Adrian Stepp
JF-Expert Member
- Jul 1, 2011
- 2,764
- 2,581
Nimepiga plan ya kusimplify mambo hapa mjini nikaamua kwamba! kila weekend especially Jumapili ni mwendo wa kande tu..kwanza na minimize cost.
Nitanunua..Maharage nusu
Njugu Nusu
Karanga Nusu
Mahindi Nusu na Nazi mbili na Mchicha fungu 5... Msosi simple but very smart..Hutaki Acha!
========
Makande ni chakula chenye mchanganyiko wa nafaka mbalimbali kama mahindi, maharage,njugu, mtama au ngano isiyokobolewa.
Mahitaji
Pia unaweza pika ya mtindo huu
Katika mapishi haya tunatumia nazi na karanga. Ni chakula bora chenye ladha bora na kukupa hamu ya kujiramba.
Mahitaji
Michango ya wadau
Nitanunua..Maharage nusu
Njugu Nusu
Karanga Nusu
Mahindi Nusu na Nazi mbili na Mchicha fungu 5... Msosi simple but very smart..Hutaki Acha!
========
Makande ni chakula chenye mchanganyiko wa nafaka mbalimbali kama mahindi, maharage,njugu, mtama au ngano isiyokobolewa.
Mahitaji
- Mahindi yaliyokobolewa(makande)kg1
- Nazi 1 kubwa
- Swaumu iliyosagwa & tangawizi vijiko 4
- Maharage nusu kg
- Nyanya 3
- Vitunguu maji 2
- Hoho 3
- Karoti 3
- Ajinamoto nusu kijiko cha chai
- Chumvi kiasi
- Celery kuchu 1
- Mafuta ya kulanprobo kikombe
- Mboga za majani kuchu 1
- Osha mahindi na maharage kisha injika jikoni baada ya nusu saa weka mahindi kisha funika yaendelee kuiva.
- Kuna nazi yako weka tui la kwanza zito, kisha saga nyanya ziweke tayari Kwa kupikwa.
- Kata vitunguu, karoti na hoho mtindo wa quips.
- Baada ya hapo weka anagalia kama makande yameiva
- Kisha weka sufuria yako ya kuungia jikoni, weka kitunguu maji baada ya dakika 1 au 2 tia mchanganyiko wako wa swaum na tangawizi endelea kukoroga.
- Tia nyanya uliyosaga kisha funika kidogo iive baada ya hapo weka makande.
- Endelea kukoroga kisha punguzia moto chakula chako kiive taratibu ukishaona yameiva vizuri tia tui la nazi na koroga ili lisikatike. Epua andaa mezani
Pia unaweza pika ya mtindo huu
Katika mapishi haya tunatumia nazi na karanga. Ni chakula bora chenye ladha bora na kukupa hamu ya kujiramba.
Mahitaji
- Mahindi yaliyokobolewa – kilo 1½
- Maharage ½ kilo
- Vitunguu maji 3
- Nyanya 2
- Karanga ¼ kilo
- Njugu mawe ½ kilo
- Pilipili hoho 1
- Chumvi kijiko 1 cha chai
- Mafuta ¼ lita
- Nazi kubwa 2.
- Chambua maharage, mahindi, karanga na njugu mawe kisha osha vizuri.
- Changanya maharage, mahindi na njungumawe pamoja.
- Bandika sufuria ya maji jikoni. Weka mchanganyiko wa maharage, weka chumvi kisha acha mchanganyiko uchemke vizuri. Kwa kawaida maharage yanachukua muda mrefu kuiva vizuri. Hivyo unaweza kusubiria takribani dakika 25-30 ili kuhakikisha yameiva. Kama maji yakikauka kabla ya maharage kuiva, ongeza maji kiasi ili yaive vizuri.
- Andaa vitunguu, pilipili hoho na nyanya kwa kuosha kisha kuvikata vipande vidogo vidogo. Weka vizuri na kusubiria kuvichanganya na makande.
- Andaa tui la nazi kwa kuchuja tui zito ili liwe tayari kuchanganya na chakula.
- Kama maharage na njugumawe yakikaribia kuiva (takribani dakika 30) weka karanga kwenye mchanganyiko. Koroga ili vichanganyike vizuri. Acha iendelee kuchemka na subiria hadi mchanganyiko uive vizuri. Mchanganyiko ukiiva vizuri toa jikoni na hifadhi pembeni.
- Bandika sufuria, weka mafuta ya kula kisha acha yachemke.
- Mafuta yakipata moto vizuri weka vitunguu kisha koroga koroga hadi vibadilike rangi na kuanza kuwa na rangi ya udongo.
- Weka pilipili hoho, karoti. Koroga kiasi kwa muda wa dakika 2 hadi 3.
- Weka nyanya, koroga kiasi na kisha funika na mfuniko. Acha nyanya ziive vizuri kwa mvuke ili ziwe laini. Baada ya dakika 6-8 unaweza kuponda ua kusaga nyanya ili kupata mchuzi wenye rojo. Koroga ili kupata mchanganyiko mzuri.
- Nyanya zikiiva vizuri weka mchanganyiko wa maharage kwenye sufuria. Koroga vizuri hadi mchangyiko uwe sawia. Onja ili kujua kama kiwango cha chumvi kinatosha. Unaweza kuongeza kama haitoshi.
- Weka tui la nazi huku ukikoroga ili kuzuia tui kukatika. Koroga hadi ianze kuchemka.
- Funika sufuria na subiria kwa muda wa dakika 10, kisha ipua chakula jikoni ili upate kujiramba.
Michango ya wadau
----Mimi huwa nayapenda ya Nazi m
na Hiriki...
Mahitaji:
*Nazi (kubwa) yakikolea Nazi yananoga sanaaa
*Kitunguu maji
*mafuta ya kupikia kiasi
*Karoti (ukipenda)
*Hiriki
*chumvi kiasi
Baada ya kuchemsha makande yako na kuiva vizuri, yaepue yaweke pembeni
Bandika sufuria jikoni, tia mafuta ya kupikia kiasi, yakipata moto tia vitunguu ulivyovikatakata...
Kaanga vitunguu, vikianza kuwa brown tia karoti ulizokata katika shape uipendayo
Vikishachanganyika mimina makande ulochemsha tia na hiriki uchanganye pamoja
Kisha weka tui la pili la Nazi, na chumvi, koroga tui lichanganyike na makande, acha vichemke pamoja...
Kisha weka tui zito, koroga vizuri, vikishachemka na kuchanganyika vizuri epua...Makande yako tayari kwa kuliwa...
Mimi huyaweka na sukari pia ...
Jee inajuwa jinsi ya kupika makande?
Makande ni chakula cha mchanganyiko wa mahindi na maharage pamoja na vikorombwezo vingine kama vile vitunguu,karoti,hoho muda mwingine hata nyanya unaweza kuweka.
Katika mapishi ya makande unaweza kuunga kwa kutumia mafuta au ukaweka hata nazi.
Hivi ndivyo jinsi ya kupika makande ya nazi,karibuni sana
Mimi huwa nayapenda ya Nazi
na Hiriki...
Mahitaji:
*Nazi (kubwa) yakikolea Nazi yananoga sanaaa
*Kitunguu maji
*mafuta ya kupikia kiasi
*Karoti (ukipenda)
*Hiriki
View attachment 477880*chumvi kiasi
Baada ya kuchemsha makande yako na kuiva vizuri, yaepue yaweke pembeni
Bandika sufuria jikoni, tia mafuta ya kupikia kiasi, yakipata moto tia vitunguu ulivyovikatakata... Kaanga vitunguu, vikianza kuwa brown tia karoti ulizokata katika shape uipendayo
Vikishachanganyika mimina makande ulochemsha tia na hiriki uchanganye pamoja
Kisha weka tui la pili la Nazi, na chumvi, koroga tui lichanganyike na makande, acha vichemke pamoja... Kisha weka tui zito, koroga vizuri, vikishachemka na kuchanganyika vizuri epua...Makande yako tayari kwa kuliwa... Mimi huyaweka na sukari pia ... Hebu jaribu kumtagi na mwenzio aje naye ajuwe ni namna gani ya kupika makande.