Makamu wa rais wa Iran kuja kesho Tz: kuna nn nyuma ya pazia?

dosama

JF-Expert Member
Dec 25, 2010
912
957
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Dk. Mohamad Reza Rahimi, atawasili jijini Dar es Salaam kesho tayari kwa ziara ya siku tatu ya kikazi hapa nchini, ambapo atalakiwa na mwenyeji wake, Makamu wa Rais wa Tanzania, Dk. Gharib Bilal.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Balozi wa Irani nchini, Mohsen Movahedi, alisema wakati wa ziara yake, Dk. Rahimi ataweka jiwe la msingi katika ujenzi wa hospitali mbili za kisasa huko Kigamboni na Mkoa wa Magharibi Unguja.

“Jumatano ataweka jiwe la msingi katika ujenzi wa hospitali ya Kigamboni itakayogharimu sh. bilioni 1.5 na Alhamisi atakuwa Zanzibar kwa jukumu kama hilo katika ujenzi wa hospitali itakayogharimu sh. bilioni mbili,” alifafanua Balozi Movahedi na kuongeza kuwa, keshokutwa pia atazindua zahanati mpya ya Msasani ambayo imejengwa kwa ufadhili wa Serikali ya Iran.

Akitoa ratiba ya ziara hiyo, Balozi Movahedi alisema mapema Jumatano, Dk. Rahimi ataonana na kufanya mazungumzo na Rais Jakaya Kikwete Ikulu Dar es Salaam, kabla kuzumgumza na mwenyeji wake, Dk. Bilal na kisha kukutana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

“Lengo kubwa la ziara ya Dk. Rahimi hapa Tanzania ni kukuza mahusiano ya kidiplomasia na kihistoria kati ya Tanzaania na Iran. Ni katika msingi huo Iran imetoa msaada wa ujenzi wa hospitali hizo mbili, pia itaweka vifaa na kuanza kuendesha chuo cha mafunzo stadi cha Zanzibar,” alisema balozi huyo wa Iran nchini.

Kwa upande wa Zanzibar, Dk. Rahimi atakutana na kufanya mazungumzo ya kina na Rais wa Zanzibar, Dk. Mohamed Shein, Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharrif Hamadi na Makamu wa Pili wa Rais, Balozi Iddi Seif.
.

Interejensia ya Jf naomba msaada kuna nini nyuma ya pazia?
 
Hoja yako haina maana yoyote, mbona nchi hii inatembelewa na viongozi toka nchi mbalimbali duniani, kwani uone kuna jambo tofauti kwa huyu kuja Tz!
 
Hoja yako haina maana yoyote, mbona nchi hii inatembelewa na viongozi toka nchi mbalimbali duniani, kwani uone kuna jambo tofauti kwa huyu kuja Tz!

What you see is not always what you get, ndio maana ukawa na akili, ili uweze kuchambua mambo. Sio kila mgeni ana lengo la kusalimia.
 
Nimeshindwa kuelewa hasa ulikua na malengo gani ktk thread yako..
Labda kwa vile hujawa muwazi wa kile unachokiwaza. Lakini nikuulize TATIZO nini mpaka useme kuna lililojificha nyuma pazia?? mbona viongozi wengi wamekuja ktk hii nchi: Mkumbuke Bush alipofunga safari kutoka Marekani kuja kutuletea neti...hili ulilihoji??

Nadhani UDINI ndio unakutesa na inawezekana moyoni unawatusi wazazibar waliochoma kanisa jana (Hata mimi siwaungi mkono) lakini wewe una chuki ya udini kuliko wao
 
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Dk. Mohamad Reza Rahimi, atawasili jijini Dar es Salaam kesho tayari kwa ziara ya siku tatu ya kikazi hapa nchini, ambapo atalakiwa na mwenyeji wake, Makamu wa Rais wa Tanzania, Dk. Gharib Bilal.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Balozi wa Irani nchini, Mohsen Movahedi, alisema wakati wa ziara yake, Dk. Rahimi ataweka jiwe la msingi katika ujenzi wa hospitali mbili za kisasa huko Kigamboni na Mkoa wa Magharibi Unguja.

“Jumatano ataweka jiwe la msingi katika ujenzi wa hospitali ya Kigamboni itakayogharimu sh. bilioni 1.5 na Alhamisi atakuwa Zanzibar kwa jukumu kama hilo katika ujenzi wa hospitali itakayogharimu sh. bilioni mbili,” alifafanua Balozi Movahedi na kuongeza kuwa, keshokutwa pia atazindua zahanati mpya ya Msasani ambayo imejengwa kwa ufadhili wa Serikali ya Iran.

Akitoa ratiba ya ziara hiyo, Balozi Movahedi alisema mapema Jumatano, Dk. Rahimi ataonana na kufanya mazungumzo na Rais Jakaya Kikwete Ikulu Dar es Salaam, kabla kuzumgumza na mwenyeji wake, Dk. Bilal na kisha kukutana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

“Lengo kubwa la ziara ya Dk. Rahimi hapa Tanzania ni kukuza mahusiano ya kidiplomasia na kihistoria kati ya Tanzaania na Iran. Ni katika msingi huo Iran imetoa msaada wa ujenzi wa hospitali hizo mbili, pia itaweka vifaa na kuanza kuendesha chuo cha mafunzo stadi cha Zanzibar,” alisema balozi huyo wa Iran nchini.

Kwa upande wa Zanzibar, Dk. Rahimi atakutana na kufanya mazungumzo ya kina na Rais wa Zanzibar, Dk. Mohamed Shein, Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharrif Hamadi na Makamu wa Pili wa Rais, Balozi Iddi Seif.
.

Interejensia ya Jf naomba msaada kuna nini nyuma ya pazia?

lazima aende kwenye chuo chao (hata kama tutafichwa)
 
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Dk. Mohamad Reza Rahimi, atawasili jijini Dar es Salaam kesho tayari kwa ziara ya siku tatu ya kikazi hapa nchini, ambapo atalakiwa na mwenyeji wake, Makamu wa Rais wa Tanzania, Dk. Gharib Bilal. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Balozi wa Irani nchini, Mohsen Movahedi, alisema wakati wa ziara yake, Dk. Rahimi ataweka jiwe la msingi katika ujenzi wa hospitali mbili za kisasa huko Kigamboni na Mkoa wa Magharibi Unguja. "Jumatano ataweka jiwe la msingi katika ujenzi wa hospitali ya Kigamboni itakayogharimu sh. bilioni 1.5 na Alhamisi atakuwa Zanzibar kwa jukumu kama hilo katika ujenzi wa hospitali itakayogharimu sh. bilioni mbili," alifafanua Balozi Movahedi na kuongeza kuwa, keshokutwa pia atazindua zahanati mpya ya Msasani ambayo imejengwa kwa ufadhili wa Serikali ya Iran. Akitoa ratiba ya ziara hiyo, Balozi Movahedi alisema mapema Jumatano, Dk. Rahimi ataonana na kufanya mazungumzo na Rais Jakaya Kikwete Ikulu Dar es Salaam, kabla kuzumgumza na mwenyeji wake, Dk. Bilal na kisha kukutana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. "Lengo kubwa la ziara ya Dk. Rahimi hapa Tanzania ni kukuza mahusiano ya kidiplomasia na kihistoria kati ya Tanzaania na Iran. Ni katika msingi huo Iran imetoa msaada wa ujenzi wa hospitali hizo mbili, pia itaweka vifaa na kuanza kuendesha chuo cha mafunzo stadi cha Zanzibar," alisema balozi huyo wa Iran nchini. Kwa upande wa Zanzibar, Dk. Rahimi atakutana na kufanya mazungumzo ya kina na Rais wa Zanzibar, Dk. Mohamed Shein, Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharrif Hamadi na Makamu wa Pili wa Rais, Balozi Iddi Seif. . Interejensia ya Jf naomba msaada kuna nini nyuma ya pazia?
Huu ni utoto na upuuzi mkubwa unaoonyesha kwamba hata kama ulipita shule bac hujaelimika hata kidogo au hujui kusoma. Habari inajieleza wazi kuwa huyo Makamu atafanya shughuli ipi na ipi, sasa unataka nini tena. Labda tusaidie tujue ikiwa hizo shughuli zilizoainishwa si za kweli(hazipo hapa nchini). Watanzania lets focus on development programs rather than non multiplier things as what you posted! Very low posting
 
Imethibitika kumbe walisainishana kutumia bendela ya Tanzania katika meli za Irani zinazobeba mafuta
 
Nimeshindwa kuelewa hasa ulikua na malengo gani ktk thread yako..
Labda kwa vile hujawa muwazi wa kile unachokiwaza. Lakini nikuulize TATIZO nini mpaka useme kuna lililojificha nyuma pazia?? mbona viongozi wengi wamekuja ktk hii nchi: Mkumbuke Bush alipofunga safari kutoka Marekani kuja kutuletea neti...hili ulilihoji??

Nadhani UDINI ndio unakutesa na inawezekana moyoni unawatusi wazazibar waliochoma kanisa jana (Hata mimi siwaungi mkono) lakini wewe una chuki ya udini kuliko wao
Bush aluvyokuja alileta mtafaruku mkubwa sana kule Kigamboni, hadi sasa watu wanatakiwa kuhamishwa. Hao wa Iran nao huwezi jua maana wanafululiza sana na hata meli zao za mafuta wanabadilisha umiliki kuzifanya za Tanzania
 
Anaenda kuwapa big-hi UAMUSHO Kazi wanayofanya huko na huenda wakapewa vitendea kazi.
 
Kiufupi tu anakaribishwa sana kwa mikono miwili na ajisikie yupo nyumbani.Ila pia umesahau au hujui kama Iran wametusamehe mamilioni au mabilioni ya pesa muda wa mwezi tu uliopita kwa hiyo natoa shukurani nyingi kwa Iran.Na kama wamekuja kuwekeza ktk afya pia natoa shukurani nyingi kwani hata Zimbabwe wanafaidika walala hoi kwa matibabu ya wa Iran.Kwakweli tunahitaji hospitali kwasababu wenye uwezo wanakimbilia India na walala hoi wanabanana na kufa kwa hio labda watatuletea barka na mwenyezi mungu awazidishie imani.

Ukiona mtu anachangia kwa jazba ya ubaguzi wa dini basi ujue kaishiwa na maneno na hawezi hata kujituma kiakili.Na mleta mada sijajua hasa ni nini unachohitaji kujua na sioni kama kuna siri yoyote.Wanayo haki ya kuekeza alimradi hawaendi kinyume na sheria za kwetu.Kuhusu Zanzibar labda hamfamu kama Iran inayo historia ya karne nyingi zilizopita kama waliwahi kufika Zanzibar.Wengi wenu humu hamzijui historia za uhakika mnabaki kuropoka tu.Wa Iran wamewahikuacha historia ya msikiti ambao ni mmoja ktk misikiti ya zamani ulijengwa tokea mwaka 1107 AD.Kwahivo wanayohaki ya kuwahisani kwakuwa Iran ni nchi mojawapo tajiri na uchumi wake ni mzuri pamoja na vikwazo alivowekewa.

Watanzania mkiendelea na hizo alnacha zenu za kijinga kuhusu ugaidi kwakweli tutadumaa kiakili.Maana kunaelekea watu kulazimishwa nini tupende na nini tusipende.Kila mtu abaki na dini yake na aheshimu dini ya mtu mwingine.Utu ndio kitu muhimu sana na kama tunaondoa utu wetu na kujivisha shada la ubaguzi basi hatufiki popote tutaishia midomo tu.Sijawahi kusikia nchi inaendelea kwa ubaguzi na ndio maana unaona nchi hii haijapiga hatua yoyote kwasababu ya ubaguzi wa ndani kwa ndani na mpaka leo hii tunashuhudia waziwazi bila ya kificho.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom