RGforever
JF-Expert Member
- Apr 3, 2011
- 6,878
- 5,424
Mashambulio dhidi ya makanisa mawili nchini Nigeria yameuwa watu kama wanne.
Shambulio kubwa lilifanywa katika mji wa Jos, katikati mwa Nigeria.
Wakuu wanasema watu watatu walikufa na zaidi ya 40 kujeruhiwa wakati mshambuliaji wa kujitolea mhanga, alipojiripuanje ya kanisa.
Kishindo cha mripuko huo kilibomoa sehemu ya jengo.
Shambulio la pili lilifanywa katika mji wa Biu, kaskazini-mashariki mwa nchi.
Polisi walisema wanaume kadha waliokuwa na silaha, walifyatua risasi wakati wa ibada ya asubuhi, na kumuuwa mwanamke mmoja.
Hakuna aliyekiri kuhusika na mashambulio hayo.
Katika miezi ya karibuni, wapiganaji wa Kiislamu wa kundila Boko Haram wamefanya mashambulio kadha kwa bunduki na mabomu.
source BBC SWAHILI