Makamba: Tumeshindwa, tumejifunza

Zizu

Member
Sep 9, 2010
67
19
January Makamba on Twitter "You win some you lose some ukikubali hilo life becomes easier tumeshindwa wakati muafaka we will take lessons"

LIKE FATHER LIKE SON
 
Inawezekana Makamaba anajikosha, lakini mimi naona mbali zaidi ya hapo.
Siasa ni mchezo wa ushindani na bahati mbaya ni mchezo mchafu. Lakini kama mchezo wowote, kunakuwa na ushindani. Mchezaji mzuri na anayeheshimika ni yule anayekubali "kushinda na kushindwa".

Tunamwona Makamba anajikosha kwa sababu Watanzania bado hatujakua kidemokrasia kiasi cha kukubali kushindwa, kwa hivyo anapotokea mmoja akakubali anaonekana "ametoka sayari nyengine". Ikiwa Makamba kayasema haya kwa dhati yake ninampongeza, ndio ukomavu wa kidemokrasia huo.
 
Hongera Makamba, hizo ndiyo siasa za kistaarabu, wafundishe na viongozi wako wa chama, maana ndiyo wanaoua hii CCM ni viongozi tu hakuna wengine, wanajiona MUNGU WATU.
 
Mnafiki huyo alikuwa anahonga Tripla A juzi
Ni sababu ya ziada ya kumpa hongera kwani hata baada ya kuhonga wameshindwa na amekubali kushindwa. Wapo wanohonga, wakitoka patupu wanaanza kuleta fujo.

Sincerely, nimefurahi. Siasa za chuki tusizipe nafasi zaidi. Hatutakiwi kuwaona wapinzani wetu kuwa ni maadui zetu, bali watu tunaoweza kujifunza kutoka kwao kutokana na mazuri na mabaya yao.
 
[h=6]John Chiligati
[/h][h=6]HONGERENI CHADEMA KWA USHINDI WA ARUMERU MASHARIKI,DEMOKRASIA IMECHUKUA MKONDO WAKE,HONGERENI SANA CCM KWA KUONYESHA UKOMAVU WA KISIASA KWA KUYAKUBALI MATOKE NA KULINDA AMANI CHINI YA DEMOKRASIA CHANGA,TUJIPANGE,TUNA NAFASI YA KURUDISHA IMANI YA CHAMA CHETU KWA WATANZANIA[/h]Imenipendeza · · Sambaza · kama saa moja iliyopita near Dar es Salaam ·
 
Angemalizia kwa kusema THIS IS THE BEGINNING OF THE END OF CCM AND HON. MAMVI.
 
John Chiligati


HONGERENI CHADEMA KWA USHINDI WA ARUMERU MASHARIKI,DEMOKRASIA IMECHUKUA MKONDO WAKE,HONGERENI SANA CCM KWA KUONYESHA UKOMAVU WA KISIASA KWA KUYAKUBALI MATOKE NA KULINDA AMANI CHINI YA DEMOKRASIA CHANGA,TUJIPANGE,TUNA NAFASI YA KURUDISHA IMANI YA CHAMA CHETU KWA WATANZANIA

Imenipendeza · · Sambaza · kama saa moja iliyopita near Dar es Salaam ·

Kwa hakika kama haya yamesemwa na Chiligati ni kwa sababu kafurahi chama chake kuangukia pua.
Chiligati alitoa chozi kwenye CC baada ya mwenyekiti wake kumchuuza...

Ushindi wa Nassari umeleta raha hata ndani ya CCM, hawashukuru bure hao!

Binafsi nilifurahi kumwona Sioi ukumbini wakati mshindi anatangazwa, ni bahati mbaya sana amefanywa kafara.
 
CCM hawawezi kujifunza chochote when still in power. They must be put on the table a get heart, liver,kidney transplant. In short lazima wapasuliwe na kuundwa upya -nje ya meza ya utawala. Vingenevyo inabidi waendelee kuishi kwa matumaini kwa msaada wa Prof Maji Marefu. THE END!
 
Hongera Makamba, hizo ndiyo siasa za kistaarabu, wafundishe na viongozi wako wa chama, maana ndiyo wanaoua hii CCM ni viongozi tu hakuna wengine, wanajiona MUNGU WATU.

Hakuna siasa za kistaarabu. Ustaarabu katik siasa ni kunadi sera na kuwaacha watu huru wamchague wanayemtaka. Hivi sivyo kwa siasa za TZ chini ya serikali ya CCM. Siasa za kistaarabu haziwezi kuwa na watu wengine kuwa na masanduku yaliyokwishapigiwa kura kabla ya uchaguzi. Mwigulu Nchemba atuambie masanduku ya kura kayatoa wapi kabla ya uchaguzi?

Makamba na Nape wanajifanya wastaarabu kwa kukubali yaashe wakati watu wamepata ushindi kwa jasho jingi. Makamba kama wanataka kukubali ukweli hata kama unauma wauchukue ukweli huu; "CCM inapumulia mashine, nadhani 2014 itakuwa katika chumba cha maiti na 2015 tutafanya mazishi yake". Kama hawataki kukubali ukweli waende wafanye utafiti, na watuambie ni asilimia ngapi ya Watanzania inawaunga mkono. Nawatahadharisha kuwa wasichakachue utafiti maana wao hakuna wanachoaacha kuchakachua.
 
makamba ni miongon mwa watu wenye kuona mbali ndan ya CCM,sielewi ni kwann yuko CCM,coz anauwezo wa kujenga hoja ila kinachomponza ni chama,
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom