Prophet
JF-Expert Member
- Aug 31, 2010
- 274
- 124
wanamshangaa kwa jinsi anavyoliongoza bunge, hawajui wasifu wake.
wanapandwa jazba kwa kudhani anakosea sheria, hawajasoma wasifu wake.
wanaacha kufuatilia kinachoendelea ndani ya vikao vya bunge, eti limekosa umaarufu wake wa zamani, hawajafuatilia wasifu wa huyu mama.
Eti na TBC1 wanaona wanapoteza muda kurusha matangazo yasiyo na waangaliaji wengi. Walimnadi wakati wa uteuzi/uchaguzi wakiwa wameruka vipengele muhimu vya wasifu wake.
Wasifu wake unajieleza, Mh. Msekwa amemaliza kabisaaaa kwa kuusoma hadhalani. Kiongozi wa kutunga sheria asiye mwanasheria. Wabunge watunga sheria kutokuwa wanasheria si tatizo, ila kiongozi wao lazima azijue sheria hizo tena kwa vyeti vinavyoonesha kuwa anaweza. Kama hii si hoja basi katika vyeti vyetu viwe vinapata update ya kufudhu taaluma fulani kwa kigezo cha UZOEFU na si ufaulu wa mitihani. Hivi ndivyo spika wetu anavyotaka hali iwe.
Uwepo wa mwanasheria mkuu bungeni si hoja kulingana na majukumu aliyonayo pale bungeni. Ukweli utasimama daima kama alivyosema Shaaban Robert katika shairi lake la Ukweli (kama sijakosea, ila sintajuta kama nitakuwa nimekosea kwa kuingilia fani za kina mpoto).
Ukweli huo ni kuwa kiongozi wa watunga sheria awe mwanasheria, muongoza njia lazima aijue njia. Hata siku moja hautaweza kutunga kitabu (Novel) eti kwakuwa umesoma novel nyingi sana, wala huwezi kuongoza filamu kwa kigezo tu cha kuwa mteja mzuri wa cinemax na alibaba.
Ukibisha angalia bongo movies na linganisha na huko ambapo kuliwafanya waamini kuwa hata wao wataweza bila ya kuliona darasa hata moja la tasnia ya filamu.
Makinda kubali yaishe, kila mtu anajua upo hapo kishabiki tu na nidhamu ya woga ya Chamachetu cha mapambo chajenga wizi.
wanapandwa jazba kwa kudhani anakosea sheria, hawajasoma wasifu wake.
wanaacha kufuatilia kinachoendelea ndani ya vikao vya bunge, eti limekosa umaarufu wake wa zamani, hawajafuatilia wasifu wa huyu mama.
Eti na TBC1 wanaona wanapoteza muda kurusha matangazo yasiyo na waangaliaji wengi. Walimnadi wakati wa uteuzi/uchaguzi wakiwa wameruka vipengele muhimu vya wasifu wake.
Wasifu wake unajieleza, Mh. Msekwa amemaliza kabisaaaa kwa kuusoma hadhalani. Kiongozi wa kutunga sheria asiye mwanasheria. Wabunge watunga sheria kutokuwa wanasheria si tatizo, ila kiongozi wao lazima azijue sheria hizo tena kwa vyeti vinavyoonesha kuwa anaweza. Kama hii si hoja basi katika vyeti vyetu viwe vinapata update ya kufudhu taaluma fulani kwa kigezo cha UZOEFU na si ufaulu wa mitihani. Hivi ndivyo spika wetu anavyotaka hali iwe.
Uwepo wa mwanasheria mkuu bungeni si hoja kulingana na majukumu aliyonayo pale bungeni. Ukweli utasimama daima kama alivyosema Shaaban Robert katika shairi lake la Ukweli (kama sijakosea, ila sintajuta kama nitakuwa nimekosea kwa kuingilia fani za kina mpoto).
Ukweli huo ni kuwa kiongozi wa watunga sheria awe mwanasheria, muongoza njia lazima aijue njia. Hata siku moja hautaweza kutunga kitabu (Novel) eti kwakuwa umesoma novel nyingi sana, wala huwezi kuongoza filamu kwa kigezo tu cha kuwa mteja mzuri wa cinemax na alibaba.
Ukibisha angalia bongo movies na linganisha na huko ambapo kuliwafanya waamini kuwa hata wao wataweza bila ya kuliona darasa hata moja la tasnia ya filamu.
Makinda kubali yaishe, kila mtu anajua upo hapo kishabiki tu na nidhamu ya woga ya Chamachetu cha mapambo chajenga wizi.