faloyce2001
Member
- Feb 18, 2010
- 24
- 11
Naandika tena kuyataka makampuni ya simu kuweka wazi gharama zao za kupiga simu badala ilivyo sasa ya kuibiwa kwa kukatwa gharama kubwa bila taarifa. Kwa mfano Tigo wanadanganya kuwa gharama ya kupiga simu eti ni sh 1 kwa sekunde wakati ni uongo mtupu. Wadau jaribuni kufuatilia mtagundua gharama za kupiga simu tigo kwenda tigo ni zaidi ya sh 4 kwa sekunde. Tigo acheni wizi huo au tuhamie kwenye basi jekundu? Kama mnataka kufa kufeni wenyewe msife na watu. Ninyi ni Mafisadi kama mafisadi wengine.