BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,009
Date::11/10/2008
Makamba chupuchupu tena
Na Ramadhan Semtawa, Dodoma
Mwananchi
NJAMA za kumngoa Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Yusuph Makamba, zimegonga ukuta.
Kugonga ukuta kwa fitna hizo kumekuja siku chache baada ya baadhi ya wabunge wa CCM, kutaka katibu mkuu huyo angoke ili kukijenga chama.
Matarajio ilikuwa ni kuona ajenda hiyo ikipenyezwa siku ya kwanza ya mkutano huo hapo juzi, lakini haikuwa hivyo na hadi mkutano unamalizika haikuwepo hata katika mengineyo.
Duru za habari za kuaminika kutoka ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu (NEC), zilisema ajenda hiyo haikuwepo kabisa tangu awali kuanza kwa mkutano.
Kwa mujibu wa duru hizo, uamuzi huo wa NEC kutoipenyeza ajenda hiyo unatokana na kwamba waliokuwa wametoa maoni yao ni wabunge katika kikao chao kama wabunge wa CCM.
Hiyo haikuwa ajenda ya mkutano, haikuwepo kabisa, wala hakuna aliyeiingiza hata katika mengineyo, zilisema duru hizo za kuaminika.
Kwa mujibu wea duru hizo, ajenda za mkutano zilihusu zaidi nafasi za majina ya wanachama katika jumuiya na namna bora ya kupata wagombea kuanzia ngazi za mashina, kata na ubunge.
Akijibu tuhuma hizo dhidi yake, Makamba aliliambia gazeti hili kwamba hakuwa na tatizo na maoni ya wabunge hao kwani ni wao waliokaa wakazungumza si chama.
Makamba huku akionekana kuwa na matumaini na kujiamini, alisema hakuwa na wasiwasi kwani hiyo haikuwa ajenda ya chama.
Sikia ndugu yangu, ninachokwambia hayo yalikuwa ni maoni ya baadhi ya wabunge wa CCM, wao walikaa katika mkutano wao si chama, alisema Makamba.
Huku akiwa mchangamfu, aliongeza: Sasa mimi ndiyo nakwambia hivyo, lakini unataka habari za kuokoteza mitaani kaandike, alisema.
Alipoelezwa kwamba, Mwananchi ni gazeti halitaki kuokoteza habari za mitaani kama mengine ndiyo limemtafuta (Makamba), alijibu: Hilo nafahamu ninyi ni watu makini, msisikilize habari za kuokoteza mitaani.
Katibu Mkuu huyo ambaye muda mwingi hupenda kuzungumza kwa kuchanganya maneno ya Kisambaa na kunukuuu aya za vitabu vya dini, alisema alishtushwa pia na taarifa kwamba juzi alitolewa katika kikao kwa muda.
Ninavyokwambia, mimi ndiye nimekuwa naandiki muhtasari wa mkutano, sasa nitolewe nje kivipi? alihoji na kuongeza:
Hapa ninapokwambia ndiyo natoka kumsindikiza mwenyekiti akapumzike, sasa haya mambo mengine ni ya kuchekesha.
Makamba ni Katibu Mkuu ambaye katika uongozi wake, amekuwa akipata upinzani kutoka kwa baadhi ya wanachama wakielezwa kutoridhishwa na utendaji wake.
Joto la hali hiyo lilipanda zaidi baada ya uchaguzi mdogo wa Tarime, ambao CCM ilipoteza kiti hicho.
Makamba chupuchupu tena
Na Ramadhan Semtawa, Dodoma
Mwananchi
NJAMA za kumngoa Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Yusuph Makamba, zimegonga ukuta.
Kugonga ukuta kwa fitna hizo kumekuja siku chache baada ya baadhi ya wabunge wa CCM, kutaka katibu mkuu huyo angoke ili kukijenga chama.
Matarajio ilikuwa ni kuona ajenda hiyo ikipenyezwa siku ya kwanza ya mkutano huo hapo juzi, lakini haikuwa hivyo na hadi mkutano unamalizika haikuwepo hata katika mengineyo.
Duru za habari za kuaminika kutoka ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu (NEC), zilisema ajenda hiyo haikuwepo kabisa tangu awali kuanza kwa mkutano.
Kwa mujibu wa duru hizo, uamuzi huo wa NEC kutoipenyeza ajenda hiyo unatokana na kwamba waliokuwa wametoa maoni yao ni wabunge katika kikao chao kama wabunge wa CCM.
Hiyo haikuwa ajenda ya mkutano, haikuwepo kabisa, wala hakuna aliyeiingiza hata katika mengineyo, zilisema duru hizo za kuaminika.
Kwa mujibu wea duru hizo, ajenda za mkutano zilihusu zaidi nafasi za majina ya wanachama katika jumuiya na namna bora ya kupata wagombea kuanzia ngazi za mashina, kata na ubunge.
Akijibu tuhuma hizo dhidi yake, Makamba aliliambia gazeti hili kwamba hakuwa na tatizo na maoni ya wabunge hao kwani ni wao waliokaa wakazungumza si chama.
Makamba huku akionekana kuwa na matumaini na kujiamini, alisema hakuwa na wasiwasi kwani hiyo haikuwa ajenda ya chama.
Sikia ndugu yangu, ninachokwambia hayo yalikuwa ni maoni ya baadhi ya wabunge wa CCM, wao walikaa katika mkutano wao si chama, alisema Makamba.
Huku akiwa mchangamfu, aliongeza: Sasa mimi ndiyo nakwambia hivyo, lakini unataka habari za kuokoteza mitaani kaandike, alisema.
Alipoelezwa kwamba, Mwananchi ni gazeti halitaki kuokoteza habari za mitaani kama mengine ndiyo limemtafuta (Makamba), alijibu: Hilo nafahamu ninyi ni watu makini, msisikilize habari za kuokoteza mitaani.
Katibu Mkuu huyo ambaye muda mwingi hupenda kuzungumza kwa kuchanganya maneno ya Kisambaa na kunukuuu aya za vitabu vya dini, alisema alishtushwa pia na taarifa kwamba juzi alitolewa katika kikao kwa muda.
Ninavyokwambia, mimi ndiye nimekuwa naandiki muhtasari wa mkutano, sasa nitolewe nje kivipi? alihoji na kuongeza:
Hapa ninapokwambia ndiyo natoka kumsindikiza mwenyekiti akapumzike, sasa haya mambo mengine ni ya kuchekesha.
Makamba ni Katibu Mkuu ambaye katika uongozi wake, amekuwa akipata upinzani kutoka kwa baadhi ya wanachama wakielezwa kutoridhishwa na utendaji wake.
Joto la hali hiyo lilipanda zaidi baada ya uchaguzi mdogo wa Tarime, ambao CCM ilipoteza kiti hicho.