VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Makanali kadhaa wa Kiongozi wa Libya aliye kwenye waya mkali hivi sasa,Kanali Muhammar Gaddafi wametua bila ruhusa na ndege zao za kivita katika kisiwa cha Bahari ya Medditerrania,Malta.Walipokamatwa na kuhojiwa,Makanali hao wamedai kuwa wametorokea huko baada ya kukataa kutii amri ya kushambulia kwa mabomu umati wa waandamanaji katika mji wa Benghazi,yalipoanzia maandamano ya kumng'oa madarakani Gaddafi.Baada ya kukataa amri hiyo ya kijeshi,makanali hao walisafiri takribani umbali wa saa moja na kutua kwa dharura Malta.Bado wanashikiliwa na maofisa wa Malta kwa uchunguzi na taarifa zaidi.Je,hawa ni mashujaa au wasaliti?