MAKAMBA avishwa GAMBA

Aaron

JF-Expert Member
Nov 18, 2010
3,019
4,693
JANUARY MAKAMBA kavishwa gamba rasmi baada ya kupewa unaibu waziri sasa ni kibaraka wa CCM zile kelele zake bungeni nadhani zitapungua na ZITTO atakosa kampan yake...
 
Sio zitapungua, kwisha kabisa!
Hicho ndicho baba yake alichotaka - awe waziri.
However, hiyo ndo safari ya kuwa waziri kamili in less than two yrs to come!

Read this space!
JANUARY MAKAMBA kavishwa gamba rasmi baada ya kupewa unaibu waziri sasa ni kibaraka wa CCM zile kelele zake bungeni nadhani zitapungua na ZITTO atakosa kampan yake...
 
JANUARY MAKAMBA kavishwa gamba rasmi baada ya kupewa unaibu waziri sasa ni kibaraka wa CCM zile kelele zake bungeni nadhani zitapungua na ZITTO atakosa kampan yake...

Mpuliza tarumbeta kaonyeshwa ndimu/limao. shughuli imekwisha.
 
Ndio maana alikataa kusain form ya kutokuwa na imani na PM.
 
ila jamaa wamemmaliza vibaya, hawezi tena kuongea maana anatakiwa kuitetea serikali.kwisha kazi yake.jamaa hawa ni wabaya kweli kweli kwenye mipango.
 
JANUARY MAKAMBA kavishwa gamba rasmi baada ya kupewa unaibu waziri sasa ni kibaraka wa CCM zile kelele zake bungeni nadhani zitapungua na ZITTO atakosa kampan yake...
January Makamba ni ni CCM na ataendelea kuwa CCM mpaka atoke huko, lakini hilo la uwaziri kama kweli ni mpambanaji hakutaweza kumfanya arudi nyuma. Huu ni mtihani kwake, ndipo Watanzania na vijana wenzake watakamjua ukweli wa yale aliyokuwa akiyapigia kelele.

Kuhusu Zitto kukosa kampani yake, hapa nina mawazo tafauti. Watu kuwa wanatoka vyma tafauti hakuna maana wawe ni maadui. Mnaweza kutafautiana vyama lakini mkawa na mtazamo mmoja (ijapokuwa mkawa mnatumia mbinu tafauti). Kwangu mimi, siasa si uhasama.

Mpinzani wako ni kioo chako cha kuangalia wapi pana kasoro ukajirekebisha. Nguvu ya CDM inatokana na makosa ya CCM.
 
Uteuzi wa January Makamba una walakini. Rais alipaswa alione hili kwamba kuna conflict of interests katika wizara hii ambayo pamoja na mambo mengine ni kuyadhibiti makampuni ya simu ikiwemo Vodacom. Dada yake Mwantum alitumia nafasi yake kupitia Vodacom Foundation kumwandalia mazingira ya ushindi jimboni kwake Bumbuli. Shule zilijengwa na vifaa vya elimu vilipelekwa kwa mgongo wa vodacom social responsibility, hata zahanati zilipata ufadhili wa vodacom. Je January ataweza kudhibiti makampuni ya simu yanayokiuka taratibu za kodi etc likiwemo la dada yake la Vodacom?
 
Uteuzi wa January Makamba una walakini. Rais alipaswa alione hili kwamba kuna conflict of interests katika wizara hii ambayo pamoja na mambo mengine ni kuyadhibiti makampuni ya simu ikiwemo Vodacom. Dada yake Mwantum alitumia nafasi yake kupitia Vodacom Foundation kumwandalia mazingira ya ushindi jimboni kwake Bumbuli. Shule zilijengwa na vifaa vya elimu vilipelekwa kwa mgongo wa vodacom social responsibility, hata zahanati zilipata ufadhili wa vodacom. Je January ataweza kudhibiti makampuni ya simu yanayokiuka taratibu za kodi etc likiwemo la dada yake la Vodacom?

dada yake Mwamvita...
 
Back
Top Bottom