rafiki yake ni wachafu, bahati yake ni kwa vile bado nchi hii imejaza watu wanaopenda amani, wengi wao wakiwa bado wajinga na wasiojuwa hata haki zao. Lakini mabadiliko yameshaanza na watu Tz wanaanza kuamka na itakuwa vigumu sana kwa watu wenye madudu yao kuwania uongozi wa kitaifa bila kukaguliwa na kuumbuliwa. EL safari hii ataumbuliwa sana tu...

Mkapa amekuja kuchafuka baadae. Hawezi kuwa sawa na mtu mwenye tuhuma lukuki hata kabla ya kuingia Ikulu. Hatutaki watu wa jinsi hiyo, kama unampenda sana, mchukuwe ukanywe naye chai..
 
Ufisadi wa Mkapa haukuanza baada ya kuwa rais kwani kiti cha urais hakimfanyi mtu kuwa fisadi.Ufisadi ni hulka ya mtu, hivyo Mkapa alikuwa fisadi tangu anazaliwa ila tu alikuwa ameficha makucha yake, sasa Mwalimu hakulijua hilo, fine,lakini kutokujua ufisadi wa Mkapa hakumuondolei lawama ya kuwa ni yeye aliyemuingiza ikulu.
DW na wewe umetumwa tu na mwenzako ni Shifta. Ukweli huna hoja ya maana bali unapoteza muda wako ku-spin maneno ili uweze kutowa shutuma zako kwa hayati baba wa taifa. Mimi sikubaliani nanyi katika lengo lenu kamwe...
  • Sasa hiyo maneno uliyosema hapo juu je, unaweza kututhibishia kuwa Mkapa alikuwa fisadi tangu kuzaliwa?
  • Je Nyerere kutojuwa ufisadi wa Mkapa linakuwaje ni kosa kwake?
  • Je ulitaka awe malaika ili ajue mambo ya wakati uliopo na unaokuja?
Hizo lawama unazotowa na kipimo unachopimia ndicho utakachopimiwa na wewe...
 
Eheeeeeeee!!!!!!!si umeona ehh wameacha mada wanajadili mambo ya dini,JF mambo yote.Kibiblia shetani alikuwa ndie malaika mkuu hadi alipoasi.
 
Hayati Baba wa Taifa alishasema Makongoro ni Mhuni!
Kama unamkumbuka enzi zake alizokuwa NCCR na Kuingia mjengoni kupitia jimbo la Kamanda Lema
 
Hakuwahi kuwa malaika bali aliishi na malaika "Just reminding"

Alikua malaika miongoni mwa malaika wengi mbinguni kabla hajasukumwa na tamaa yake binafsi na kuasi na hivyo kujifanya mwenyewe Shetani na Ibilisi (Shetani maana yake MPINZANI na
Ibilisi maana yake ni MCHONGEZI) pale alipomdanganya Hawa ktk bustani ya Eden (refer Mwanzo sura ya 2)
 
Ufisadi wa Mkapa haukuanza baada ya kuwa rais kwani kiti cha urais hakimfanyi mtu kuwa fisadi.Ufisadi ni hulka ya mtu, hivyo Mkapa alikuwa fisadi tangu anazaliwa ila tu alikuwa ameficha makucha yake, sasa Mwalimu hakulijua hilo, fine,lakini kutokujua ufisadi wa Mkapa hakumuondolei lawama ya kuwa ni yeye aliyemuingiza ikulu.

Hakuna mtu anayezaliwa akiwa Fisadi mkuu. Ufisadi unatokana tu na tamaa za mtu mwenyewe iwe kwa kutamani yeye mwenyewe moja kwa moja au kwa kushawishiwa kutamani vitu flani na hivyo kusukumwa kuvipata kwa njia isiyo ya halali. Inawezekana Mkapa alikuwa na Tamaa hiyo wakati Mwalimu yupo lakini haikujidhihirisha kiasi cha Mwalimu kuitambua. Ufisadi wa Mkapa umekuja kujidhihirisha baada ya Mwalimu kufa.
Hapo kama unamlaumu Mwalimu kwa hilo basi ni kumlaumu kwa mapungufu yake kama binadamu kwamba hana uwezo wa kusoma yaliyo hasa moyoni mwa Mtu ambayo kimsingi anaweza kuwaza zuri leo na kesho akawaza lingine baya.

Point yangu kuu ni kuwa hakuna mtu anayezaliwa na hulka ya Tabia mbaya au nzuri. Ila mtu anajifunza na kukuza tabia nzuri au mbaya
 
Jamani hii habari ni ya lini? Makongoro aliyasema hayo katika kikao kilichoisha jana (25/11/2011) ni katika kikao kile cha mwezi Aprili, 2011? Naona humu JF tumeanza mtindo kulishana habari kama vile ni habari mpya kumbe ya zamani. Hata kama habari ni relevant ni vizuri ikawekwa sawa kwamba ni lini na wapi yalisemwa hayo.

Chanzo cha habari kimewekwa. sasa wewe unataka nini tena kiwekwe sawa.Soma.
 
Naliongea hili nikiwa sina maslahi kabisa na magamba! Mkuu usisahau wakati ule kiuongozi walau Mkapa alikuwa nafuu kuliko, Lowassa. Vichwa aina ya rostam ndo walimchakachua akili yake kuelekea 2005.

Alichakachuliwa na tumbo lake mwenyewe.Hata mama Ngina wake anasingiziwa.
 
Makongoro mwenyewe alikataliwa na Mwl. Hata alipochaguliwa kuwa Mbunge wa Arusha Mwl aliwabeza watu wa Arusha na kusema wanaongozwa na kipofu. "Hana jipya".
 
We vipi JK alipo inia mko wa Lowassa juu nakusema hajapata kuona mtu kama yeye ni kwa sababu Lowassa
aliamua kujiuzuru uwaziri mkuu kwa ajili yakumlinda raisi na madudu yake manake serikali ingeanguka kwa mara yakwanza bongo kwahiyo jamaa akajitoa mhanga kumlinda mshikaji sasa naona JK anamtosa EL kimtindo kwa njia ya Nape ndio maana juzi ktk kikao cha NEC EL alianza kumwaga unga kwa kumwambia alivyo mpigia cm wakati akiwa nje ya nchi kwamba hii Richmond anaiona nikampuni ya kitapeli JK akamwambia hapa nimepata ushauri toka kwa makatibu wakuu wawizara husika hakunakitukama hicho
Haya matatizo yakudaiwa na Richmond Tanesco kuparaganyika katika kuto ahuduma ya umeme yote hayo msabishaji mkubwa ni bwana JK kwasababu aliijua fika kampuni hewa ya Richmond naalikuwa namaslahi nayo mojakwamoja.
 
Huyu Makongoro sijui Makhirikhiri ni uharo tu anaouongea.
Baba yake alimshika mkono Mkapa na kutuambia kuwa Mkapa ni mtu safi.

Sasa ana usafi gani kwa mali alizojilimbikizia yeye na mkewe?

Usimlaumu Nyerere. Kumbuka Mkapa alijivua gamba la usafi baada tu ya Nyerere kufa, ndipo akaanza kuonesha true colours zake
 
Back
Top Bottom