Makapi ya CCM yanapokuwa ngano kwa CHADEMA

Mie sioni tatizo lolote kwa wanachama wa CCM walioenguliwa kimajungu (Kama ilivyomtokea Slaa kipindi kile), kuhamia vyama vya upinzani. Ila wasi wasi wangu, kuna baaadhi yao ni mamluki ambao wametumwa ili kuleta mtafaruku mzito katika kinyang'anyiro hiki. Yawezekana, wakapewa nafasi ya kuwakilisha chama chochote walichohamia katika upinzani halafu wakajitoa katika siku za mwisho, na kuwaletea fadhaa wananchi, wanachama na viongozi wa chama husika.

Due diligence inatakiwa sana kwa vyama hivi kuwafanyia watu hawa.

Tatizo lingine liko kwetu kwa wanajamvi ambao wengi wenu humu mnaweza kabisa kuingia katika Siasa lakini mmebaki mnapiga makelele nje tu, na kuacha nchi yetu inashikwa na wanyang'anyi. Tulitafakari hili, hata katika uchaguzi wa 2015.

Mapato ya vyama vya upinzani ni madogo sana (not quantified) hivyo kuweza kumudu kumsimamisha mtu makini katika kila jimbo ni kazi nzito, na ndio maana kuna sehemu utakuta hamna jinsi zaidi ya kuwakubali waliotemwa Sisiemu.

Mungu Ibariki Tanzania. Tutafika tu.
 
Siasa ni si Hasa waungwana. Opportunity haiji mara mbili. Kama mgombea hakutendewa haki na chama alichokuwamo na kisha kujiunga na chama kingine huku pia anakubalika kwa wananchi nadhani huo ni mtaji kwa chama kilichompokea. tena ukizingatia kua chama alichoingia hakikua na mgombea katika jimbo husika. Ujenzi wa nyumba haukuepushi na kuingia gharama. Refer Slaa alipojiunga Chadema na kuleta ushindi Karatu kisha tazama anavyowatesa CCM now
 
Mimi naomba kuelimishwa.
Ni nani anaye-set:
1. specifications za hilo chekecheke linalopembua makapi from ngano?
2. criteria ya kipi makapi na kipi ngano?

Hayo mambo mawili hapo juu ni very subjective na yanaweza ku-draw different schools of thought.
Kinachoonekana makapi kwa CCM kinaweza kuwa ngano kwa opposition. The converse is also true.
Nielimisheni tafadhali.
 
hivi huwa wanachukua makapi kwa sababu chama hakina uwezo wa kuzalisha ngano yake wenyewe?

sijaona bado mantiki ya kuchukua makapi kisha ukayapa thamani ya zaidi ya ngano yenyewe hata kama yanafaida.

hakuna Makapi bana, Thomas Nyimbo ni makapi, wakati amewamwaga wale wooote wapinzani wake......
kama kila Mtoka CCM ni makapi, BASI ccm YOTE NI MATAKATAKA TU, MAANA iwe ujiko ama ushujaa Tambwe Hiza, Lamwai, Amani Kabouru , Kurudi ccm IWE DHAMBI KWA WAPINZANI KUWAPOKEA KINA nYIMBO, Arcado Ntagazwa, Shibuda, je si heri kumsimamisha Shibuda kule kwao , kuliko kuacha Jimbo bila kumsimamisha mgombea, waacheni longolongo, wametoka kina Ngawaiya wamegeuka Lulu CCM.
 
Bahati mbaya huwezi kupata dona kutoka ktk ngano! Ktk ngano hakitupwi kitu hata zile pumba za majani yake hupewa farasi wakala.
Mkuu, nani kawaambia CCM ndiyo yenye chujio lisilo na matunde tena yakuwekwa kwa makusudi ili wale wembamba kifedha wadondoke na wale wanene kifedha wabaki?
Nani kasema mchujo wa CCM ndio mchujo wenye ubora, na kila ambaye akuchaguliwa na CCM basi ni makapi?..........This is a skewed thinking. Sawa na kufikiri kuwa kwa vile Chadema haijawahi kuwa serikalini basi ikiingia itabidi iweke mpaka wakurugenzi wapya ambao ni wa Chadema.
kuna ubaya gani kuwa unafikiri unaweza ku-workout issues zenu na mkeo, then dakika ya mwisho anakwambia mbona mi sina time na wewe, what do you do? keep crying? go get a life!!
 
ndio maana wachambuzi wa siasa wanasema Dr Slaa anafaa lakini ataundaje dola kwa watu wa kuazimaazima bila ya kuwajenga wafuasi wao muda marefu? Kila siku CHADEMA wanasema CCM ni mafisadi lakini ajabu wanapokea wagombea CCM bila hata kuwajua kwa undani.Bado naamini CHADEMA ni chama kizuri lakini hakijakomaa kukipa nchi. Kama leo Dr Slaa atashinda kuwa Rais hana watu wa kuunda serikali kwani kama CHADEMA wanathubutu kuokoteza wagombea wa nafasi mbalimbali bila mpangilio bila shaka wataokoteza watu wa kuunda serikali yao. Tuwape muda wa kujijenga zaidi.

Hivi chama kinakomaa namna gani? Yaani kiishi miaka 50 au ni mfumo bora! CCM inayoitwa imekomaa mbona sioni siasa za ukomavu? Tunaingia ktk mtego wa CCM kila wakati kujigamba wamekomaa wakati hawana hata itikadi ya kueleweka kwa miaka 10 iliyopita.

Kinachotakiwa ni personalities na mfumo mzuri wa kuwapata viongozi. Hata CCM hili limewashinda. Ndo maana hata vibaka wanachaguliwa kiurahisi tu! Mtu anakata kadi wiki ya kuchukuwa fomu, anashinda na baadaye ni waziri. Au chama kinamkomaza?

Pale Malawi, chama kiliundwa na Rais akiwa madarakani na leo hii hakuna taabu ukilinganisha na waliokuwepo kabla yake.

Slaa akishinda hawezi kushindwa kuongoza dola maana sioni tofauti ya ubora wa hao walioko CCM ukilinganisha na CHADEMA.

Tukubali kwamba vyama na siasa zetu zitaendelea kuwa za kitoto mpaka tutakapokuwa na mifumo imara ya nchi bila kujali ni CCM, CUF au TLP anayeshika ikulu. Hili halitahitaji chama chenye miaka 90, itakuwa ni bahati kama tutampata Rawlings wetu.
 
Tafsiri ya makapi ni pana sana. Ukipembua mchele yale mapumba yanayotupwa ambayo huwa ni kiasi kidogo na kubaki mchele mwingi hii ni tafsiri moja. Pia ukichukua udongo na kupembua dhahabu ambayo ni kidogo na kutupa udongo ambao ni mwingi hapa makapi ni huu udongo.

Hawa watu wanaohama CCM ni dhahabu, hawakutumia rushwa ndio maana hawakupata kuteuliwa CCM. Ukitaka ubunge kupitia CCM ni lazima uwe tajiri (yaani uwe na hela nyingi za takrima). kama huna hutapata haijarishi wewe ni Malechela au Ntagazwa.

Huwezi kujua hili kwa hakika bila kuwapa muda wa kutosha kujionyesha true nature yao ndani ya upinzani. Inawezekana wamekuwa mzigo hata CCM ndiyo maana wakatoswa.

Ndiyo maana wengine tunapendekeza wapewe muda mpaka 2015 waangaliwe.
 
Mkuu, nani kawaambia CCM ndiyo yenye chujio lisilo na matunde tena yakuwekwa kwa makusudi ili wale wembamba kifedha wadondoke na wale wanene kifedha wabaki?
Nani kasema mchujo wa CCM ndio mchujo wenye ubora, na kila ambaye akuchaguliwa na CCM basi ni makapi?..........This is a skewed thinking. Sawa na kufikiri kuwa kwa vile Chadema haijawahi kuwa serikalini basi ikiingia itabidi iweke mpaka wakurugenzi wapya ambao ni wa Chadema.
kuna ubaya gani kuwa unafikiri unaweza ku-workout issues zenu na mkeo, then dakika ya mwisho anakwambia mbona mi sina time na wewe, what do you do? keep crying? go get a life!!

CHADEMA yenyewe haina chujio lake? Inachukua watu tu bila kuwachuja ?
 
Hivi chama kinakomaa namna gani? Yaani kiishi miaka 50 au ni mfumo bora! CCM inayoitwa imekomaa mbona sioni siasa za ukomavu? Tunaingia ktk mtego wa CCM kila wakati kujigamba wamekomaa wakati hawana hata itikadi ya kueleweka kwa miaka 10 iliyopita.

Kinachotakiwa ni personalities na mfumo mzuri wa kuwapata viongozi. Hata CCM hili limewashinda. Ndo maana hata vibaka wanachaguliwa kiurahisi tu! Mtu anakata kadi wiki ya kuchukuwa fomu, anashinda na baadaye ni waziri. Au chama kinamkomaza?

Pale Malawi, chama kiliundwa na Rais akiwa madarakani na leo hii hakuna taabu ukilinganisha na waliokuwepo kabla yake.

Slaa akishinda hawezi kushindwa kuongoza dola maana sioni tofauti ya ubora wa hao walioko CCM ukilinganisha na CHADEMA.

Tukubali kwamba vyama na siasa zetu zitaendelea kuwa za kitoto mpaka tutakapokuwa na mifumo imara ya nchi bila kujali ni CCM, CUF au TLP anayeshika ikulu. Hili halitahitaji chama chenye miaka 90, itakuwa ni bahati kama tutampata Rawlings wetu.

There we go again, stressing personalities over policies. Strongman complex.
 
MAMA POROJO

Ndivyo unavyojidanga ehe!! Eti tuwape muda! Mawe! Unataka uzidi kuiba???? Ngoja kaa la moto wa Mungu aliye hai litakapokudondokea....
 
Last edited by a moderator:
Nimekuwa nikisema more or less the same thing hapa, wanaotoka CCM sasa hivi waangaliwe mpaka at least 2015, kama wameonekana kwamba wamefuata kazi ya chama -na sio kutafuta ubunge kwa sababu wameshindwa kura za maoni CCM- ndipo wapewe nafasi hizi.

Vinginevyo CHADEMA itakuwa inaalika chaos.
Wewe ndugu mbona unaota mchana? Nani alikuambia kwenye siasa za Afrika kura 'kuamini sera' za chama ndio ujiunge!! Unajua hizi siasa za kwenye mtandao zinawapoteza wengi.
 
Tutasema tanzania kuna demokrasia endapo vyama vingi vitavunjwa na vibaki vyama viwili ili kuleta chachu ya maendeleo,
 
There we go again, stressing personalities over policies. Strongman complex.

Ukiingalia Afrika na viongozi wetu wakiwa ktk mikutano yao hakuna anayeonyesha kuwa ana matatizo ya policies. Kila nchi policies safi na zenye matumaini kama National anthems zetu zilivyo.

Lakini ktk serikali zetu hizi nguvu za utendaji kila mtu anafahamu ziko ktk mtu mmoja. Hakuna jinsi kama huyo mtu mwenye nguvu hatapatikana mwenye niya njema.

Hata Europe ilikuwa hivyo ndo maana kila nchi ina shujaa wake aliyeweka misingi imara.
 
Wewe ndugu mbona unaota mchana? Nani alikuambia kwenye siasa za Afrika kura 'kuamini sera' za chama ndio ujiunge!! Unajua hizi siasa za kwenye mtandao zinawapoteza wengi.

Hakuna anayeota mchana, najua kwamba katika siasa za afrika hakuna sera ndiyo maana nikasema hiyo ni pitfall yetu.

Just because siasa za afrika hazina sera, hili halimaanishi kwamba tuwe complacent kuhusu hili na kulikubali kama limeandikwa katika mawe yanayosemekana alipewa Musa na mungu (amri kumi). Point ya kizazi kipya kujadiliana hapa katika forum ni kuona mapungufu ya siasa zetu, na kuya address, hata kama ni kwa kuyataja tu.Kuna watu wanajifunza katika hii forum, kwa hiyo angalau kuyajua tu mapungufu ni muhimu.

Ukija na kusema "wewe unaota mchana, siasa za afrika hazina sera" ni kama unaniambia niache kusema hilo. Sasa tunaambiwa kwamba hatua ya kwanza katika kulitatua tatizo ni kulitambua, tutatatuaje tatizo la siasa za afrika kutokuwa na sera (na kufuata personalities) kama hata kulisema tu tunaambiana "unaota ndoto za mchana".

Ina maana wewe unakubaliana na hizi siasa zisizofuata sera ?
 
Ukiingalia Afrika na viongozi wetu wakiwa ktk mikutano yao hakuna anayeonyesha kuwa ana matatizo ya policies. Kila nchi policies safi na zenye matumaini kama National anthems zetu zilivyo.

Lakini ktk serikali zetu hizi nguvu za utendaji kila mtu anafahamu ziko ktk mtu mmoja. Hakuna jinsi kama huyo mtu mwenye nguvu hatapatikana mwenye niya njema.

Hata Europe ilikuwa hivyo ndo maana kila nchi ina shujaa wake aliyeweka misingi imara.

Policies without implementation is like a car without fuel, pointless.

A car without fuel is as good as -if not worse than- no car, policies without implementation is as good as -if not worse than- no policies.

Kwa sababu bora hata mtu asiye na policies anaweza kusema hakupoteza muda na resources kuweka policies, huyu mwenye policies ambaye hazitumii katumia muda mwingi, watu wamepigizana kelele, marupurupu yamelipwa, katika kuweka policies, halafu hazitumiwi. Come to reflect on it, it is actually worse than pointless, it is counterproductive.
 
Huwezi kujua hili kwa hakika bila kuwapa muda wa kutosha kujionyesha true nature yao ndani ya upinzani. Inawezekana wamekuwa mzigo hata CCM ndiyo maana wakatoswa.

Ndiyo maana wengine tunapendekeza wapewe muda mpaka 2015 waangaliwe.
Utawaangaliaje wakiwa nje acha waingie wapewe kazi zitakazoifanya Chadema ione ubora wao.
 
Ina maana wewe unakubaliana na hizi siasa zisizofuata sera ?

Sikubaliani nazo kabisaaaaaaaaaaa.... lakini ukitaka kuremba kama unavyosema wewe hutafika popote. Huo ustaarabu unaotaka Afrika bado haijaufikia. Inabidi na Chadema nao wacheze kata funua.... ni hali halisi....
 
Asante kwa somo: Naona tatizo liko kwetu wananchi kwasababu tunashindwa kuihusisha CCM na umaskini wetu uliokithiri na ndio maana tutawapigia tena CCM baada ya kurubuniwa na kanga na chakula!

Ila kama mwana_CCM kakubalika na wananchi ila kafyekwa na NEC haina maana ameacha kukubalika kwetu wananchi, nikimaanisha tutampakura zetu bila kujali chama chake kwani tunamchagua mtu sio chama! Kwa hilo nadhani CHADEMA inapompokea, inatarajia kupata pia kura za wananchi waliomuunga mkono. It seems primitive maybe but that seems the reality on the ground!

Ni mawazo yangu tu!
 
Back
Top Bottom