Katibu mkuu wa CCM Taifa Mh Yusufu Rajab makamba wiki hii atafanya mkutano mkubwa wilayani Igunga ambapo atapokea maandamano makubwa. habari zaidi kutoka Igunga zinasema kuwa baada ya kupokea maandamano hayo, Mh Rajab Makamba pia atamuapisha Rostam Aziz kuwa kamanda wa vijana wilaya ya Igunga kwa kipindi cha miaka mitano ijayo, shughuli za kumuapisha R.A ilikuwa zifanyike miezi karibu miwili iliyopita lakini ziliahirishwa kutokana na R.A kuwa nje ya nchi kikazi.