Makamu wa Rais ana kazi gani?

Kwa kweli hata mimi sielewi umuhimu wa kuwa na Makamu wa Rais. Katiba ya sasa inasema kwamba Makamu wa Rais ni Msaidizi Mkuu wa Rais kuhusu mambo yote ya Jamhuri ya Muungano kwa jumla. Hususan (a) atamsaidia Rais katika kufuatilia utekelezaji wa siku hata siku za Mambo ya Muungano; (b) atafanya kazi zote atakazoagizwa na Rais; na (c) atafanya kazi zote za Rais kama Rais hayuko kazini au yuko nje ya nchi.

Kwa Makamu huyu wa Rais ni mambo yapi ya muungano ambayo amemsaidia Rais kufuatilia utekelezaji? Ina maana hizi kazi anazofanya za kuzindua na kuwa mgeni rasmi anakuwa ametumwa na Rais? Halafu kuna hili la kufanya kazi zote za Rais kama Rais hayuko kazini au yuko nje ya nchi. Sasa juzi tuu Rais alikuwa nje ya nchi na kulikuwa na mgomo wa madaktari. Je, Makamu wa Rais alifanya nini la maana kujaribu kushughulikia? Mimi nilmwona tuu alipoenda kumpokea Rais uwanja wa ndege wakati akirejea nchini. Inaonyesha labda hata madaktari walimdharau pale walipoamua kukutana na Waziri Mkuu.

Inavyoonekana ni kwamba Makamu wa Rais huwa anatekeleza madaraka yake chini ya uongozi na usimamizi wa Rais na anaongoza na kuwajibika kwa Rais kuhusu mambo au shughuli zozote anazokabidhiwa na Rais. Kwa hiyo hapa itategemeana na Rais amempa kazi gani. Kama hajampa kazi, hana cha kufanya. Na kwa vile labda hakuna kazi za kumpa, ndiyo maana labda huwa anaishia kuzindua tuu vitu, kukata utepe, kuweka jiwe la msingi na kuwa mgeni rasmi kwenye mambo ambayo yangefanywa hata na mkuu wa wilaya?
 
Makamo wa rais yupo yupo tuu standby just in case anything happens kwa rais!. Ila makamo wa rais anapokuwa mchovu mchovu, hilo nalo neno!

Mi nadhani tatizo ni kuwa he is not a bird of the same feather as the others...

Amepewa tu nafasi ile,katika jitihada za kuweka mambo sawa...

Siwezi kuelewa ukisema yupoyupo maana ana majukumu na ana mawaziri wanaoreport kwake..
 
Makamu wa Rais anatembea na mkasi wa kukatia utepe
Muzee ya Mikasi!!!!

scicors.jpg
 
Moja ya mambo ya kupendekeza kuondolewa katika katiba mpya ni nafasi ya makamu wa rais. Kufungua warsha au kukata utepe katika uzinduzi wa majengo hakuliongezei taifa chochote zaidi ya hasara kutokana na matumizi mabaya ya rasilimali - vyote 'pesa, mali na watu. Hebu fikiria, makamu wa rais akienda kwenye huo uzinduzi anaoufanya anaongozana na watu wengi ambao wangeweza kufanya kazi nyingine zenye tija zaidi.
 
MwanaFalsafa1

Nilitegemea uende extra miles kwa kusoma katiba ya JMT, ila hukufanya hivyo na unataka sie tukusomee, ww kweli ni GT ? au hujui kusoma mkuu ?

 
Last edited by a moderator:
Makamu wa rais ana kazi nne kuu:

1) Kufungua miradi/kuweka jiwe la msingi/kukata utepe

2) Kupokea wageni Ikulu wakati Kikwete akiwa safarini marekani na Ulaya

3) Kuhudhuria Sherehe za ki-imani ambazo waumini wake hupenda wageni rasmi wa serikali
01.jpg


4) Kuhudhuria kwenye misiba.......lakini mkulu kamnyang'anya hiyo task siku hizi, Mkulu anaenda mwenyewe......So, the poor guy go back to number one.....here we go...
 
muzee ya mikasi!!!!

Hahahahahahahaha jf hadi raha hoja kwa mifano hii mikasi mbona ya fundi chelehani,ungeifunga hata riboni kwa sababu yeye ni boss kubwa kukatia utepe

scicors.jpg
ndio maana mgomo wa madaktari umetokea ahaaaa makamu wa raisi yuko busy kuweka mawe ya msingi na majengo yenyewe hayaishi
 
Hana kazi na ni uharibifu wa rasilimali za taifa.Aende akafundishe fizikia kuliko kuzururazurura na kufungua hata majalo ya kutupia taka.Hii ni aibu ya nchi hii usanii kila mahali.Shit
 
Hiki cheo cha Makamu wa rais inabidi kiondolewe kwenye katiba mpya maana gharama yake ni kubwa kuliko manufaa yake. Jamaa amekuwa mtu wa mikasi kwa kwenda mbele.
 
Alichonimaliza huyu bwana ni ile siku nimekutananaye akiwa Serengeti na wake zake na alileta usumbufu mkubwa sana kwa watalii waliokua wamelipa hela zao kuja kuangalia wanyama yeye na misafara yake ya magari zaidi ya 50 na tena aliwasumbua hata na wanyama!

_DSC1066.JPG
 
Haya mambo ndiyo yanatufanya wazungu watuona wajinga. Nchi ya tatu duniani kwa omba omba eti tuna RAIS, VP, PM ufujaji tu wa pesa. Just imagine eti ka-nchi kama ZNZ ambako hakalingani hata na mkoa wa Mwanza eti kana RAIS, 1st VP, 2nd VP wizi mtupu.

Kama tumeamua kufuata system ya US basi tuwe na Rais na VP tu, cheo cha PM tukifute. Haya mambo lazima tuyaainishe kwenye katiba mpya mambo ya kujirundikia ma-vyeo na mawizara mengi ndiyo yanatafuna pesa za nchi hii. Ndiyo maana VP wetu anaitwa mzee wa mikasi kwasababu kazi yake ni kufungua/kufunga makongamano, warsha, semina, mikutano na kupanda miti (sijui amekuwa bwana miti!!)

Ndiyo maana hata suala la Jairo lilipotokea bungeni ilibidi Pinda amsubiri JK (Rais) na wala hakuweza kwenda kwa VP ingawa katiba inasema wazi kama rais hayupo basi VP ndiyo ana kaimu nafasi ya urais.
 
mwee hawa wote wakwake?
ama kweli ng'ombe hazeeki maini
hii nji ya kipunguani sana
wanashindwa kutatua
matatizo makubwa ya wananji
wana kazi ya kumangamanga
huko maporini
hivi kwanini wasingeliwa na simba
aghrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr


Alichonimaliza huyu bwana ni ile siku nimekutananaye akiwa Serengeti na wake zake na alileta usumbufu mkubwa sana kwa watalii waliokua wamelipa hela zao kuja kuangalia wanyama yeye na misafara yake ya magari zaidi ya 50 na tena aliwasumbua hata na wanyama!
 
Jibu lake ni rahisi tu. Hizi ndizo kazi zake kwa mujibu wa kifungu cha 47 katiba ya JMT. Kama kuna kazi nyingine atakuwa anafanya zaidi ya hizi hapa basi hasitahili kulipwa kwani hakuajiriwa kwa zaidi ya hizi hapa.
47.-(1) Kutakuwa na Makamu wa Rais ambaye atakuwa ndiye Msaidizi Mkuu wa Rais kuhusu mambo yote ya Jamhuri ya Muungano kwa jumla, na hususan-
(a) atamsaidia Rais katika kufuatilia utekelezaji wa siku hata siku za Mambo ya Muungano;
(b) atafanya kazi zote atakazoagizwa na Rais;
(c) atafanya kazi zote za Rais kama Rais hayuko kazini au yuko nje ya nchi.

(2) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 37(5), Makamu wa Rais atapatikana kwa kuchaguliwa katika uchaguzi ule ule kwa pamoja na Rais, baada ya kupendekezwa na chama chake wakati ule ule anapopendekezwa mgombea kiti cha Rais na watapigiwa kura kwa pamoja. Mgombea kiti cha Rais akichaguliwa basi na Mahakmu wa Rais atakuwa amechaguliwa.

(3) Mtu atateuliwa kugombea kiti cha Makamu wa Rais kwa kufuata kanuni kwamba endapo Rais wa Jamhuri ya Muungano atatoka sehemu moja ya Muungano, basi Makamu wa Rais atakuwa ni mtu anayetoka sehemu ya pili ya Muungano.


Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania


(4) Mtu hatateuliwa kugombea au kushika kiti cha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kama-
(a) ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa sheria ya Uraia;
(b) ametimiza umri wa miaka arobaini;
(c) ni mwanachama na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;
(d) anazo sifa za kumwezesha kuwa Mbunge au Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi;
(e) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya uchaguzi hajawahi kutiwa hatiani katika Mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.

(5) Chama chochote hakitazuiwa kumpendekeza mtu yeyote kuwa mgombea kiti cha Makamu wa Rais kwa sababu tu kwamba mtu huyo kwa wakati huo ameshika kiti cha Rais wa Zanzibar au kiti cha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano.

(6) Makamu wa Rais hatakuwa kwa wakati huo huo Mbunge, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, wala Rais wa Zanzibar.

(7) Endapo mtu ambaye ni Waziri Mkuu, au Rais wa Zanzibar anateuliwa au kuchaguliwa kuwa Makamu wa Rais ataacha kiti cha Waziri Mkuu, au cha Rais wa Zanzibar, kadri itakavyokuwa.

(8) Makamu wa Rais atatekeleza madaraka yake chini ya uongozi na usimamizi wa Rais, na ataongoza na kuwajibika kwa Rais kuhusu mambo au shughuli zozote atakazokabidhiwa na Rais.

 
mwee hawa wote wakwake?
ama kweli ng'ombe hazeeki maini
hii nji ya kipunguani sana
wanashindwa kutatua
matatizo makubwa ya wananji
wana kazi ya kumangamanga
huko maporini
hivi kwanini wasingeliwa na simba
aghrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr
Mmoja kushoto, mmoja kulia, sijui nibadili dini?lol

Halafu pozi la mkono mmoja mfukoni, mmoja kwenye simu, "Like a Pimp" lol
 
Nnachojua mara nyingi makamu wa rais anakuwaga mtu dhaifu sana mwenye uwezo mdogo kiuongozi ambaye hawezi kumfunik rais wake.............makamu wa rais hachaguliwi mtu ambaye ni kichwa anayeweza hata kumrekebiha rais..........yoote ili rais aonekane bora...basi.............makamu wa rais naona kazi yake kubwa ni kumshiki mkoba rais wake na kumfuta jasho///////kwa kifupi sijawahi kuon umuhimu wa makamu wa rais..........eti kwamba "bila cheo cha makamu wa rais hili jambo lisingekuwa hivi"...hakuna
 
Back
Top Bottom