Makazi Ya Polisi Rombo - Miaka 50 ya Uhuru

Madish kwenye paa yanatupa hali binafisi ya kifedha hao polisi. Sidhani kama hayo madish watakuwa wamewekewa na serikali. Tanzania watu sio maskini, serikali ndio maskini.
 
Sidhani kama watawala wanaweza wakawajali sana hata kufikiria kuwajengea nyumba zenye hadhi ya kuishi binadamu kwa sababu chochote watakachowatuma kufanya wanakifanya bila kinyongo kwa kisingizio kwamba ni amri kutoka juu kwa wakubwa. Inawezekana hata kuishi humo nayo ni amri kutoka juu kwa wakubwa hivyo ni lazima waikubali na kuitii!
 
Duh hii ni balaa
Bora hata hawa ni mbao hazina joto sana
Nenda Arusha pale uone watu wanavyoishi kwenye nyumba za bati full kuanzia chini mpaka juu na fikiria lile joto la bati mchana ila utamkuta polisi anapikia humo humo ndani

Na kipindi cha baridi ya A town yanadondosha maji kama freezer,
 
Sidhani kama watawala wanaweza wakawajali sana hata kufikiria kuwajengea nyumba zenye hadhi ya kuishi binadamu kwa sababu chochote watakachowatuma kufanya wanakifanya bila kinyongo kwa kisingizio kwamba ni amri kutoka juu kwa wakubwa. Inawezekana hata kuishi humo nayo ni amri kutoka juu kwa wakubwa hivyo ni lazima waikubali na kuitii!

cku moja nilikua internetcafe mzazi kaja kuangalia matokeo ya mwanae aliyemaliza f4 mwaka jana, akakuta kapata div 0,
akawa anamuuliza msimamizi pale ina maana hawezi kukubaliwa kujiunga hata Polisi?? watu waliokua busy na computers ghafla waliangua vicheko.
 
Kweli Polisi ni wa kuonea huruma! cha ajabu wapo mstari wa mbele kuwapiga virungu wanaowatetea na kuwalinda watawala wanaowafedhehesha na kuwadhalilisha kiasi hiki!! maisha gani haya wanaishi!
 
ila hao Askari wana hela balaa, wanashindana na wa-tunduma. Trust me i know them.

Hapo kwenye red; absolutely true. Polisi wa Rombo ni miongoni mwa watumishi wa umma matajiri zaidi Tanzania. Usishangae wanavyong'ang'ania kuishi kwenye hayo mabanda na madishi ya TV juu; wana majumba ya kifahari na mengine wanapangisha Moshi, Arusha, Marangu, Himo, na kwingineko.

Biashara ya magendo inayofanyika katika mpaka wa Tanzania - Kenya eneo la Rombo ni ya mabilioni ikianzia tangu bidhaa ndogo ndogo za mashambani kama mboga mboga hadi biashara ya "kuuza" watu - wasomali wanaoingia kila uchao hapa nchini kimagendo asilimia kubwa wanapitia Rombo na escort wanapatiwa na hao hao askari.

Kuna biashara kubwa kubwa pia - bidhaa za maliasili (mbao, wanyama pori), vifaa vya ujenzi (nondo, sementi, bati), vinywaji, biashara haramu ya kuvusha kahawa kimagendo, mahindi, sukari, na takataka zingine zote zinafanyika katika mpaka huo.

Kama ambavyo wewe kila siku unaomba siku ukifa ukamwone Mungu ndivyo askari polisi yeyote Tz anaomba apangiwe Rombo angalau kwa mwezi mmoja tu kabla hajafa. Customs za Holili, Tarakea, Kitobo, hadi Kamwanga ni balaa. Hushangai huyo jamaa (askari?) anayeonekana kwenye hiyo picha anavyoonekana mambo yake ni mazuri?
 
Ukiwakuta Four Way Bar opposite na NMB hutaamini wanavyokamata bia na mbuzi na Corolla zao wamepaki nje. Sio siri pamoja na kuishi kwenye hayo mabanda vijana wana pesa ya kutisha wanazopata kwenye dili za kuvusha mahindi na sukari kupeleka Kenya. Wengine wana nyumba zao binafsi na Noah kadhaa za kubeba abiria kwenda Moshi na Tarakea,

Mbona wanayafurahia maisha kama wapo peponi!!!!!!
dah mkuu umetaja four way nikakumbuka hom.....za rombo ni nzuri in comparison na maeneo mengne,they deserve this hadi watakapokubali changes.....
 
Hili ni moja ya majambo yanayochangia Polisi wetu kupiga ovyo raia. Frustration kibao, harufu yake mpaka kinywani na kwenye mavazi.
 
Labda wanaogopa wakiwapa nyumba nzuri watalala fofofo na kusahau majukumu yao ya kutulinda!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
hao polisi hata uwape kazi ingine ya milioni mbili kwa mwezi KATU HAWAKUBALI
waoneni hivyo hivyo hela wanapiga ile mbaya
 
Bwana Nyani Ngabu, tatizo ni kwamba hawa polisi ndio ambao hawataki kutengenezewa maisha mazuri. Walichagua wenyewe kuishi kama wanyama maana wakati wa kampeni mwaka jana, waliahidiwa maslahi mazuri, vitendea kazi vizuri nyumba bora za kuishi kwani sement na bati zingeshuka bei, lakini cha ajabu wakakataa kumuunga Dr. Slaa mkono. Mbaya zaidi ni hawa hawa wanasadikiwa kumsaidia Baba Ridhi kwa kuchakachua kura. Waliowasaidia wanapeta kwa kula kuku kwa mrija, na wao polisi wanaishi kwenye mabanda ya kuku. Wandelee kuteseka tuu kwanza mpaka akili ziwakae sawa..
Hii ni hali ya kawaida sana kwa askari wetu wengi tu na wala hakuna cha ajabu hapo.

Kama mtu ulikuwa hujui kuwa askari wa majeshi yetu ambao ni rank and file wanaishi maisha duni basi wewe huna mguso na hali halisi ilivyo Tanzania.
 
Wanapesa nyingi sana na mfumo huu unawabeba sana,what if wangekuwa hawaridhiki na huu mfumo!????ukiona kimya wamekaa kimyaaa ujue wamekubali niangusage!!!
 
Back
Top Bottom