Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,316
- 33,125
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba, amewatibua makatibu wa wilaya wa chama hicho waliogeuka `wabeba mikoba' ya wanasiasa wanaotangaza nia ya kugombea ubunge katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.
Akizungumza na viongozi wa CCM wa wilaya na mkoa katika ziara yake mkoani Kilimanjaro, Makamba alisema baadhi ya makatibu wa chama hicho, wanakiuka kanuni na taratibu kwa kuwa sehemu ya wenye nia za kugombea ubunge.
Makamba alisema tatizo la kuvunjika kwa maadili linakuwa kubwa ndani ya CCM, akitoa mfano wa ushiriki wa makatibu hao kushirikiana na wenye nia za kugombea ubunge kabla ya muda.
Aliwataja baadhi ya makatibu hao kuwa ni Alan Kingazi wa Moshi Vijijini yenye majimbo ya Vunjo na Moshi vijijini.
Mwingine ni Steven Kamote wa Moshi Mjini, kwamba wanashiriki vitendo hivyo na kuivuruga CCM.
"Katibu anabeba mikoba ya wagombea, unatarajia nini, wewe ni Katibu wa wilaya na wagombea wote wanakuja kwako…umesahau kuwa wewe ni mteule wa Kamati Kuu ya CCM, unambebea hadi mikoba yake," alihoji.
Alisema tatizo la ukiukwaji wa maadili na watu kufanya kampeni kabla ya wakati, linazidi kushamiri katika CCM.
Hata hivyo alitoa muda wa siku kumi kwa makatibu hao na wengine kuacha mara moja tabia hiyo. "Kingazi (Katibu wa CCM Moshi vijijini), shame, shame on you," alisema akimaanisha ni aibu kubwa kwa Katibu huyo.
Aidha, alisema CCM haitakubali viongozi wake kujidhalilisha na kukidhalilisha chama hicho kwa matendo yao.
"Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete ameelekeza kuwa kiongozi yoyote atakayevunja maadili na kanuni za chama nimfukuze, halafu nitoe taarifa kwenye Mkutano Mkuu," alisema.
CHANZO: NIPASHE
Akizungumza na viongozi wa CCM wa wilaya na mkoa katika ziara yake mkoani Kilimanjaro, Makamba alisema baadhi ya makatibu wa chama hicho, wanakiuka kanuni na taratibu kwa kuwa sehemu ya wenye nia za kugombea ubunge.
Makamba alisema tatizo la kuvunjika kwa maadili linakuwa kubwa ndani ya CCM, akitoa mfano wa ushiriki wa makatibu hao kushirikiana na wenye nia za kugombea ubunge kabla ya muda.
Aliwataja baadhi ya makatibu hao kuwa ni Alan Kingazi wa Moshi Vijijini yenye majimbo ya Vunjo na Moshi vijijini.
Mwingine ni Steven Kamote wa Moshi Mjini, kwamba wanashiriki vitendo hivyo na kuivuruga CCM.
"Katibu anabeba mikoba ya wagombea, unatarajia nini, wewe ni Katibu wa wilaya na wagombea wote wanakuja kwako…umesahau kuwa wewe ni mteule wa Kamati Kuu ya CCM, unambebea hadi mikoba yake," alihoji.
Alisema tatizo la ukiukwaji wa maadili na watu kufanya kampeni kabla ya wakati, linazidi kushamiri katika CCM.
Hata hivyo alitoa muda wa siku kumi kwa makatibu hao na wengine kuacha mara moja tabia hiyo. "Kingazi (Katibu wa CCM Moshi vijijini), shame, shame on you," alisema akimaanisha ni aibu kubwa kwa Katibu huyo.
Aidha, alisema CCM haitakubali viongozi wake kujidhalilisha na kukidhalilisha chama hicho kwa matendo yao.
"Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete ameelekeza kuwa kiongozi yoyote atakayevunja maadili na kanuni za chama nimfukuze, halafu nitoe taarifa kwenye Mkutano Mkuu," alisema.
CHANZO: NIPASHE