Yussuf Makamba amwinda Reginald Mengi, yeye awataja mafisadi Papa rasmi!

si wajitokeze kina Rostam na Manji na wenyewe walaani yaliyotokea Benki Kuu angalau tujue wanakerwa? Mbona hadi leo Lowassa na kina Patel na kina Don Ande hawajajitokeza kusema hata jambo moja dhidi ya EPA, na wizi wa mamilioni yetu Benki Kuu?

Wote hawa wana matatizo yao, lakini kumuweka Mengi kwenye kundi la wezi wa Benki Kuu ni kukosa kuwa wakweli.

Leo hii Mkapa aliyekuwa Rais wakati wizi mkubwa unatokea nchini hadi leo hajajitokeza kulaani yaliyotokea na badala yake amejikunyata kimya! Kina Makamba badala ya kulaani yaliyotokea wanataka kina Mengi wanyamaze! Kina Kaboyonga badala ya kulaani wizi wa fedha zetu wanataka kina Slaa wanyamazishwe! tukisema tumelaaniwa au tumerogwa watu wanasema tunajitukana!

Sasa hapa wanajitokeza wengine kujaribu kuneutralize alichosema Mengi ili tusipime madai dhidi ya wezi wa utajiri wetu! Kama kina Manji, Patel, Rostam na wenzao wanaona wameonewa na kuwa wanasingiziwa waende mahakamani! Kama wanashindwa basi na wao angalau wajitokeze na kulaani ufisadi nchini! Hawawezi; ufalme hauwezi ukajipinga wenyewe halafu ukasimama!

Kama na wenyewe wanajua Mengi ana mambo yake ya kifisadi wajitokeze basi wayaseme na kuonekana ni watetezi wa taifa basi..
kama umenisoma vema ni kwamba namuoan mengi kama msanii tu.....kila mwenye akili ya kawaida anajua kabisa hao aliowataja sio mapapa kama alivyosema papa ni JK mwenyewe na yeye anampa shavu JK kuwa yu msafi...
 
si wajitokeze kina Rostam na Manji na wenyewe walaani yaliyotokea Benki Kuu angalau tujue wanakerwa? Mbona hadi leo Lowassa na kina Patel na kina Don Ande hawajajitokeza kusema hata jambo moja dhidi ya EPA, na wizi wa mamilioni yetu Benki Kuu?

Wote hawa wana matatizo yao, lakini kumuweka Mengi kwenye kundi la wezi wa Benki Kuu ni kukosa kuwa wakweli.

Leo hii Mkapa aliyekuwa Rais wakati wizi mkubwa unatokea nchini hadi leo hajajitokeza kulaani yaliyotokea na badala yake amejikunyata kimya! Kina Makamba badala ya kulaani yaliyotokea wanataka kina Mengi wanyamaze! Kina Kaboyonga badala ya kulaani wizi wa fedha zetu wanataka kina Slaa wanyamazishwe! tukisema tumelaaniwa au tumerogwa watu wanasema tunajitukana!

Sasa hapa wanajitokeza wengine kujaribu kuneutralize alichosema Mengi ili tusipime madai dhidi ya wezi wa utajiri wetu! Kama kina Manji, Patel, Rostam na wenzao wanaona wameonewa na kuwa wanasingiziwa waende mahakamani! Kama wanashindwa basi na wao angalau wajitokeze na kulaani ufisadi nchini! Hawawezi; ufalme hauwezi ukajipinga wenyewe halafu ukasimama!

Kama na wenyewe wanajua Mengi ana mambo yake ya kifisadi wajitokeze basi wayaseme na kuonekana ni watetezi wa taifa basi..

Mwanakijiji hakuna anayejitokeza kuneutralise alichosema, bali aliyeneutralise ni yeye mwenyewe. Yeye kamsifia JK ambaye ni zao la ufisadi na pia amesifia mahakama ambazo wananchi wanakerwa nazo bado (kumbuka ule mgomo wa mahabusu wakati wa kesi ya Dito). Sasa hilo linafanya wengine tujiulize lengo la Mengi ni nini kujipendekeza au kupambana na ufisadi. Anapofanya hivyo ndiyi anafanya tukumbuke historia yake mwaka 1995 alipotishia wananchi kuwa wakichagua upinzani watauana kama Rwanda, na alikuwa akionyesha kipindi maalum cha amani. Kwa hiyo unakuta Mengi ni mtu mwenye tabia ya kujikomba ili afanikishe biashara zake. Sasa wewe kuja kumtetea hapa na kudai wengine wayaseme ni kukwepesha tu hoja. Hapa tunajadili hoja za Mengi na hao nao wakija na hoja zao tutawajadili vile vile. Hawa watu jamii ya akina Mengi ni wapotoshaji tu, umefika wakati wa uchaguzi ambapo ingestahili watu wawashauri wananchi wa kawaida wachague viongozi wazuri wao huanza kuwasifia watu fulani na kudai eti ni viongozi wasafi na waadilifu. Usanii mtupu. Wakati dili la rada linakamilishwa JK alikuwa Waziri wa Fedha, wakati akina CHavda amekula fedha za Benki akishirikiana na Idris Rashid, Kikwete alikuwa waziri, wakati IPTL inaingia JK alikuwa waziri, wakati wanachukua mapesa BoT kwenye akaunti ya EPA kwa kushirikiana na Ballali, ni JK huyo huyo ambaye alisaidiwa ili aingie ikulu, wakati Richmond JK huyo huyo alikuwa Rais aliyeubariki huo mpango. Leo anajitokeza mtu anayejitapa ni kamanda wa kupambana na ufisadi na kuanza kumsifia kwa nini tusimuone msanii??
 
kama umenisoma vema ni kwamba namuoan mengi kama msanii tu.....kila mwenye akili ya kawaida anajua kabisa hao aliowataja sio mapapa kama alivyosema papa ni JK mwenyewe na yeye anampa shavu JK kuwa yu msafi...

Hiyo ni strategy wewe kumbe na wewe ni white. Utaazaje kumwambia baba yako kikojozi? itabidi uzunguke tu kwa kusema nasikia harufu ya mkojao lakini massage imefika!
 
kama umenisoma vema ni kwamba namuoan mengi kama msanii tu.....kila mwenye akili ya kawaida anajua kabisa hao aliowataja sio mapapa kama alivyosema papa ni JK mwenyewe na yeye anampa shavu JK kuwa yu msafi...


Unahitaji maombi bila shaka...
 
Hiyo siyo strategy huo ni USANII MTUPU
mengi ningemuona hero kama angeweza kutamka kuwa JK,mkapa na watendaji wakuu wao ndio fisadi namba moja.....maana tujiulize hio mikataba hawa akina jetu walisaini wakiwa na nani? kama sio hawa mengi anawaita wasafi......

....mikataba wameandaa serikali wakaitana na akina jetu wakainishana ila leo hii wengine wawe wasafi wengine ati mafisadi.......

.....alafu huyu mengi mbona hasemi mafisadi wakina chenge,mramba yeye kakomaa na hawa wafanya biashara tu....unafikiri mie mwananchi sitakuwa na machaka labda ana wivu wa kibiashara?
 
Najiuliza...Mengi anataka kutimiza lengo gani hasa.??

Lengo lake lipo wazi, amekerwa na unyonge wa watanzania ambao kwa kiasi kikubwa unasababishwa na mafisadi papa. Labda swali lako lingeelekezwa kwa viongozi wa CCM kama kina Makamba, kuwa lengo lao ni nini kuwanyamazisha kina Mengi na wanaofanana naye kwenye vita dhidi ya ufisadi.
 
I agree totally...you cant bite the hand that feeds you, labda Mengi afanye hizi bidii kujulisha wananchi lakini sio kutegemea kwamba chochote kitafanyika juu ya hawa jamaa.

Kauli kama hizi ndizo zinazolenga kuwakatisha tamaa watu wanaojitokeza kupinga ufisadi. Kama serikali haichukui hatua sisi kama wananchi ndio wenye wajibu wa kuifanya serikali ichukue hatua. Mafisadi na wapambe wao wanatucheka na kutudharau kwa sababu ni sisi wapiga kura ambao tutawarudisha madarakani hao hao wawakumbatio mafisadi. Kitu kimoja ambacho ni wazi ni kuwa watawala wasitegemee watakaa madarakani daima. Nchi nyingi za kiafrika ikiwemo Sierra Leone, Ivory Coast n.k zilianza kumomonyoka hivi hivi kama tunavyoona Tanzania. Watu wachache mafisadi kuishikilia nchi mikononi mwao sio jambo la kujivunia hata kidogo. Tuwaunge mkono watu wanaojitokeza kupambana nao waziwazi...
 
It's sad that a couple of days ago tulijiuliza je baada ya kudiscuss JFthen what? Haya sasa tuliyo yazungumzia humu Mengi katumia Media Power yake kufanya wananchi woote wajue...je do we stand by him au tunarudi kudiscuss whether Mengi nae fisadi?

Hapa ndo tunapoachwa na wakenya ,we got the backing of one powerful media house...what else to we need??... Lets hit the streets sio kurudi humu..
 
Mengi anaweza kuwa na nia njema ya kupambana UFISADI,lakini mbona MENGI anakuwa mbaguzi kiasi hiki?Ubaguzi nao ni aina ya UFISADI.
Nasema baba yangu MENGI ni mbaguzi kwa sababu kwenye taarifa yake amesema MAFISADI wanaoitafuna nchi hawazidi kumi na kwa msisitizo akawataja walau watano,kati yao hakuna MTANZANIA KWA ASILI.JE KWANINI ASITAJE MASIFISADI WOTE ILI KUJUA KAMA WOTE SI WAZAWA WAFUTWE URAIA ?AU KUNA MASWAHIBA WAKE WAZAWA AMBAO ANASHIRIKIANA NAO KUFISADI NCHI?
Ushauri kwa baba MENGI,JIWEKE UPANDE SALAMA KWA KUWATAJA WOTE UNAOAMINI NI MAFISADI WANAOIFILISI NCHI AMBAO UNASEMA HAWAZIDI KUMI.
 
kama umenisoma vema ni kwamba namuoan mengi kama msanii tu.....kila mwenye akili ya kawaida anajua kabisa hao aliowataja sio mapapa kama alivyosema papa ni JK mwenyewe na yeye anampa shavu JK kuwa yu msafi...

Si kweli; JK hawezi kulinganishwa na hawa jamaa; tatizo la JK siyo kuiibia nchi yetu bali ni kushindwa kuongoza inavyopaswa na kuwa dhaifu kiuongozi. JK amewekwa na hawa watu na ndiyo wana call the shots! Ndiyo watu wenye nguvu kuliko hata Rais wa nchi. Ndio maana wana ujasiri wa kufanya wanalotaka kwa sababu kwao JK ni kama kikaragosi wao.

Tatizo ni kuwa kikaragosi kinaonekana kimekata kamba na kimepata uhai wake wenyewe. Na hili ndilo tunalolishuhudia. JK pamoja na udhaifu wake wote wa kiuongozi ambao nimeandika hapa mara nyingi halingani hata kidogo na hawa watu ambao wametumia udhaifu huo kujijengea himaya ya ufisadi.

Na leo wametajwa kwa majina yao. Kama wao wanajua JK ndiye papa wa ufisadi basi wao kina Manji, Rostam, Patel na wenzao wasimame kumtaja! Si wanajua mambo yake?
 
kikwete kachanganyikiwa nadhani....maana wasaidizi wake hawamsikilizi..msaidizi muaminifu lazima ufuate imani ya kiongozi..,sasa unapokuwa huna msimamo..au itikadi ..principles ..wasaidizi kila mmoja ana kuwa na msimamo wake..

huwezi kuwa na msimamo wako ..na ukabaki kuwa msaidizi wangu lazima nikutowe......msimamo tofauti na wangu utanishauri sirini..na nikiukubali utaitwa msimamo wangu...uongozi si lelemama!!!

sasa ukiona rais anaaza kuwa na wasaidizi waaminifu nje ya circle halali ya kikatiba ..kina mengi,anna kilango,kimaro..basi ujuwe na hao wasaidizi wapya wana malengo yao...mema au mabaya....!! ndiyo ilivyo....ndio maana wakaweka utaratibu ...sasa rais anaaza kutafuta faraja nje ya cabinet..theres a serious problem ..kama anashindwa kuwaambia asiopenda mienendo yao...nooooo!
 
Its sad that a couple of days ago tulijiuliza je baada ya kudiscuss jf then what?? haya sasa tuliyo yazungumzia humu mengi katumia media power yake kufanya wananchi woote wajue...je do we stand by him au tunarudi kudiscuss whether mengi nae fisadi??
Hapa ndo tunapoachwa na wakenya ,we got the backing of one powerful media house...what else to we need??...lets hit the streets sio kurudi humu..

Kwa hiyo hata Rostam angekuja kuongea na kulaani ufisadi na wewe ungemsapoti kwa sababu tulijadili siku zilizopita? Suala siyo kuongea tu bali kuongea nini. Mtu hawezi kujifanya mpambanaji halafu anabaki kuwasifia watu ambao ni zao la ufisadi eti kwa sababu wana vyeo vikubwa. Je hao waasia wangekuwa na vyeo vikubwa angewasema? Hapo ndipo tunaposema huyo siyo mpambanaji bali ni mpambe fulani tu
 
[[ Hapa tunajadili hoja za Mengi na hao nao wakija na hoja zao tutawajadili vile vile. Hawa watu jamii ya akina Mengi ni wapotoshaji tu, umefika wakati wa uchaguzi ambapo ingestahili watu wawashauri wananchi wa kawaida wachague viongozi wazuri wao huanza kuwasifia watu fulani na kudai eti ni viongozi wasafi na waadilifu. Usanii mtupu. Wakati dili la rada linakamilishwa JK alikuwa Waziri wa Fedha, wakati akina CHavda amekula fedha za Benki akishirikiana na Idris Rashid, Kikwete alikuwa waziri, wakati IPTL inaingia JK alikuwa waziri, wakati wanachukua mapesa BoT kwenye akaunti ya EPA kwa kushirikiana na Ballali, ni JK huyo huyo ambaye alisaidiwa ili aingie ikulu, wakati Richmond JK huyo huyo alikuwa Rais aliyeubariki huo mpango. Leo anajitokeza mtu anayejitapa ni kamanda wa kupambana na ufisadi na kuanza kumsifia kwa nini tusimuone msanii??

a. Tatizo ni kuwa hapa hatujadili hoja za Mengi umegeuza ili tumjadili Mengi. Mengi kasema mapapa wa ufisadi nchini ni hao aliowataja kina Rostam, Manji, Patel, na wenzao. Sasa useme kuwa alichosema hakina msingi, kwamba hawa ni wazalendo na watu safi na yakuwa Mengi anawasingizia. Kusema mambo ya Mengi au misimamo ya mengi ya 1995 ni kukwepesha hoja (red herring). Kwa sababu, watu tunabadili misimamo na tunabadili positions na wakati mwingine kutokana na kukomaa zaidi katika masuala fulani tunabadilika hata sisi wenyewe.

Kama Mengi aliipigia kampeni CCM (hata mimi nilifanya hivyo 2005 na kuwa shabiki namba moja wa JK) si ajabu baada yamuda kupita tunajikuta tunabadili mawazo. Kuna watu walikuwa karibu na Bush kwa muda mrefu lakini alipofikia mahali pa kumaliza kipindi chake watu hao walikuwa mbali naye kabisa. Hiyo ni sehemu ya siasa.

b. Je kuna ushahidi gani kuwa JK amejichotea fedha za umma? Kuna kesi ambazo Jk anastahili kuhusishwa nazo na kuna maswlai ambayo anatakiwa kujibu. Kwa yeye kutetewa na Mengi hakumfanyi kuwa ni msafi. Kwa yeye kupambana na ufisadi au kuongoza hizo harakati kwa maoni ya baadhi ya watu haina maana yeye mwenyewe si zao la ufisadi. As long as he is not against us he is for us!

Kikwete akijitokeza na kuwatetea mafisadi basi atakuwa amejiweka upande wao so far pamoja na mapungufu yake mengi na hata kunufaika he has not come against our cause so, an enemy of my enemies is my friend!

c. Hata kama tukiweza kuonesha kuwa JK amenufaika na ufisadi na ya kuwa yeye mwenyewe ni fisadi (kitu ambacho kinawezekana) there is nothing we can do. Hatuwezi kumfungulia mashtaka na hata pale ambapo tunafikiri tunaweza inabidi tufuate mlolongo mkubwa na mashtaka hayo yanaenda katika bunge ambapo kuna process inayoshinda ya kufufua mtu! Hivyo, kusema JK ni fisadi au vipi ili tukubaliane kuwa ni fisadi ni kujiridhisha akili tu na kutuliza vionjo vyetu kwa sababu there is nothing we can not (at least for now) dhidi yake! So why waste our energy?

Kwa hawa wengine tunaweza kuwashughulikia na inapaswa kuwashughulikia sasa kama wakifika huko na kusema JK ni mshirika wetu waache wao waseme na hapo tutambana Jk.. lakini kujaribu kuhamisha culpability kutoka kwa kina Rostam na kujaribu kuwakwepesha makosa yao (ambayo naweza kuyahesabu) ni kujaribu kukwepesha hoja.

Hawa watu watatu peke yao wana maswali lukuki ya kujibu na ingekuwa nchi nyingine wangekuwa wametiwa pingu zamani. Tatizo kubwa ni je JK katika kupewa sifa hizi zote yuko tayari kuona watu hawa na marafiki zake wakisimamishwa kizimbani?
 
Kwa hiyo hata Rostam angekuja kuongea na kulaani ufisadi na wewe ungemsapoti kwa sababu tulijadili siku zilizopita? Suala siyo kuongea tu bali kuongea nini. Mtu hawezi kujifanya mpambanaji halafu anabaki kuwasifia watu ambao ni zao la ufisadi eti kwa sababu wana vyeo vikubwa. Je hao waasia wangekuwa na vyeo vikubwa angewasema? Hapo ndipo tunaposema huyo siyo mpambanaji bali ni mpambe fulani tu

Mheshimiwa its not as clear cut as you think! Mengi is just opening the flood gates, what matters here is that the average tanzanian who had no access to the internet to see what we usualy discuss now knows wats up! Lets be realistic, there is no way in hell rostam anaweza kusimama na kukandia ufisadi like mwakyembe said " he may have the money but not the moral authority to point fingers".
 
kikwete kachanganyikiwa nadhani....maana wasaidizi wake hawamsikilizi..msaidizi muaminifu lazima ufuate imani ya kiongozi..,sasa unapokuwa huna msimamo..au itikadi ..principles ..wasaidizi kila mmoja ana kuwa na msimamo wake..

huwezi kuwa na msimamo wako ..na ukabaki kuwa msaidizi wangu lazima nikutowe......msimamo tofauti na wangu utanishauri sirini..na nikiukubali utaitwa msimamo wangu...uongozi si lelemama!!!

sasa ukiona rais anaaza kuwa na wasaidizi waaminifu nje ya circle halali ya kikatiba ..kina mengi,anna kilango,kimaro..basi ujuwe na hao wasaidizi wapya wana malengo yao...mema au mabaya....!! ndiyo ilivyo....ndio maana wakaweka utaratibu ...sasa rais anaaza kutafuta faraja nje ya cabinet..theres a serious problem ..kama anashindwa kuwaambia asiopenda mienendo yao...nooooo!

PM.. tunachofanya sasa hivi na kinachoendelea ni kuendelea kuchora mpaka kati ya JK na kundi lililomwingiza madarakani. Hao wasaidizi unaowazungumzia ndio genge kubwa la ufujaji wa fedha za walipa kodi; wangejua mwenyewe anawaangalia ili atakapowaangusha watashangaa. Si kwamba hajui.

Hawa wasaidizi tulishawalalamikia tangu suala la Mapanki lilipokuja na sasa tunatambua kuwa hawafanyi kazi yao vizuri na wamekuwa wakimshauri vibaya.
 
PM.. tunachofanya sasa hivi na kinachoendelea ni kuendelea kuchora mpaka kati ya JK na kundi lililomwingiza madarakani. Hao wasaidizi unaowazungumzia ndio genge kubwa la ufujaji wa fedha za walipa kodi; wangejua mwenyewe anawaangalia ili atakapowaangusha watashangaa. Si kwamba hajui.

Hawa wasaidizi tulishawalalamikia tangu suala la Mapanki lilipokuja na sasa tunatambua kuwa hawafanyi kazi yao vizuri na wamekuwa wakimshauri vibaya.


Mwanakijiji kwa nini uchore mipaka kati ya JK na kundi linalomwingiza? Au ndiyo strategy ya Mengi ili mwishowe yeye ndiyo aanze kucall the shots. Kama unakubali kwamba kundi lililomwingiza ni chafu kwa nini yeye awe msafi? Leo hii mwanakijiji unakuja na kusema kwamba JK atofautishwe na kundi lake kwi kwi kwi kwi. Au kwa sababu bosi wako Mengi kamsifia na wewe unaanza kuimba sifa za JK.

Mwanakijiji sikuchagulii nani umpigie kampeni, lakini tambua kuwa ukimpigia kampeni fisadi ukija kuniambia unapambana na ufisadi nitakuuliza hata wewe?? Au unafanya usanii
 
- Unajua wabongo tufike mahali tujifunze kutofautisha ishus, na kwamba kila kitu kina msimu wake, katika huu msimu tulionao sasa hivi Mengi anahitaji support yetu wapenda mabadiliko kwa sababu otherwise unakuwa unam-support Makamba, ambaye hana lolote isipokuwa kuwakilisha kundi la mafisadi.

- At this time and point, kum-support Mengi, ni kubadilisha upepo wa kisiasa kwa taifa na pia kujenga mandate mpya kwa the next president, Mengi na wabunge wapiganaji they need our support now kwa sababu hata Muungwana hawezi kwenda kusimama na wabunge wake walio mafisadi mbele ye wananchi, ninasema hawezi, ndio maana hata huko Busanda wamepigwa marufuku kugusa, hujawahi kumsikia Auntie Sophia akigusa kwenye uchaguzi mdogo, pamoja na kwua Mwenyekiti wa wanawake na huko anayegomeba ni kwa CCM ni mwanamke mwenzake.

- Sikubaliani na some tactics za Mengi, lakini kwenye hili la kupigana na mafisadi ninampa 100% support, na ninasema kwamba we need him now than ever, the fact kwamba Makamba anaweza kwenda CC na kuanza kumlilia Mengi ni ukweli ulio wazi kwamba mafisadi wanamuogopa ndio maana wamemtuma Makamba, kama kuna anyeujua ufisadi wa Mengi kwa taifa, auweke hapa ili tuujue na kuuchambua, in the absence ya political alternative katika taifa letu sasa, Mengi stands tall na anahitaji our support.

Respect.

FMES!
 
there is no way in hell rostam anaweza kusimama na kukandia ufisadi like mwakyembe said " he may have the money but not the moral authority to point fingers".

Rostam mwaka jana kasimama na kuwasema akina Mengi pamoja na Mtikila je hiyo nayo inahitaji moral authority? Mengi naye leo kaongea kamsema Rostam je hiyo nayo inahitaji moral authority gani? Mwakyembe naye si alikuja kwa waandishi na yeye akamsema Rostam wakati yeye mwenyewe anahisa kwenye kampuni ya umeme je alikuwa na moyo authority, Je Mtikila alivyokuja kumsema Rostam wakati amevuta milioni tatu toka kwake je alikuwa na moral authority gani? Ndiyo maana nakwambia issue ni nini kimeongelewa na mtu siyo nani kaongea. Sasa Mengi anamsifia JK ambaye mimi binafsi namwona ni zao la ufisadi sasa kwa nini nisimtilie shaka?
 
Back
Top Bottom