Du hata Baraza kivuli (la wabunge wa Upinzani) nalo wajiuzulu haiwezekani watanzania wakafa kwa mabomu tena ya mjini kabisa
WANANCHI HATUKO SALAMA TENA WALA MALI ZETU, KIIO KILA LEO NA MAYATIMA KUONGEZEKA: KWA HILI SERIKALI NZIMA IJIUZULU HATA KABLA YA MAANDAMANO
YA KUTETEA 'UHAI WA WENZETU' KUANZA KOTE NCHINI
Mheshimiwa Kikwete kama amiri jeshi mkuu ajiuzulu pamoja na serikali yake.
Yalianza na vifo vya raia kule (1) Pemba, baadaye (2) Unguja, Kisha (3) Mbagala, nako Arusha Mjini, (4) mauaji ya wakulima kule Mashamba ya mpunga kule Mabuki Mbeya na sasa (5) Gongolamboto.
Ajabu ni kwamba licha ya wananchi wengi kuuaua na mali zao kuteketea, hakuna hata mtu mmoja aliyewahi kuwajibika wala kuwajibishwa serikalini. Kote ni kiburi na jeuri tu mbe ya kupotea uhai wa mtu na watoto kubaki miyatima!!!
Jukumu la msingi halijazingatiwa; kuna watu wanasinzia kwenye majukumu nyeti na sasa kutugharimu kiasi hini, wananchi hatuko salama!! Tusianze kuzungusha kiswahili hapa ni uhai umepotea kwa uzembe!!! Hawa mayatima wanahitaji sauti zetu!!
Hatutaki tena tume kwani hata kule Mbagala chombo kama hicho hakikutusaidia zaidi ya kuwapa wanasiasa na makampuni ya kibiashara kujinadi kwenye kioo cha televisheni mgongoni mwa msiba na damu kwa wengine.
Jukumu la kwanza la kuhitajika uwepo wa serikali katikati yetu NI KUHAKIKISHA USALAMA KILA MMOJA WETU NA MALI ZETU. Kwa mtaji hizi picha nilizoona, serikali nzima ya CCM ijiuzulu mara moja
Mauaji Arusha walitupuuza kana kwamba kuliuaua nzi tu. Kule kwenye mashamba ya mpunga wala hawakujishughulisha kitu kuwajibika mtu. Sasa kama kweli kuna JAMBO AMBALO KIUKWELI KABISA KINATUHITAJI KUANDAMANA MPAKA KUELEWEKE NI KATIKA KUTETEA UHAI WA WENZETU.
Kama tutaona vifo hivi kama vile ni ya 'akina wale' na kwamba sisi wengine hatuhusiki basi hapo ndipo kiama chetu kinapoanzia. Kwa vifo hivi vyote 17 taifa tumepata yatima wangapiii?????????????
Debris and arms were hurled across the Tanzanian of city of Dar es Salaam on Wednesday night after an accident triggered a series of explosions at Gongola Mboto military base.
Tanzania's Red Cross says about 200 children who lost their parents during the confusion of the blasts are being cared for at the city's stadium.
Jamanii kuna habari za kiintelijensia zinasema jeshi lilishakuwa tayari kwa milipuko dalili zilishaanza kuonekana tangu saa 5 asubuhi....waliwapigia simu wastaafu wa vyeo juu...woote wanaokaa ukonga na gmboto kuwa waondoke.....kuna mstaafu mmj ambae ame pooza anaishi ukonga aliondoka saa 9,,.....,wanajeshi walishajiandaaa wakawa on high alert hajafa hata mmj....walijua...fanyeni utafiti
mara zote hesabu znazohusisha askari hukokotoa kati ya raia na askari.
Mkuu,
Kuna wanajeshi zaidi ya 4 wamepoteza maisha. Ngoja niendelee na intelijensia yangu nitakuja na majina kabisa. Kuna malalamiko ya ufanyaji kazi katika mazingira magumu hasa kwa sakari wa vyeo vya chini. Kifupi ni uzembe tu ndicho kilichopelekea maafa hayo.
Mtumishi wa mungu Masa na wengine: Inawezekana kabisa kuwa hakuna mwanajeshi hata mmoja aliyekufa na hiyo inawezekana tu kama yafuatayo ni sahihi.
1. Wanajeshi kama watunza silaha na watu waliokuwa karibu kabisa na mlipuko siku ya tukio hawakuwa wanalinda maghala hayo
2. Wanajeshi walikuwa na perfect information juu ya ulipukaji wa mabomu hayo, yaani siku, saa na mahala patakapolipuka mabomu hayo
3. Kwa kuwa wanajeshi wao wamefundishwa mbinu za kujilinda na mabomu vitani haswa pale yanapolengwa kwao basi ni dhahiri kuwa wanajeshi walichukua tahadhari ya kujilinda na mabomu hayo hata kabla hayajalipuka vinginevyo yangewakuta kama wenzao wa Mbagala ambao hawakuwa na taarifa rasmi ya ujio wa milipuko
4. Wanajeshi walipoona yanakaribia kulipuka wakaamua kuingia kwenye mahandaki yao yaliyozagaa kambini na kuyaacha mabomu yalipuke mpaka yatakapotulia ndipo wakatoka na kutangaza wameyadhibiti.
Kama hayo yote hapo juu ndivyo ilivyokuwa basi ni dhahiri mlipuko huu ulikuwa ni wa makusudi na wenye lengo la kuwadhuru wananchi wasio na hatia ili kutimiza malengo fulani, kwa definition ya kuua raia wasio na hatia kwa malengo ya kisiasa, huu unastahili kuitwa ni UGAIDI japo si wakujitoa muhanga. Vinginevyo ni lazima out of control milipuko ianze na kudhuru from the source kabla ya kule yatakapotua mabomu hayo kama ni perimeter ya 10 kilometer au below.
Ndugu wanaJF kua kitu kinanishangaza, hivi katika milipuko ya mabomu Gongo la Mboto hakuna wanajeshi aliojeruhiwa na kufa? Mbona hatuambiwi?
Nashukuru Hofstede kwa kuungana nami ... HUU NI UGAIDI MKUBWA SANA. Ikiwa wanajeshi walijua mapema, naamini amiri Jeshi mkuu pia alijua, kwa nini haikuchukuliwa tahadhari? Kwanini wananchi waachwe wakifa na kuhangaika. Kulikuwa na uwezekano mkubwa kabisa wa kupunguza maafa hayo kwa kuwaonya wananchi mapema ili wahamishe familia zao, kuliko zile patashika za usiku.
Eti wao wanajua kuyakwepa!!!!
Ni siri za jeshi hizo. usipende kuzichimbua
Kufikia hitimisho haraka namna hii wengine tunapata wasiwasi, the motive behind andiko lako. Mimi nikuulize kama umeweza kuandika haya yote kwani usipate ushahidi hata wa mwanajeshi mmoja aliyekufa? Hawa wanajeshi wana ndugu, misiba yao lazima itawaguza na ndugu zao. Sasa unataka tuamini kuwa kunamwanajeshi amekufa ndugu zao na waliohudhuria msiba wake wote wafungwe mdomo na serikali wasiseme? Kwanini mbagala waseme kuwa wanajeshi wamekufa na gongolamboto waamue kuwa kimya? Wewe unataka tuamini kuwa wanajeshi wanaweza kukubali vifo vya wenzao viweze kutumika kwa maslahi ya mtu au kikundi cha watu? Pengine unaweza kuwafanya watu wengine kukuamini lakini sio mimi.
Wananchi wenzangu huu utamaduni wa kutokujiuzulu mtu hata iweje ni jambo ambalo tunalo nia ya dhati na uwezo pia wa kuubadili kwa kuchukua hatua sasa hivi.Tanzania will remain as Tanzania as it is! no body will act and you will never get the truth and there will be no consequences out of it!! it is sad and sickening! Mungu ibariki Tz!