RC Makonda: Marufuku viongozi wa Dini kupanga foleni ofisi za Wakuu wa Wilaya

View attachment 388265Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amepiga marufuku viongozi wa dini kupanga foleni wanapokwenda katika ofisi za wakuu wa wilaya wa mkoa huo.

Makonda ametoa agizo hilo leo jijini Dar es salaam wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa ofisi za Baraza kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata)

"Natoa wito kwa wakuu wa wilaya wote katika mkoa wangu, ni marufuku kumkuta kiongozi wa dini kupanga foleni katika ofisi zenu,hawa watu lazima waheshimiwe kama viongozi wengine wanavyoheshimiwa "alisema

Kuhusu ujenzi wa ofisi za Bakwata, Makonda amesema kuwa ujenzi huo umefadhiliwa na mfuko wa GSM.

" GSM foundation ndio inayojenga ofisi za Bakwata hivyo jamii inayonunua bidhaa za GSM ijue kuwa fedha wanazotoa zitarudi kwa jamii "alisema

Mufti mkuu wa Tanzania sheikh Abubakar Zubairy bin Ally, amewataka waumini wa dini ya kiislaam kuachana na dhana potofu ya kuwa jengo hilo si halali kutokana na jitihada za ujenzi wake kufanywa na muumini wa kikristo.

" Katu hatutashtushwa na kejeli za mitandaoni, Mkuu wa mkoa anayohaki ya kusaidia jamii ambayo imezungukwa na makundi mbalimbali ya dini "alisema.

Kiongozi wa imani flani ana umuhimu kuliko mwananchi aliewahi kwenye foleni?Mbona mnatufanya wananchi sisi ni takataka?

Imani ya mtu ina uhusiano gani upendeleo?Kwanini lakini wananchi tunaonewa hivi?

Serikali na watu jamii ya makonda wanadhani ndio kua karibu na viongozi wa dini ndio kua karibu na mioyo ya wananchi wanafeli kupita maelezo,haki ya mtu haitulizwi kwa upuuzi wa dini,mtu akichoka ni kachoka,tuheshimiane,kuna siku tutalipuka ujue
 
Ahahahaha huyu dogo mbona anaanzisha mambo magumu kutekelezwa!! Mwenyekiti wa jumuiya nae kiongozi wa dini sasa kwenye jamii wapo wenyeviti wangapi na je zoezi la utambuzi kwa hao viongozi wanapofika kwenye hizo ofisi mbona litazidisha foleni maradufu? na kama shekhe anatambulika kwa kanzu na kofia yake ya heshima je kila atakayefika kwenye hizo ofisi akisema ni kiongozi watamkataliaje? Haya mambo bana sijui tutaishia wapi kila kitu amri
 
Naomba kujuzwa haswa hii GSM ni taasisi inayojihusisha na nini lengo lake???

Kwanini wanawatumia watu wenye ushawishi kwenye kutoa misaada kama wanasiasa wafanyabiashara tifauti wasanii wakubwa?

Ni kwanini watu wanawatumia kama agency ya kutolea au kupokelea misaada?

Ni shughuli gani hasa wanaifanya for a living na ownership yake ipo vipi???
Mtaka-Anthony-380x240.jpg
PIX 4 A.JPG
images-1.jpg
3(1).JPG
IMG_1776.jpg
images.jpg
AliKiba-akiwa-na-bosi-wa-GSM.jpg
CezZoTkW4AA6sxY.jpg
CeImR8aVAAEUg_X.jpg
alafu makonda ana intetest gani kwenye hii company mbona yupo kama nae ni shareholder?
 
Mi hapo hata sijamuelewa.... ni viongozi gani hasa anaozungumzia hapa??? Kiongozi wa dini mathalani kwa wakristo.... je ni Kadinali?? Askofu?? Mchungaji/padre? Sista?? Kiongozi wa jumuiya?? Mzee wa kanisa???Katekista??

Na utamjuaje hasa huyu ni kiongozi wa dini?? Atakuwa kavaa kitambulisho?? Kwa waislam kwa mfano kiongozi wa dini ni yule atakayevaa kanzu?? Ni viongozi wa bakwata au mashehe wa misikiti?? Au mashehe wa mikoa/wilaya?? maimamu??

Na nje ya wakristu na waislam... dini nyingine kama za babu yangu Mtuweta, ambaye yeye ndio kiongozi wake mkuu wilayani, atazitambua?? Au anazungumzia dini zilizoletwa na ndege/meli??

Ngoja tuendelee na hii sinema mpya maana zile za walimu kupanda bure daladala, kuondoa ombaomba, kufukuza machangudoa nk nk nk..... bado zinaendelea. Strerling hauwawi....
hata wenyeviti wa jumuiya ni viongozi wa dini

Burudani itakuja pale ambapo kuna viongozi wa dini kama kumi hivi wanasubiri huduma... sijui watapanga foleni?
 
Naomba kujuzwa haswa hii GSM ni taasisi inayojihusisha na nini lengo lake???

Kwanini wanawatumia watu wenye ushawishi kwenye kutoa misaada kama wanasiasa wafanyabiashara tifauti wasanii wakubwa?

Ni kwanini watu wanawatumia kama agency ya kutolea au kupokelea misaada?

Ni shughuli gani hasa wanaifanya for a living na ownership yake ipo vipi???
naskia ina uhusiano fulani na home shopping center
 
Ni hii serikali au ni Mako...
Nilijua Serikali haina Dini
Ila naona hii Dar ya Mako...
Ina Dini

???

Mkuu hacha uchochezi wa kidini ww....kama ni mwislam husijenge chuki kuona aliyeweka jiwe la msingi ni mkiristo....na kama ni mkiristo hiwe vivyo hivyo.....Serikali kweli haina dini ila sio kwamba haitambui na kuheshimu watu/raia wenye dini....
 
GSM,ni kampuni ya hedha awadh kama sijakosea,wanauza cement za dangote,mabati,pikipiki,magodoro n,k, ni waislamu,paul makonda ni kama anaweka tu support,lakin sidhan kama yeye ndo ametoa hzo hela kujenga,NA HATA KAMA NA YEYE AKISAIDIA HAKUNA UHARAMU,MUNGU NDO ANAJUA KAMA ATAMLIPA AU LA,TUSIHUKUMU,TUPONGEZE KWA HLO
 
Back
Top Bottom