MAKINDA: Swala la Lema sitalirudisha bungeni (Amehofia nini?)

Kwa huu mwelekeo mjengo utabinafsihwa bila ya sisi kujua, na wahusika watapeleka maelezo kwenye hardcopy
 
[Usitake ionakane wanawake hawawezi Mheshimiwa!!]

LD tatizo hapa si makinda kuwa mwanamke, labda hujaguswa au hujaelewa kinachoongelewa katika hii mada, Naomba urudie kuisoma upya. wanaongelea kushindwa kuongoza bunge kwa spika na si mwanamke Anne!!!!
 
Hapo kwenye RED, kama huo ndo uwongo wenyewe wa PINDA basi tunapoteza muda hapa. Na ni bora kodi yangu isitumike kujadili huo utumbo! NImekuwa nikiuliza mara kwa mara hapa Pinda kadanganya nini, kumbe ni Kusema Chadema ndio chanzo cha vurugu Arusha! Mbona huo ni ukweli tu. Chadema wanaandama agains agizo halali la polisi, polisi wanawazui kwa kutumia nguvu, vurugu zinatokea! Sasa hapo chanzo ni nani kama sio Chadema! Acheni ushabiki wa KIPUUZI!
We Jesuit ni bongo lala kweli kweli. Hujui PM kadanganya nini???????? Kama ni hivyo akili yako inafanya kazi kwa limoti, unajazwa ujinga unamwaga hapa jamvini!!!!!!!!
Ebu jiulize kwa nini Spika anasita kuanika taarifa ya Mpambanaji Lema bungeni kweupe????? Anataka kupotezea eti atamaliza mwenyewe, hapo tena hujajua ukweli uko wapi.
Bado huamini PM alisema uongo??????????
 
Huyu mama alikurupuka
So let us see what will happen next , Sijui ataliamaliza vipi akiwa na Lema na Pinda au kimya kimya Ikiwa ni kimya kimya CHADEMA watahoji amelimaliza vipi labda kwa kuangalia kanuni za bunge zinasemaji ikiwa suala lilianzia bungeni na Spika akaamua kilichinjia baharini bila taarifa
 
wamegundua kuwa PM hakuwa na data sahihi, sasa lazima wamlinde.
 
Usitake ionakane wanawake hawawezi Mheshimiwa!!

Sidhani kama ndugu yangu anazungumzia au kuhusisha jinsia katika hili. Hapa linalozungumziwa ni uwezo wa mtu kiutendaji hasa katika nyanja ya uongozi makini na wenye maamuzi sahihi. Kwa hiyo usihofu kwa hilo. Huenda hata Eng Manyanya angeongoza bora zaidi kuliko aliyeko sasa
 
MAKINDA alaumiwi kwa sababu ya uanamke wake, tatizo la MAKINDA anaweka maslahi ya chama na kundi fulani ndani ya chama chao mbele kuliko Maslahi ya UMMA. Uwezo wa kuongoza anao lakini KIATU cha mahaba na upendeleo AKIVUE. Amasivyo itaonekana USPIKA ni cheo kizlicho mzidi uwezo. Haiwezekani mama kakaa BUNGENI zaidi ya miaka 30 hajanye mambo ambayo MBUNGE aliye na asiyezidi miezi mitatu MNYIKA ambaini kuwa anachemsha, yeye kaombwa muongozo badala ya kutoa muongozo anatoa karipio na kutaka uthibitisho, Sasa kulielewa hili inataka uwe mwanaume? kwa sasa mimi naamini ni mapenzi kwa CHAMA chake kuliko nchi yake ndiko kunamfanya apotoke, lakini akiendelea ni wazi itajidhihirisha kuwa si mapenzi kwa chama chake bali uwezo na uelewa mdogo alionao ndio tatizo limsumbualo.

Kumbuka PM ni mbunge kama wenzake bahati yake ni kuwa Rais kamteua kuwa PM hivyo kama mbunge anadanganya kwa nini PM nae asiweze kudanganya? je na hili inabidi uwe mwanaume kulitambua?

Kumbuka kazi ya wabunge ni kuwawakilisha wananchi kuidadisi serikali mambo mbalimbali yausuyo maslahi ya wananchi hao na Taifa kwa Ujumla, kinadharia kauli ya MBUNGE ni kauli ya wananchi wa JIMBO lake, lakini kiuhalisia kauli ya PM Bungeni ni kauli ya Serikali. Sasa Bunge anapotekeleza jukumu lake la kuihoji serikali kuhusiana na wananchi wa jimbo lake kuuwawa na serikali halafu PM anatoa jibu lisilo sahihi, MBUNGE kuhoji kama kiongozi mkubwa akipotosha/kudanganya nini kinafanyaika ni kosa?

MAKINDA anasema PM ni kiongozi mkubwa na anayepaswa kuheshimiwa, Hilo ni sahihi kabisa, lakini anayepaswa kuheshimiwa ni lazima na yeye hajiheshimu pia na kuheshimu wenzake, sijui kama kulielewa suala hilo linahitaji uwe mwanaume?

Kama PM kashindwa kujieshimu na kuwatungia uongo wenzake, kuhoji ni hatua gani inapaswa kuchukuliwa juu yake ni kosa la kukemewa?

Tatizo hapa si jinsia ya Mama MAKINDA, watu wanachohoji ni uwezo wake ktk kuliongoza BUNGE, Yupo mama HILLARY CLINTON, MAMA ROSE MIGILLO, Mama SHORTY wa UK aliyetupigania tusiumizwe kuhusu RADA nk MBONA ni wanawake lakini wameonyesha uwezo wa juu?

Tatizo si jinsia tatizo uwezo wa kiutendaji wa mama MAKINDA

Ndg zangu tatizo hapa si jinsia, bali ni ufedhuri na uelewa ndogo changanya na nyodo ya jeuri ya mafisadi walio muweka hapo alipo.

Mbona former Speaker wa USA Nany Pelosi aliperform vizuri tuu.

Huyu Anna Makinda ni mjeuri na mjinga, analinda maslahi ya mafisadi.

Ulitegemea nini baada ya kuona Mzee Six akingolewa??????????Si ni mipango ya muda mrefu ya mafisadi na SISIEMU kuliteka bunge????????? Lakini sasa Watanzania tumeshituka hatutakubali jamani tuwashe moto wetu Jangwani kuonyesha kuwa hatukubali ujinga huo na dhuluma zao!!!!!!!!

moz-screenshot.png
moz-screenshot-1.png

 
.......Katika hali ya kawaida, spika hapaswi kudharau magazeti, kwani hata kufika kwake hapo kwa njia moja au nyingine kumechangiwa kwa kiasi kikubwa na vyombo vya habari mbalimbali yakiwamo magazeti anayoyaita barua.[/COLOR]
Leo itakuwa ajabu kwa spika kutoa lugha za kebehi kuwa hawezi kufanya kazi kupitia magazeti ambayo anayaona kuwa sawa na barua.......

mkuu...pole sana kwa maumivu..

huyu mama ni zero minus...

hivi unakumbuka alisemaje aliposhutumiwa kuwa amewekwa hapo kwa nguvu za mafisadi????

alikanusha na kusema bungeni hakuna mafisadi kwani kwa ufahamu wake...fisadi ni mtu(mwanaume) anaetembea na wake za watu...

she is kichekesho kwa kimombo...:laugh:
 
Katika hili Spika Makinda umelikoroga
ban.mtazamo.jpg

Shehe Semtawa

amka2.gif
KUCHAGULIWA kwa Spika wa Bunge, Anne Makinda, kulizua mabishano kutoka kwa wadau mbalimbali kuwa asingeweza kuongoza Bunge hilo, kwa kile kilichoelezwa kuwa jazba alizonazo zingeshindwa kuamua mambo ya msingi.
Spika huyu amerithishwa nafasi hiyo kutoka kwa aliyemtangulia, Samuel Sitta, ambaye alionekana kukubalika miongoni mwa jamii kutokana na uendeshaji wake wa Bunge lililopita.
Kabla hata ya kufikia nusu ya mwaka tangu kuanza kwake kazi, spika huyu amekuwa akionyesha dosari mbalimbali katika kusimamia vikao vya Bunge, kitu ambacho kinawapa nafasi waliokuwa wakimpinga kupata nguvu ya kudhihirisha maneno yao ya awali.
Makinda, anatumia vibaya kiti chake kwa kudhani kuwa yeye ni mwelewa wa kila kitu kuliko wengine, wakati sivyo, kwani wapo wengi wenye uwezo wa kufanya kazi ile.
Atambue kuwa huu si wakati wa kuburuzana, kwani kila mmoja katika nchi hii ana haki ya kujieleza ili mradi hakuna kitendo chochote kinachoashiria uvunjifu wa amani katika yale yatakayoelezwa.
Tukio la spika Makinda la hivi karibuni kuyaita magazeti kuwa ni sawa na barua hivyo hawezi kufanya kazi kwa kuyaamini, si la busara.
Hatua ya Spika huyo kutamka maneno hayo ilifanyika baada ya mwandishi wa gazeti moja la kila siku kutoa maoni yake gazetini kuhusu staili ya uongozi wa spika huyo katika chombo hicho.
Kwa hili nadhani Spika Makinda hakutenda haki kwa waandishi wa habari pia inasikitisha kwa mtu mweledi kama yeye kushindwa kutofautisha barua na gazeti.
Kwa kumsaidia kidogo, barua ni taarifa inayoandikwa na mtu mmoja bila kupitiwa na zaidi ya mtu mmoja kwenda kwa mwingine, hiki ni kitendo cha mawasiliano kati ya mtu na mtu na si vinginevyo.
Wakati gazeti ni chombo ambacho kinaongozwa na kundi la watu ambao wana taaluma ya uandishi wa habari ambayo ina miiko yake kikazi.
Ni wajibu wa spika kuelewa kuwa kwenye vyombo vya habari hakuna kukurupuka bali kila kinachoandikwa huwa kinapembuliwa kwa lengo la kuielimisha jamii kinachotokea.
Nashindwa kuamini kuwa spika kweli hajui maana halisi ya gazeti ambalo huwa linakuwa na safu kama maoni ya mhariri, makala za mahojiano, uchambuzi wa nyanja mbalimbali, habari za michezo na burudani, mashairi na hata barua za wasomaji na mambo kadha wa kadha.
Kama kweli havielewi hivi basi nadhani umefika wakati yeye kutambua kuwa kuna vitu hivyo ambavyo vinatumia katika nyakati mbalimbali katika magazeti.
Ni wakati pia kwake kuitambua vizuri tasnia hii ya habari kuwa ni pana, kinyume na anavyoifikiri pamoja na wengine, wakiwemo baadhi ya wanasiasa.
Hata hivyo, anaweza kutusaidia katika kusoma kwake kama aliwahi kufundishwa na walimu aliyokutana nao kuwa gazeti ni barua, atuambie.
Uandishi wa habari ni fani iliyotukuta na yenye kuaminika miongoni mwa jamii kutokana na kuibua mambo mbalimbali ikiwamo ufisadi kinyume inavyotazamwa na kuchafuliwa na watu wachache wasiopenda kufuata maadili ya kazi zao na haki za wengine.
Katika hali ya kawaida, spika hapaswi kudharau magazeti, kwani hata kufika kwake hapo kwa njia moja au nyingine kumechangiwa kwa kiasi kikubwa na vyombo vya habari mbalimbali yakiwamo magazeti anayoyaita barua.
Leo itakuwa ajabu kwa spika kutoa lugha za kebehi kuwa hawezi kufanya kazi kupitia magazeti ambayo anayaona kuwa sawa na barua.
Kwa hili ukiwa kama mwanadamu kubali umepotoka na huna budi kuomba radhi.
Kwa mtazamo wangu, sitaki nikuone kuwa wewe ni bora kiongozi, bali nataka uwe kiongozi bora, hivyo ni vema kuacha kuwadharau wale ambao hawajaonyesha dharau katika kazi zako ambazo kwa kiasi kikubwa zinahitaji msaada wa wana habari.
Ukiwa kiongozi wa wananchi unapaswa kuwa mvumilivu pale unapo kosolewa kwani kama ungekaa nyumbani kwako hakuna ambaye angejaribu kukuelekeza jinsi ya kufanya kazi kwa kufuata kanuni.
Si vizuri kuingia kwenye mgogoro na wanahabari hadi kufikia hatua ambayo huko nyuma iliwahi kutokea kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Omar Mapuri.
Kwa kuwa Bunge hili ni fupi, bado unao muda wa kutoa tamko kuhusiana na kauli yako ile ambayo kwa kiasi kikubwa haikubaliki kwa tasnia ya habari.

1. Kama ni mweledi kweli kama ulivyosema, ataomba radhi. Tena iwe bungeni huko huko na watu wote tusikie.

2. Waandishi wa habari mmechangia sana kuwapamba watu hata wasiotufaa. Kwa hiyo ni matunda ya kazi yenu. Mwenyewe umesema vyombo vya habari ndio vimemfikisha hapo alipo.
 
pm yuko sahihi kabisa na hakusema uwongo, nyie chadema mliisha pewa agizo la kuacha maandamo, kwa utovu wenu wa nidhamu, kujitafutia umaarufu kwa gharama za maisha ya watu na kujifanya wajuzi kama sio wajuvi, ndiko kuliko sababisha mauaji na vurugu za arusha.

crap....
 
PM yuko sahihi kabisa na hakusema uwongo, nyie CHADEMA mliisha pewa agizo la kuacha maandamo, kwa utovu wenu wa nidhamu, kujitafutia umaarufu kwa gharama za maisha ya watu na kujifanya wajuzi kama sio wajuvi, ndiko kuliko sababisha mauaji na vurugu za Arusha.

wewe mdau ni mama Makinda! Mbona unajionyesha F zako.
 
Mbona huu ni mwanzo tu! Tutegemee pumba na under-perfomance zaidi kutoka kwa huyu bibi. Siku zote mtu aliyewekwa kwa maslahi fulani hawezi kuwa na chochote cha ziada zaidi ya kuvuruga utaratibu ili kuwafurahisha kina nanii. Tutamkumbuka sana chuma cha pua.
 
Mie nashindwa kumjaji kwa kweli maana kilema chake kwangu ni kikubwa sana .......sijui wapi pa kumwanzia.
Poor Tanzania sijui ni taifa lililolaaniwa?? Mbona kila kona ni uozo tu??:sick:
 
Kwa kuwa mpaka sasa hivi Lema hajapewa mwongozo wa Spika kuhusu utaratibu inapotokea mtu mzito kama Pinda kulidanganya bunge, Makinda hana namna, atabanwa atoe mwongozo na hapo haiwezi kuwa sehemu nyingine ispokuwa ndani ya bunge.
 
PM yuko sahihi kabisa na hakusema uwongo, nyie CHADEMA mliisha pewa agizo la kuacha maandamo, kwa utovu wenu wa nidhamu, kujitafutia umaarufu kwa gharama za maisha ya watu na kujifanya wajuzi kama sio wajuvi, ndiko kuliko sababisha mauaji na vurugu za Arusha.

Kweli kabisa! Hapo umenena! CHADEMA hasa ndio walisababisha hiyo tafrani ya Arusha. Pia kuna ushahidi dhahiri kwamba CHADEMA imekuwa ikila njama na wafanyabiashara ili bei za vitu mbalimbali zipande, JK na CCM waonekane hawafanyi kazi. ni wazi pia wao ndio wanachochea migomo vyuo vyote vilivyogoma. na pia kuna watu wao kule hazina wanakula njama mishahara icheleweshwe ili wafanyakazi nao wagome! yaani we acha tu, hawa CHADEMA! unajua hata kule DAWASA wamejiingiza, maji hayapatikani. hata kule Mtera, walikula njama na yule jamaa anayefungulia bwawa, maji kayafungulia yamekwisha yoote! ndio huu mgao wa umeme unatuumiza. nimepata tetesi hata hii milipuko ina mkono wa CHADEMA! nadhani tuilaani CHADEMA na tuandamane ili ifutwe kwenye daftari ya msajili wa vyama, baada ya hapo nadhani tutaishi raha mustarehe na Maisha bora kwa kila mtanzania yatawezekana!
 
PM yuko sahihi kabisa na hakusema uwongo, nyie CHADEMA mliisha pewa agizo la kuacha maandamo, kwa utovu wenu wa nidhamu, kujitafutia umaarufu kwa gharama za maisha ya watu na kujifanya wajuzi kama sio wajuvi, ndiko kuliko sababisha mauaji na vurugu za Arusha.

Ubongo matope
 
Asipoacha Ukurupukaji,bunge litamfukunyua na kumgagadua,hatimaye umaarufu anaotaka ataambulia "ufuliaji". Akichakachua tu, atajikuta ni Spika wa kwanza kusababisha uvunjifu wa Amani Bungeni na Tanzania kwa Ujumla. Aluta continua Godbless Lema!
 
PM yuko sahihi kabisa na hakusema uwongo, nyie CHADEMA mliisha pewa agizo la kuacha maandamo, kwa utovu wenu wa nidhamu, kujitafutia umaarufu kwa gharama za maisha ya watu na kujifanya wajuzi kama sio wajuvi, ndiko kuliko sababisha mauaji na vurugu za Arusha.

Yuko sahihi au hayuko sahihi siyo kinachojadiliwa hapa. Aliombwa mwongozo. Angetoa mwogozo kisha aendelee na taratibu nyingine yeye akarukia kwenye conclusion. Chadema na serikali wanatofautiana kuhusu mauaji ya Arusha hivyo kusoma taarifa ya Lema atawezaje kupembua ukweli uko wapi wakati ule wa Pinda hakuupata kwa maandishi na in details?

All in All huyu mama ana FFFFFFF ya confidence, anakurupuka sana na ni mjuaji. Ndiyo maana alikuwa akizozana sana na Zitto wakati akiwa Naibu Spika kutokana na kukurupuka. Sasa kaanza malumbano na vyombo vya habari. Yeye ni kiongozi kama anaona hataweka taarifa kwenye vyombo vya habari waambie unaongozwa na kanuni na umeona the best way ni A, B, C kejeli kwa vyombo vya habari za kazi gani?
 
Kweli kabisa! Hapo umenena! CHADEMA hasa ndio walisababisha hiyo tafrani ya Arusha. Pia kuna ushahidi dhahiri kwamba CHADEMA imekuwa ikila njama na wafanyabiashara ili bei za vitu mbalimbali zipande, JK na CCM waonekane hawafanyi kazi. ni wazi pia wao ndio wanachochea migomo vyuo vyote vilivyogoma. na pia kuna watu wao kule hazina wanakula njama mishahara icheleweshwe ili wafanyakazi nao wagome! yaani we acha tu, hawa CHADEMA! unajua hata kule DAWASA wamejiingiza, maji hayapatikani. hata kule Mtera, walikula njama na yule jamaa anayefungulia bwawa, maji kayafungulia yamekwisha yoote! ndio huu mgao wa umeme unatuumiza. nimepata tetesi hata hii milipuko ina mkono wa CHADEMA! nadhani tuilaani CHADEMA na tuandamane ili ifutwe kwenye daftari ya msajili wa vyama, baada ya hapo nadhani tutaishi raha mustarehe na Maisha bora kwa kila mtanzania yatawezekana!

Hao jamaa huwa wanaonyesha pumba zao waonekane pia wapo!

Yote haya umeyaandika kudhihirisha kuna ombwe la uongozi. Umewajibu vizuri kabisa kwani siyokitu kimoja tu wanapindisha ili wawe salama
1. Serikali imefanya nini kudhibiti mfumuko wa bei? Wanaopandisha bei makusudi imewafanyia nini? tafsiri yangu ni weak Government
2. Wanafunzi wanagoma bila sababu za msingi? Migomo inaonekana ni uhaini wakati ni kutoa yale ambayo watu wengi hawayaoni. Tafuta sababu za migomo ujue kama siyo mambo yanayohitaji kuwajibishwa kwa watu badala ya kuwafukuza wagomaji. Tafsiri yangu ni weak government
3. Kucheleweshwa kwa mishahara kwangu ni weak Government
4. Maji kutokupatikana ni tatizo la upinzani? basi na mabomu pia ni wapinzani. Hiyo pia jibu ni weak government
5. na matatizo chungu mzima

Ndugu Mindi tuendelee tu kuwaambia udhaifu wa serikali whether they like or not
 
Back
Top Bottom