Makomandoo wetu wa Tanzania

Tatizo maelezo yenu yote yanaelezea eti jinsi gani watatupa kipondo sisi ambao hatuna mafunzo yoyote pindi tuwachokozapo kama justification ya u-fit wao na kwa wote watakaothubutu ulimwenguni, ,duu!

KakaJahazi;
Ni kweli ulilosema. Maana sasa tutashindwa kuwatofautisha na mtu mwingine ambaye ana uwezo wa kupigana hata na watu 40 wote wakagwaya. Issue hapa ni je, when it comes kwenye maswala ambayo wamekuwa trained kwa ajili yake, wako fit? Ila mimi kwa upande mwingine nadhani kwenye ukommandoor kuna international standards ambazo bado zinazingatiwa in a strict sense kwamba komandoo wa hapa, US, Israel, India, Pakistan, n.k. hawawezi kutofautiana ujuzi, labda vifaa vya kutumia, na pengine hawa wa kwetu sababu ni watu wanaozaliwa kwenye mazingira magumu tangu wakiwa watoto mchanga, wanaweza kuwa wako fit zaidi kwenye fierce situations kuliko hata wale wa mataifa makubwa, sema tu wanaweza kuzidiwa vifaa vya kutumia, ila kama ni bare foot, bare handed, nadhani hapa tunao wanaoweza kummninya hata chui ukafikiri wanaminya paka!
 
mkuu usiwe na mashaka sana, vijana wako sawa kule hakuna siasa.
Lengo la maonyesho halikuwa kutisha watu, bali zaidi ni kusherehesha, na kunogesha sikukuu.

Kama hawa mabwana wakifanya vitu serious tegemea yafuatayo
1. Dar haitakalika
2. Majirani zetu na maadui + mataifa ya nje watajua yale wasiyotakiwa kujua

note: Wataalamu wa kijeshi wa mataifa wanaweza kuusoma mchezo kwa kumuangalia mwanajeshi jinsi anavyo tembea, shika siraha, ruka na kujua mengi kuhusu kikosi cahke haya lazima yazuliwe yasitoke nje

Kwa hiyo mlipokuwa mnavunja tofali kwa kichwa siku ile pale uwanja wa taifa, mlikuwa mna-send message gani kwa hao 'outsiders'?
 
Kwa hiyo mlipokuwa mnavunja tofali kwa kichwa siku ile pale uwanja wa taifa, mlikuwa mna-send message gani kwa hao 'outsiders'?

sema walipokuwa sio mlipokuwa (uliniona), bila shaka walikuwa wanataka kuwapunguzia wabongo stress za maisha na kuwapa raha bila shaka ulifurahi sana kwani mpaka leo unakumbuka,

omba Mungu uwepo tukifikisha Miaka 100, utaona mtu anatafuna chuma kwa meno, in short itakuwa zaidi ya mazingaombwe,

I WILL BE WAITING YOU THERE
@ 09/12/2061
 
kama hawapelekwi CUBA,CHINA,RUSSIA au US wapelekwe wakaongeze ma ujuzi maana kuna leo na kesho!
 
mkuu usiwe na mashaka sana, vijana wako sawa kule hakuna siasa.
Lengo la maonyesho halikuwa kutisha watu, bali zaidi ni kusherehesha, na kunogesha sikukuu.

Kama hawa mabwana wakifanya vitu serious tegemea yafuatayo
1. Dar haitakalika
2. Majirani zetu na maadui + mataifa ya nje watajua yale wasiyotakiwa kujua

note: Wataalamu wa kijeshi wa mataifa wanaweza kuusoma mchezo kwa kumuangalia mwanajeshi jinsi anavyo tembea, shika siraha, ruka na kujua mengi kuhusu kikosi cahke haya lazima yazuliwe yasitoke nje
QUOTE] Hiyo namba 2...'mataifa ya nje' mbona jeshi letu bado ni tegemezi ki technologia nk..miundombinu yake mingi ni ya kurithi kwa wakoloni..tunalo la kuwaficha kweli au porojo tu..viongozi wa jeshi wanaweka pesa ughaibuni, sijui kama siri za jeshi nazo ziko salama au?..
 
kuna wadau wangu wapo huko-mara ya mwisho kukutana naye hapo mdaula alikuwa ametoka mkoa wa pwani kwenye mafunzo waliyokuwa wakifanya pamoja na US army-AFRICOM,
 
tusubiri siku ya mechi(vita) ndio tutaelewa weledi wa makomando wetu.

Mkuu sisi waTZ tuendelee na kilimo kwanza chetu, mambo ya vita hatuyawezi. JWTZ lilikuwa 'Jeshi' enzi za Nyerere. Lkn sasa hivi wamekuwa manyang'au tu, wamekuwa wezi, majambazi na mafisadi, weledi wa jeshi haupo tena. Si unakumbuka Lt. Gen. Shimbo alivyokutwa na 3tril... Je, amezitoa wapi. Shimbo ni 'Chief of Staff' wa Jeshi, afu anakuwa fisadi, unategemea kuna jeshi? Mfano mwingine, si unaona JK anavyokumbatia mafisadi, mwisho serikali inakuwa kama aina mwenye, sasa na jeshi sasa hivi liko liko kama serikali ya JK. Kwa hiyo ikitokea vita, tutapigwa kama wachumba, hatuna jeshi sisi...
 
Mkuu sisi waTZ tuendelee na kilimo kwanza chetu, mambo ya vita hatuyawezi. JWTZ lilikuwa 'Jeshi' enzi za Nyerere. Lkn sasa hivi wamekuwa manyang'au tu, wamekuwa wezi, majambazi na mafisadi, weledi wa jeshi haupo tena. Si unakumbuka Lt. Gen. Shimbo alivyokutwa na 3tril... Je, amezitoa wapi. Shimbo ni 'Chief of Staff' wa Jeshi, afu anakuwa fisadi, unategemea kuna jeshi? Mfano mwingine, si unaona JK anavyokumbatia mafisadi, mwisho serikali inakuwa kama aina mwenye, sasa na jeshi sasa hivi liko liko kama serikali ya JK. Kwa hiyo ikitokea vita, tutapigwa kama wachumba, hatuna jeshi sisi...

Ushaamua kupiga makombora kwa baba ritz? Weye noma.
 
bila shaka utakua moja wao maana badala ya kunifafanulia with facts kama wenzako wewe unanitisha!!!

Makwarukwaru hujatishwa umeambiwa ukweli au kwa lugha nyingine jambo ulilwta halistahili kujadiliwa humu linahusu usalama wa nchi siyo kila unachofikiri lazima ukiandike pata sifa za hao watu kupitia mazungumzo ya kawaida na watu mbalimbali siyo uanike kila kitu humu hatuendi hivyo baba.
 
makomandoo wetu wamepata mafunzo ya kutosha na wapo imara hawawezi kuonesha hadharani ujuzi wao wote kwani majirani wataona na kujua level ya ujuzi wao na inaweza hatarisha usalama wa nchi yetu ndio maana siku zote huwezi kuwasikia ovyo ovyo ila hujifunza ndani na je ya nchi pia hata nchi rafiki wanajua kuwa tuna jeshi makini na makomandoo pia tunao makini.
ila nawaombea wasichakachuliwe na wanasiasa na kutumika ndivyosivyo.
 
Kwa kweli nimeamini waswahili hatukosi la kusema hata kama ni vitu serious kama ulinzi tunajikosoa wenyewe yaani dahh si mchezo.

Labda nieleze kwa uwelewa wangu mdogo tu kuwa unavyozunguzia komandoo unazumzia mlinzi maalumu mwenye kila aina ya mafunzo ya kivita na siyo kama profesa ambaye amespecialize labda kwenye mifupa au siasa au geography au vinginevyo. Hivyo ili kupata mafunzo ya aina zote ni lazima aende sehemu mbalimbali kujifunza namna ya kujilinda kulinda nchi kwa mwili, mabomu, akili na propaganda. Hivi vyote ni lazima uwe navyo na ndiyo maana wataalamu wa vita wansema komando mmoja ni sawa na wanajeshi wa kawaida 1000. Amefuzu katika anga, majini, ardhini, misako, intelgence na all maujana ya ukombozi na ndiyo maana tuliona wapo wanajeshi zaidi laki moja afghanistan lazi walitumwa makomandoo at most 10 tu kumtoa roho osama na hiyo ni kwasababu yule bwana ni field mashal ambaye ni hatari kuliko komandoo mwenyewe ujue. Wewe unasema kuvunja tofali badala na kuona wale vijana kam 15 waliopita wamevaa kofia kama majani walivyo wakakamavu, waliokua wanapitisha ndege kutoa saluti wanaizungusha hapo juu inabinuka hukuona?

Ndugu yangu nafikiri tuache kujidharau tujiamini na cha msingi ni kushauri kujitanua zaidi kutumia jeshi letu na idara ya usalama wa taifa kuijenga nchi kupambana na uwizi wa mali ya umma na ulaghai wa wanasiaga wa kuivuruga nchi badala ya kusubiri mambo ya haribike ndiyo waingilie kati kwa coup.
 
hao makomandoo wa bongo muwasikie tu hvyo hvyo wanafanya mazoezi ya hatari me nna mdogo wangu alichaguliwa akaenda morogoro kapigishwa zoezi kajua akitoka kule full komandoo atapata angalau bawa moja kamaliza mafunzo karudi home hoi kaambulia kofia nyekundu anaambiwa hyo basic training,mbona kaacha jeshi sasa hv anamalizia degree ya uhasibu kaona arudi shule hao watu ni hatari.
 
Ivi na wale wanao mzungukaga jk ambao mara nying unakuta wamevaa suti nyeusi,nao ni makomando au askari wa kawaida?
 
Wakuu wengi mmekuwa mkielezea jinsi gani hao makomandoo walivyofit ukilinganisha na mtu wa kawaida anayeshinda baa kula bia na nyama choma tu hata ukiampa mechi ya kitandani anachemka,Mi nadhani tupaswa kuwalinganisha na makomandoo wenzao wa nchi nyingine na kwa vile ni ngumu kupata facts ya wa nchi nyingine basi kuwaongelea hawa ni porojo za vijiweni tu.Tukizungumzia ufit wa jeshi kiujumla mimi nina wasiwasi sana na jeshi letu kutokana na serikali legelege tuliyokuwa nayo # commander in chief legelege na ukijumlisha na ukosefu wa uzalendo tuliokuwa nao kuna wajeda wengi tu wanaweza kula kona kikiwaka,sidhani kama tunaweza kusimama na kagame sasa hivi au Wakenya wenye vifaa vya kisasa sana (military expenditure yao kwenye kununua silaha ni x 10 ya kwetu) uimara ya jeshi/Makomandoo enzi za leo ni teknolojia sio uwezo wa kuvunja vyuma/matofali kwa vichwa na ukizingatia ufisadi mkubwa uliokuwepo sasa hivi na usiri wa ununuzi wa silaha jeshini sina shaka kuwa hizo hela huwa zinaishia kwenye accounts za akina shimbo na mwamunyange na kujenga magorofa badala ya kununua silaha au kununua sub-standards silaha.NI BORA TUJIFANYE KUWA BUSY NA KILIMO KWANZA NA KUOMBA TUSIVAMIWE HATUNA JESHI SASAHIVI NA WALA HATUNA SERIKALI IMARA LET'S CHANGE OUR POLITICS FIRST
 
Napata ukakasi sana hasa nikiwaza hichi kitu.Komandoo ni askari aliepitia mafunzo ya kijeshi na ya hali ya juu mno.

Zamani ilikua ukisikia komamdoo mpaka damu inasisimka na wengi wao katika jeshi letu walikua wanapata mafunzo yao nje ya nchi kama Cuba,Misri na Israel.Je sasa hawa wanaotoka pale Morogoro wana sifa kama zile za wale?

Au ndo wale waliotufanyia show ya kupasua tofali kwa kichwa pale uwanja wa taifa siku ya miaka 50 ya kupata bendera(kwani siamini kama bado tuko huru)?

Vita zenyewe ziko wapi Siku hizi? Tukiwapeleka nje wanatumalizia hela tuu. Bora tuwape "MalandCuiser" watulie hapa hapa. Kimyaaa!
 
mi nimepitia madojo si rasmi tokea enzi za miaka 80 -kwa watu wa dar watawakumbuka akina kiringo , Santana , (MwambaZero Jimmy Castro- marehemu hawa )Abdala Master sikuwa na rank yeyote zaidi ya kuwa najua kutifua ugomvi wa haja, miaka ya mbele uzeeni kwangu nika kutana ni vijana na mikanda yao kamasi ziliwatoka nawengine wakijidai wamechukua mafunzo kutoka nje au walimu wa nje.
Mikwara mbuzi tu hiyo!!
 
KakaJahazi;
Ni kweli ulilosema. Maana sasa tutashindwa kuwatofautisha na mtu mwingine ambaye ana uwezo wa kupigana hata na watu 40 wote wakagwaya. Issue hapa ni je, when it comes kwenye maswala ambayo wamekuwa trained kwa ajili yake, wako fit? Ila mimi kwa upande mwingine nadhani kwenye ukommandoor kuna international standards ambazo bado zinazingatiwa in a strict sense kwamba komandoo wa hapa, US, Israel, India, Pakistan, n.k. hawawezi kutofautiana ujuzi, labda vifaa vya kutumia, na pengine hawa wa kwetu sababu ni watu wanaozaliwa kwenye mazingira magumu tangu wakiwa watoto mchanga, wanaweza kuwa wako fit zaidi kwenye fierce situations kuliko hata wale wa mataifa makubwa, sema tu wanaweza kuzidiwa vifaa vya kutumia, ila kama ni bare foot, bare handed, nadhani hapa tunao wanaoweza kummninya hata chui ukafikiri wanaminya paka!

masikhara kwenye mambo ya msingi nakuomba sana sana sana sana.kwa jina la mungu uache!!i have come face to face with that thing....u dont know how it feels kukutana nalo na kwamba linaweza kukutafuna just like that!wacha kabisa bana wwe!
 
Wakuu wengi mmekuwa mkielezea jinsi gani hao makomandoo walivyofit ukilinganisha na mtu wa kawaida...

Huu ni mlinganisho potofu, kupasua jiwe kwa kichwa bila ya mbinu nyingine za kisasa za kupigana iwe ana kwa ana au kwa vifaa ni bure..wanaweza kuwa wanafundishwa kutafuna mawe lakini wakikutana na makomandoo wenzao wanachakazwa kama watoto..kuna kisa cha komandoo mmoja alifariki dunia kule Comoro kwa kushindwa kuogelea ni moja ya mifano ya kutokung'ang'ania kupasua mawe kwa vichwa wakati mahitaji ya kikomandoo ni zaidi ya hapo..!
 
Back
Top Bottom