Makamu wa Rais Shein is the Best in Leadership: (Picha)

Dr. Shein alikuwa Makamu wa Rais wa Mkapa ambaye wakati wa utawala wake ufisadi ulijengwa na kuimarishwa kikamilifu. Sasa ni Makamu wa Rais wa Kikwete anayeendeleza ufisadi huo uliojengwa na Mkapa akisaidiwa na Shein. Hadi leo sijamsikia akikemea ufisadi kwa nguvu zake zote. Shein siyo mwanasiasa bali ni mtu aliyechukuliwa kutokana na uzezeta (upole?) wake ili aendelee kutekeleza majukumu ya Bosi wake bila kuhoji kinachoendelea. Yeye ni aina ya "NDIYO BWANA"! Hafai kuwa Rais ajaye. Labda awe Rais wa Wapemba.
 
Tatizo Shein na hata dr Omar, hawawezi kuchaguliwa kwa sababu wabongo tunapenda wababe na mapedejee na mabishoo.
When we start rewarding people on merit, ndipo tutakapoanza kupata maendeleo ya kweli.
I think we need a leader with:
Shein's Simplicity + Kikwete's Charisma + Mkapa's Brains(and Ubabe) + a dash of Magufuli mixed with Pinda - Edward Lowassa.
 
Kwa kazi zake as stipulated in the URT constitution.. Mtarajiwa ameziainisha ni lazima afunikwe na Waziri Mkuu... Lkn pia tujiulize kwani huyu jamaa alikua chaguo la Mkulu Kikwete?

Wengi wanasema yuko simple, hana makuu, si fisadi etc... Nafikiri,its a high time now for we Tanzanians to think beyond that. Hatutaki na tusiwa-assess viongozi wetu kwa haiba na kwamba ni simple, au sio fisadi.... we want leaders ambao ni result-oriented, leaders ambao tutawa-assess kwa walichotufanyia watanzania.... Kwa roles zake ni nini amefanya cha maana na upole, u-simple wake, kutokua fisadi hadi tumsifie? Naombeni mnitajie jamani... Labda sijui...au nimesahau.....au sioni tu kama ni mafanikio....

The man is cool, halina mjadala hilo...... Lakini we want results guys. Like anyone, in Kikwete's entourage, they're fulfilling their election manifesto..... Lets assess our leaders kwa kuangalia hiyo na roles zao km zilivyoainishwa ktk katiba badala ya kuangalia haiba zao, na kwamba ni watu wa watu kisa wamefika Missenyi shambani.....while anakula per diems zake, na si ajabu siku hiyo kaondoka Missenyi lkn kuna watu wengi walilala njaa, na hawana basic needs km mwenye hilo shamba lilivyostawi anae-represent wachache ktk vijiji vungi vya Tanzania..... Wengi tumekulia vijijini tunajua hali za huko!

I stand to be corrected objectively!
 
Raisi ni Salim au Lipumba ,ikiwa mnataka Raisi alietulia hana mhali na mtu ,straight forward ,fanya unafanya huwezi ondoka.
hao ni watu ambao kwa sasa inaweza kujivunia kuwa wanaweza kabisa kuiondoa Tz katika hali iliyo.
Salim ni mtu ambae ubabe wa kukuwajibisha anao ,maana ni mtu anaonekana ni act alone hana mshirika zaidi ya kuhudhuria ,kwa hali iliyopo hawezi kupinga kitu kwani anaielewa hali ya walioshika madaraka ni wabishi na ving'ang'anizi kwa maslahi binafsi hivyo naweza kusema hana meno.

Lipumba ni mtu wa mahesabu nina uhakika kabisa anaweza kukatakata mishaara ya kuanzia yeye mwenyewe ,mawaziri ,wabunge na sehemu zote za serikali ambazo zitakuwa chini ya uongozi wake ,kama unaweza endelea na kazi kama huwezi kaanzishe biashala zako nje ya serikali na zaidi atatumia uchumi wa Nchi kuwaendeleza wananchi huko huko waliko bila ya kuhitaji kufuatilia miji yenye umeme. Lipumba anaamini uimarishaji wa infrastructure kwa kuunganisha mikoa na nchi jirani ni muhimu ,kuimarisha bandari zote za hapa nchini kuwa za kisasa na zenye ushindani wa kimataifa akitegemea soko la nchi za Ruanda Burundi Congo Zambia ,Malawi Uganda kuwa zitaweza kabisa kutumia bandari za Tanzania na hivyo kuliingizia Taifa fedha ya uhakika. Kwa ufupi ni mchumi na mawazo yake hayaendani mbali na namna ya kutaka hali ya mtanzania iwe ya juu kama anavyoona huko nchi za walioendelea ambazo ujuzi wake unatumika na kuzaa matunda.Hivyo nguvu yake ni kuhakikisha maelezo toka ikulu yanafuatwa na kufanyiwa kazi sio kukaa kila mwisho wa mwezi na kusoma matangazo ya kifo.
 
Lipumba ni Kiongozi mzuri lakini hafai kutuongoza akiwa na CUF kwa sababu ya udini katika chama hicho
 
I really really hope this is a joke and one in very very bad taste !! Huyu naweza kumfananisha tu na katope mtoto wa ajabu. Salama yake huko huko kukavu - mshushie tu mvua, anamomonyeka. Anikumbusha ice cream - salama yake baridi tena ndani ya jokofu - nje kwenye joto inayeyuka. Mwacheni Shein hapo hapo alipo kivulini na mikasi yake - huko juu hakuwezi !!
 
Kwa hakika uongozi wa Makamu wa Rais Sheni ni mzuri
Labda ni kwa sababu he is a mathematician. I have noticed kwamba hawa watu waliojifunza hesabu wanafikiria kwa mantiki sana. Labda kwa sababu axiom na Theorems wanazojifunza.
 
Kiongozi lazima awe mfano bora kwa wananchi wake. Shein si fisadi kama Mkapa na hana ubishoo kama Kikwete. Tunahitaji kiongozi muadilifu kama Shein... halafu hata viongozi atakaofanya nao kazi (akiwa Rais) ni lazima wataiga uadilifu wake, vinginevyo watakuwa hawapikiki chungu kimoja.

Kwa kipindi chote cha umakamu wake, ametekeleza mashauri ya viongozi wasio mfano bora... na hakuiga chochote kutoka kwao! To me he is a focused gentleman!

Akiwa Rais, Shein atavaa husika ya watanzania! Mafisadi na mabishoo hawataona ndani. Huyu ni kiongozi wa kweli.

Kila mtu atatimiza wajibu wake.. na ndio kazi ya Rais kuhakikisha hayo!

Rais akiwa Fisadi kama Mkapa, ndipo unapata watu kama akina Lowassa, Balali, Mramba, Yona n.k

Rais akiwa bishoo kama kikwete, hakuna maendeleo na ndipo unapata watu kama Salva, Nchimbi n.k hakuna kazi ni ubishoo mtupu!!!!!
 
Asante MMKJ. The man is simple, humble and down to earth. Hana majigambo, hajisikii, yaani yopo yupo tuu. Mungu ambariki sana!.
Nakumbuka mwaka 2002 alikuja Rome kuhudhuria Mkutano wa World Food Day, Ten Years After. Baada ya Mkutano, on his way home, Alitakiwa apande Alitalia mpaka Bern, aunganishe na Swiss Air back home. Kufika airport Taarifa zikaja Alitalia imefilisika hivyo hakuna ndege. swissair wakamwambia asubiri hapo atatumiwa ndege nyingine any moment. Alisubiri tangu saa 2 asubuhi mpaka saa 10 Jioni. Balozi wakati huo Mahalu akashauri arudi hotelini lakini Muungwana akasema atasubiri tuu hapo hapo kama watu wengine.
Alipata fursa ya kuongea na waTanzania tuliokuwa hapo, kusema kweli ni mtu wa ajabu, hakuonyesha kukerwa kokote, yaani ana uvumilivu wa ajabu. Wangekuwa viongozi wengine mbona pangekuwa hapatoshi.
Binafsi japo tuliteseka sana haswa akina sisi wa senti zero on your way home, lakini
Tulifarijika sana kuteseka na Mkuu wetu miongoni mwetu.
He is really A Man of The People!. Tena bora JK asimalizie his second term bali ampishe huyu jamaa. Ni mtu wa Swala 5 kiukweli sio za kuzugia ama kuonyeshea watu waone. Nchi itatulia neema na ustawi vitaonekana.

You might be right man, I appreciate the man
 
Kwa hakika uongozi wa Makamu wa Rais Sheni ni mzuri
Labda ni kwa sababu he is a mathematician. I have noticed kwamba hawa watu waliojifunza hesabu wanafikiria kwa mantiki sana. Labda kwa sababu axiom na Theorems wanazojifunza.


Shein ni MD na ana PhD ya biochemistry kama sikosei.sasa huo u mathematician umetoka wapi?
 
Back
Top Bottom