Yussuf Makamba amwinda Reginald Mengi, yeye awataja mafisadi Papa rasmi!

Imekaa vibaya wala haijatulia, why now near election? katumwa na nani? na bado tutasikia mengi sana prior to 2010
 
Mpaka sasa naweza kusema mambo matatu

1.Mzee ni Mbaguzi

2.Familia imemshinda

3.Ana wivu,fitina na chuki na watu anaoshindana nao kibiashara

Haiingii akilini leo kusema mafisadi ni watu watano tu,ambao tena wamehusishwa na kesi za hivi karibuni za kifisadi.

Anogopa kuwataja watu ambao wanafahamika
kabisa kuwa wamertufiksha hapa.

Hataki kuigusa CCM na watu wake kwa kuwa anawaogopa watamaliza.

Ameweza kujenga hoja kuwa mafisadi ni wahindi tu,na tuwabague wakati hao hao wahindi wanatumia na mafisadi mama ambao wapo serikalini,wakubwa ambo mengi anawaogopa kuwasema

Mkuu G,

Mbona sasa unatoka kwenye hoja. Yeye katimiza wajibu wake kwa kutaja 5. Na wewe itisha mkutano leo uongezee wengine kwenye hiyo orodha. Kwani umezuiliwa. Anataja watu ambao ana ushahidi wa kutosha ndo maana hana wasi wasi hata wakienda mahakamani. Naona tunaanza porojo za kupotosha mjadala. Yeye ameonesha mfano na mtu mwingine aje basi ataje wengine. Lazima anazo sababu za kufanya hivyo. Ziwe za wazi au zilizo jificha. La muhimu kwetu ni kumpongeza na kujadili nini kinatakiwa kufuata baada ya hapa.
 
Labda wewe ndiyo une-clarify wazi hivi hao jamaa waliotajwa hapo ni weupi, kwa standard yako! Mie sioni hata kidogo lipo suala la rangi; hapa ni ufisadi tu; mweusi au mweupi ufisadi ni ule ule; nyie ndiyo ndumila kuwili. Hapo chini umetaja dini; lo; hapo ndipo tunachoshana kabisa. Kwa nusubongo yako umeongelea vitu ambavyo vinakutawala wewe katika hizi discussions na maamuzi, Dini na Rangi ya mtu; hapa hamna vyote viwili; bali ni Utaifa; hata hao wewe uliowataja ni WaTanzania kwa hiyo punguza hiyo jazba. Mengi kafanya hatua moja mbele labda ungeendeleza jingine hapo huwezi kum-demoralise mtu!

Asante mkuu, watu kama hao wako wengi tu na humu JF ndio wanazidi kushamiri, yaani wao kila kitu kinatazamwa "kidini"!! Yaani wao kila likitajwa jambo wanaangalia wa dini yangu huyu kwanza. Hii ni mbegu mbaya kabisa ambayo naamini kama watanzania wataacha iendelee kukua itaangamiza kabisa taifa letu,.... kama kumtu katukosea tunaangalia ukweli, ni kweli kakosa? sio tuangalie dini! Maendeleo ya kweli tutayapata kwa kujitambua kwamba sisi ni watanzania na tunatakiwa kuwa wazalendo wa kweli kwa nchi yetu. Hayo ya dini yatatupeteza tu.....nyumba za ibada si zipo! tukashinde huko.
 
Mkuu hii ni janja ya nyani tuu,mahindi yanakomaa shambani,Wakati umefika kujitakasa kwa kila njia hata kama ni kuyatosa magabacholi wazawa wasalimike haya.Mengi ni kipaza sauti tuu wala asiudanganye umma waWatanzania,
 
Mzee mengi wala usijali...MIMI NA BAADHI YA WATANZANIA WENGI TULIOKO VIJIJINI TUPO NYUMA YAKO..na mafisadi waambiwe kuwa WE DONT DIE WE MULTIPLY...mungu ibariki Tanzania yas NYERERE.
 
Je vita yetu ya kupambana na umaskini itafanikiwa kwa kuwataja tuu mafisadi hadharani??

Kuna haja ya kupambana na mafisadi wenyewe au wale wanaowapa nafasi nzuri ya kutuibia???

Hapa jamvini naomba tujadili kwa kina na mnisaidie kuelewa zaidi!!!!!

Bado ninaamini ccm ndo tatizo kubwa la umaskini tunaoendelea nao mpaka sasa....
 
Makamba mwenyewe siyo msafi, hilo tunalifahamu. Tunaweza kusema anakumbatia mafisadi, kama moto umeanza kuwawakia hao mafisadi naye babu Makamba aweke kichwa maji, moto huo kuuzima ni ngumu.

Mungu Ibariki Tanzania.
 
Risk taker!!

Big five to Regnald Mengi!
Katika taarifa aliyotoa MwEnyekiti wa IPP kuna kitu kubwa ambacho sijui kwa nini anachelea kukitaja nacho ni suuport ya watu waliokuwepo na waliopo serikalini (zote zilizopita kuanzia ile ya Marehemu Nyerere na mpaka hii awamu ya nne ya JMK) ambao ni wabia wakubwa waliowezesha kufanikisha ufisadi!!

Mafanikio hayo yamewezeshwa kwa viwango mbali mbali katika wizara zote bila kubagua;mashirika ya umma,Benki Kuu;mabenki ya biashara;vyama vya siasa;asasi za kiraia na vyuo vikuu! Wizara ya fedha/hazina ndiyo mhimili mkuu katika kuwezesha uharamia huo because it is said that ''it takes two to tangle''
Rai yangu ni kwamba basi tusiwe waoga tuwataje kwa majina watu wote na wanaofahamika waliokuwa watumishi wa umma kama {akina Edward Lowasa;Robert Mboma; Daniel Yona;Gray Mgonja; Benjamin William Mkapa na familia yake; Cleopa Msuya;Balozi ALIYEKUWA SA jina lake nimelisahau} bila kwasahau akina MASHA ;Nizar Karamagi na wengine wengi tu!! ambao ghafla bin vuu wamekuwa matajiri wa kutupwa!

Na kama kweli JMK sio mmoja wao basi wote wahojiwe watueleze huo utajiri wao waliupata wapi? Wakati tumekua na kucheza nao kuanzia chandimu mara wana makasri Tahadhari Mkapa asiseme nina wivu wa kike!
Naweza nikaandika hata kurasa elfu kutoka kichwani mwangu ila nawaachia na nyie mpasue Bongo!!

Mwisho nimpongeze kaka yangu Mengi kwa ujasiri wa kumtaja Subash Patel hapo umepiga Ikulu ya Mwinyi!! Bado hujawagusa akina Dewji;Bahresa na wale walikimbia Debt conversion mashamba ya Mkonge!! Akina Mkapa walidesa kwa huyu jamaa kwani ni mkimya humdhanii wala hutamskia popote!!! Tete heeee !!! Yahh!!!Simba mwenda pole iko gonjwa!!!! Kula nyama nyingi?
Mengi aanika mafisadi papa

KATIKA hali isiyo ya kawaida, Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni za IPP, Bw. Reginald Mengi ameibuka na kudai nchi inahujumiwa kundi dogo la watu aliowaita 'mafisadi papa' na wamejiandaa kutoa roho za wanaowapinga kwa gharama yoyote.

Bw. Mengi alitoa kauli hiyo jana Dar es Salaam katika mkutano wake na waandishi wa habari na kueleza kuwa mafisadi hao wameifikisha nchi pabaya kwani hawataki kuguswa.

Aliwataja watu hao wakiwemo wafanyabiashara na wanasiasa (majina tunayo) na kueleza kuwa wameivuruga nchi kwa kiasi kikubwa.

"Nia njema ya Rais Jakaya Kikwete ya kupambana na mafisadi na aina zote za uovu zimewashtua mafisadi na sasa wamecharuka wanapambana na watu wote wanaomsaidia Rais kupambana nao kuwazuia wasiendelee kuitafuna nchi,"alisema Bw. Mengi.

Bw. Mengi alisema mafisadi hao wanatuhumiwa kuiba mabilioni ya fedha za wananchi, na baya zaidi, yamehamisha pesa hizo nje ya nchi.

Alisema wanaotuhumiwa wanahusishwa na karibu ya kila kashfa kubwa iliyoibuka hapa nchini.

"Jitihada kubwa za Rais Kikwete kuleta maendeleo na Maisha Bora kwa kila Mtanzania zinadhoofishwa na wizi mkubwa wa rasilimali za Taifa,"alisema Bw. Mengi na kuongeza;

"Bado Watanzania wengi wanaandamwa na umasikini mkubwa, hawajui hata mlo mmoja kwa siku utatoka wapi"

Bw. Mengi ambaye pia ni mfanyabiashara maarufu nchini, alisema cha kusikitisha ni kwamba pale Mtanzania mwema mwenye uwezo anaposaidia jamii kuondokana na umaskini, mafisadi wamekuwa wakipiga kelele kuwa misaada ya aina hiyo ina agenda na kupinga kwa kutaka Watanzania wafe njaa na matatizo mengine.

"Inavyoonekana nia ya mafisadi hao sasa ni kuvuruga nchi na si ajabu wakaunga mkono matatizo yanayotokana na kampuni ya Kuvuna na Kupanda mbegu, DECI na Watanzania wakabaki wakifukuzana na wachungaji bila kujiuliza ni kina nani hasa wanachochea vurugu hizo,"alisema.

Bw. Mengi alisema DECI imeleta matatizo makubwa katika nchi mbalimbali duniani, ambapo iliiangusha Serikali ya Albania na kwamba hatma yake ikiendelea kuchochewa na watu wapenda vurugu, italeta matatizo makubwa hapa nchini.

Alisema kuwa mafisadi papa hao hawaibi rasilimali tu, bali wanaiba pia muda, badala ya wananchi kutumia muda katika shughuli za maendeleo, wanajikuta wakiutumia kupambana nao.

Bw. Mengi alidai mafisadi hao wanatumia fedha walizoiba kuanzisha magazeti ya kujenga kiburi cha kudharau Watanzania, kuwatukana na kuwanyanyasa.

"Inakuwa ni kesi ya mwizi kumkimbiza na kumpiga aliyeibiwa. Hata sasa hivi mafisadi hao wanaendelea kutumia uwezo wao wa kiuchumi uliotokana na wizi wa rasilimali za nchi kuwashawishi na kupata miradi mikubwa mikubwa kwa kutumia majina tofauti tofauti huku wakipuuza kabisa kelele za wananchi kuhusu ufisadi wao,"alisema.

Alisema Watanzania wanaolia na ufisadi ni mamilioni wakiongozwa na Rais Kikwete, lakini wachache waliojitokeza na wanajulikana kwa majina.

Alieleza kuwa hata hivyo kuna tetesi kwamba mafisadi papa wamedhamiria kuwatokomeza kabisa wapinga ufisadi wanaojulikana kwa majina.

Alisema mafisadi hao ni lazima wajue kwamba iwapo wapambanaji hao wa ufisadi watadhuriwa kwa njia yoyote, ndani au nje ya nchi, watawajibishwa na Watanzania.

Alisema mafisadi hao wanafanya kila wawezalo kuhakikisha Watanzania wanaopiga vita ufisadi, wanaangamia kwa njia mbalimbali zikwemo sumu, ajali au kwa kupigwa risasi ili kuondoa ushahidi.

"Watanzania mtasikia tu kwamba fulani amefia nje ya nchi na mtachukulia kama kitu cha kawaida kumbe mafisadi ndio waliotekeleza azma yao, ni lazima muwe macho kwani wanataka kuisambaratisha nchi,"alisema.

Aliwataka Watanzania kujiuliza mafisadi wanapata wapi ujasiri, majigambo, dharau, nguvu za kuwatukana na kuwanyanyasa ?

Alisema mafisadi wote hususani wale wanaotuhumiwa kuwa mafisadi papa ni lazima washughulikiwe, la sivyo wataiyumbisha na kuitikisa nchi na kwamba ni lazima Watanzania waone kwamba sasa nchi imefika mahali pa kusema imetosha.

Bw. Mengi alisema amejitoa muhanga kupigana vita dhidi ya mafisadi na kubainisha kuwa yeyote atakayekerwa na hatua ya kuitwa 'fisadi papa 'aende mahakamani ili wakapambane kisheria.

SOURCE; MAJIRA
 
Je vita yetu ya kupambana na umaskini itafanikiwa kwa kuwataja tuu mafisadi hadharani??

Kuna haja ya kupambana na mafisadi wenyewe au wale wanaowapa nafasi nzuri ya kutuibia???

Hapa jamvini naomba tujadili kwa kina na mnisaidie kuelewa zaidi!!!!!

Bado ninaamini ccm ndo tatizo kubwa la umaskini tunaoendelea nao mpaka sasa....

kaka nyauba nadhani hatua ya kwanza ya kusolve any problem ni kukubali kuwa tatizo hilo lipo...nalo ni ufisadi, pili ku-identify key elements/actors kwenye hilo tatizo...i.e. kuwataja wahusika kama alivyofanya mzee wetu mengi na tatu ni ku-set/kuweka mipango au mikakati ya kupambana na hao actors wakuu...after mapambano ni kuset new system itakayozuia kujirudia tena kwa tatizo hilo.
nadhani mengi amesema na kutusaidia ku-identify top 5 fisadis..sasa ni juu yetu watanzania ku-deal nao hawa...haiwezekani every mega scam wawepo wao tuu...name any scam in this cpountry ambayo wao hao top 5 hawamo....ni maoni tu coz we dare to talk openly with our heart and inner parts of our minds.
 
Mkodeleaji and the Like;
Mengi ametaja mafisadi anaowajua, na sisi wote tunawajua. That is fine, he is brave and then he played his part.
Sasa wewe Mkodoleaji (na the like); mnajua wazi kuwa Mengi anawaacha wengine pembeni, kama Muungwana JK, yes, mie naamini kabisa JK is a major culprit; (and I have stated this before); Sasa ni zamu yako kusimama na kusema JK ni fisadi mkuu, you have that freedom, lakini kumkandamiza Mengi kwa kazi nzuri aliyoifanya si vizuri. Kumbuka kuwa unavyoanza kum-discourage mtu kama huyu shujaa, then you demorlarise others also. It is then your next part to take on JK; let us go one step forward instead of backward!
Mkuu, licha ya kwamba uchambuzi wa 'negativity' sio kitu kigeni, LAKINI hii itaigharimu Tanzania safari ndefu sana sababu ya uchanga na umasikini wa nchi yetu. Tunajaribu kujenga 'mentality' isiyomwafaka kwa janga la ufisadi ambao wote tunajua kwamba bila ya kuutokomeza hakuna hatua tutakayopiga. Inabidi tubasilike na kufumba macho pale tunapopata mtu anayeweza kujitokeza na kukemea jambo ambalo tunajua linaiangamiza nchi. Mengi, Mwakyembe, Kilango, ..., wamethubutu kusema wazi kile ambacho hakuna yeyote anaweza kupinga kwamba sio cha kweli. Ukiangalia nafasi za hawa watu wote, wanaweza kukaa kimya na wakaendelea kula kuku kwa uhai wao uliobaki, lakini wanasema kwa kuwa wanaguswa na wanataka tubadilike.

BTW, Mengi amesema nchi inatafunwa na watu wasiozidi kumi, yeye ametaja watu wasiozidi watano, ni vema kama Mkodoleaji et al. wangejitokeza wakamalizia list ikiwa pamoja na kumtaja JK (ambaye Mengi ameshindwa kumtaja pengine kwa sababu za kidiplomasia).
 
Mengi anasumbuliwa na Maradhi ya UGOZI na ndio maana aliowataja wote ni WEUPE, Hii ni hatari sana kwa TANZANIA yetu hasa kwa wakati huu ambao CCM imeifikisha Nchi pahala pabaya kwa kuwaweka Watanzania katika Umasikini wa Kutupwa.Kauli yake inaweza kuchochea fujo kati ya Sisi Walalahoi na wale Weupe wote Wenye Kiapato kwa Dhana tu ya Kuwa Wote ni MAFISADI.

Ukitizama kwa umakini kauli yake imeficha jambo moja kubwa nalo ni lile alilolisema Makamba kuwa Mengi anaajenda ya SIRI ya Kuimaliza CCM pamoja na KIKWETE sio Kweli kama anampenda Kikwete hampendi hata kidogo na anampiga Vita kwani likitokea lolote baya kwa kauli ya Mengi litammaliza Kikwete Kisiasa.

Hivi Mengi anamficha nani kama nae sie FISADIIIII Hii inajulikana au alishindwa nini Kumtaja MKAPA, YONA , MRAMBA, CHENGE, MARANADA IDDI SIMBA, KARAMAGI nk au kwa kuwa hawa ni WEUSI na Wengi wa Dini yake Mengiii ? au Kwao ni Kumojaaaaaaaa.

CCM Yote imejaaa uchafu uliokithiri akiwemo na yeye Mengi kama mwanachama wa CCM Hivi karibuni Mengi huyu huyu MNAFIKI alimwaga MIlioni Mia moja Kwa Umoja wa WANAWAKE CCM Kule mkowani Mbeya akijuwa kuwa ni Umoja wa Chama Cha Mafisadi sasa aeleweke nini Mzee Huyu kama sio Ndumila Kuwili wa Ufisadiiiiiiiiiiiii.

Makamba mwenyewe siyo msafi, hilo tunalifahamu. Tunaweza kusema anakumbatia mafisadi, kama moto umeanza kuwawakia hao mafisadi naye babu Makamba aweke kichwa maji, moto huo kuuzima ni ngumu.

Mungu Ibariki Tanzania.

Naona watu wengi wameshupalia kwa nini kataja watu wenye rangi nyeupe ...lakini si ndio anao ushahidi wake na amewapa nafasi ya kwenda mahakamani kama wanaweza.

Pili nimesikiliza kwenye audio yake amesema neno moja, kuwa unaweza kubadilisha/kung'oa makatibu wakuu, mawaziri au watendaji wengine kwenye mawizara kwa kosa au tuhuma za kupokea rushwa kutoka kwa mapapa lakini ukaonekana ni mchezo wa kuigiza tu .....dawa iliyo kamilifu ni kudeal na mapapa wenyewe watoaji.
 
Hao mafisadi kawaanika vipi? Kamtaja nani? Kipi kipya alichosema? Mbona tunaridhika kirahisi hivi? Hamna substance katika alichoongea bali posturing tu.

Amandla........
 
Siku zotehuwa nachannganyikiwa na sioni kama ni ukweli:

1. Kumtenga Kikwete na ufisadi
2. kuwa kikwete ana mipnago mzuri na nchi!
3. Kuwa hawa wote hawawataji hao mafisadi na hawana mipango ya kuwapeleka mahakamani kazi kusema tu!

Kama Mengi na mapesa yake hana mpango wa kumshtaki ngau fisadi mmoja kama demo, je mimi ninayetiokea nyarugusu mwanza nitasemaje? sina uwezo wa kupata mwanasheri na kumlipa!

Hiii imebaki wimbo wa mafisadi, mafisadi thinga are not going on, JK wanayemsifia ndiye mwenye Rungu na madaraka yote juu ya mafisadi lakini wapi!!!!!!

anawahamisha toka huku kwenda kule!

Ndani tatizo ni rais, hwa wote watabadilika tu JK akibadilika, hawa wote watafanya watakavyo kama JK naye yuko kama wao.

Mengi kweli unaheshimika, lakini UNAPOTOA KAULI REJEA, ZISIZOPNA IMPACT YOYOTE -zaidi ya publicity, BASI TUTACHEZA TU HUU WIMBO, miaka inaenda....
 
Hao mafisadi kawaanika vipi? Kamtaja nani? Kipi kipya alichosema? Mbona tunaridhika kirahisi hivi? Hamna substance katika alichoongea bali posturing tu.

Amandla........


Naona tuko kwenye boti moja kaka , thanks

Hii style ya kutaka kupendwa na jamii tumeigundua, hana jipya!!!!!!!!!
 
Mkuu hii ni janja ya nyani tuu,mahindi yanakomaa shambani,Wakati umefika kujitakasa kwa kila njia hata kama ni kuyatosa magabacholi wazawa wasalimike haya.Mengi ni kipaza sauti tuu wala asiudanganye umma waWatanzania,

Ujumbe umefika
 
Mkuu G,

Mbona sasa unatoka kwenye hoja. Yeye katimiza wajibu wake kwa kutaja 5. Na wewe itisha mkutano leo uongezee wengine kwenye hiyo orodha. Kwani umezuiliwa. Anataja watu ambao ana ushahidi wa kutosha ndo maana hana wasi wasi hata wakienda mahakamani. Naona tunaanza porojo za kupotosha mjadala. Yeye ameonesha mfano na mtu mwingine aje basi ataje wengine. Lazima anazo sababu za kufanya hivyo. Ziwe za wazi au zilizo jificha. La muhimu kwetu ni kumpongeza na kujadili nini kinatakiwa kufuata baada ya hapa.

Sio kupotosha amewataja wakati na yeye yumo humohumo ,kila siku tunasema anaeuchukia ufisadi ajitenge ,maana nusu ya wafuasi wa Sultani CCM utawasikia wakisema kama Mengi na wengine kumshinda yeye ,lakini bado wanaonekana wamejibanza humohumo na hawawachukulii sheria yeyote ile si kuwafukuza uanachama wala kuvuliwa madaraka ,wale walioshitakiwa naamini kabisa wanendelea kupokea mshahara wao na wakishinda wanaweza kabisa kuidai serikali fidia ya kuharibiwa jina.

Tunasema wajitenge na Chama Tawala ambacho ndicho chimbuko la ufisadi ,wakae pemeni kuungana na WaTz wengine katika vita hii ,Mengi amewataja wote ni kutoka Chama Cha CCM halafu huko huko anawajazia mipesa , Sasa uhakika gani kwamba feza alioyoichomeka kwa umoja wa wanawake wa CCM huwa hapo sipo zinapoishia isipokuwa ni njia tu ya kupitia ili zifike kunakohusika.

Kuna vyama vya upinzani vinapigana vita hii ya ufisadi kwanini Mengi ikiwa anajiamini asivisaidie kuvitilia fedha ili kufanikisha ushindi lakini badala yake anawajazia mafisadi mapesa kwenye account zao. He is the one hakuna haja ya kupongezwa kama kupongezwa basi wanaohitaji kupongezwa ni wale wanaopanda juu ya majukwaa na kusema CCM ni Chama Cha mafisadi na si kupongezwa Mengi ,wapinzani hawamhitaji mtu kutoka upande wa CCM katika vita hii ,hii ni vita ya upinzani dhidi ya Chama Tawala ,Mengi anamsifu Kikwete wakati ushindi wa 2005 wa Kikwete unahusishwa na fedha ya ufisadi nasema upinzani hauhitaji kampeni za Mengi maana tatizo linaonyesha bado tupo pale kwenye Mwakiembe na Rostam confrontations ,Mengi anaendeleza kwa kutoa sapoti kwa mlango wa nyuma ili kubamiza upande wa Rostam na sio anapiga vita ufisadi kwa kuwa ana uchungu sana na raia ,hivi ni vita ndani ya CCM na sio kuwasaidia watanzania kujikwamua katika hali duni ya maisha ,vita vya kumkomboa Mtz vitaletwa na kusimamiwa na walio nje ya CCM na sio waliondani.
 

1. Katika statement yake amesema kuwa mafisadi wakubwa wanaoimaliza Tanzania hawazidi kumi.

2. Na yeye akaamua kuwataja watano ambao amewaita 'mafisadi papa' -

1. Rostam Aziz, 2. Tonil Somaiya, 3. Yusuf Manji, 4. Subash Patel na 5. Jeetu Patel.

Amesema hawa wanatuhumiwa kuiba mabilioni ya wananchi na mbaya zaidi fesha hizo wamezihamishia nje ya nchi.


- Hapa hakuna kawaida, majina yametajwa rasmi sasa ni wajibu wetu kuchunguza wameiba nini, wapi? Wameshirikiana na nani?

- Tusiwe wazembe wa kusubiri Mengi atufanyie kila kitu, ndio maana tunakwama, maana tufanyiwe kila kitu mpaka kufikiriwa, that is pathetic!

FMES!
 
Makamba and the whole CCM are bunch of liars, they don't deserve more than a life jail time
 
- Afadhali ya Mengi, kuliko upinzani wa CUF na Zitto, wanayecheka mpaka jino la mwisho na JK huku wamevaa kanzu wanakwenda kwenye pilau sio Lipumba na Seif? Unajichekesha na "fisadi" na kwenda kula naye pilau?

- Halafu unamlaumu Mengi anayewachapa bakora fisadis?



FMES
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom