Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Makamba amrushia kombora Mzindakaya
na Bakari Kimwanga
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba, jana amevunja ukimya na kumrushia kombora Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kwela, Dk. Chrisant Mzindakaya, na kusema kuwa kamwe CCM haitaepuka kupata na kutathmini mawazo na michango ya wazee wa chama hicho.
Akizungumza na Tanzania Daima jana katika mahojiano maalumu, alisema sasa uzee wala ujana si sifa ndani ya CCM ila kinachotakiwa ni kupima utendaji kazi na si kuishia kulaumu bila kutoa njia ya nini kifanyike kwa makosa yanayojitokeza ndani ya CCM.
Februari 12 mwaka huu, Dk. Chrisant Mzindakaya, alisema baadhi ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamechoka, hawana upeo na mbinu za kutatua matatizo ya kiuchumi na kijamii.
Alisema ndani ya CCM kuna makundi mawili ya wazee, huku akilitaja kundi la kwanza ni lile ambalo limeombwa kutokana na busara zao na kubarikiwa na Kamati Kuu ya CCM na kundi la pili ni la wazee walioomba kugombea na wanachama wakawachagua katika mikutano ya uchaguzi.
Alisema wakati umefika kwa baadhi ya viongozi kungatuka na kuwaachia wenye mawazo mapya kuongoza.
Kutokana na kauli hiyo, Makamba alisema ili chama hicho kiweze kufanya kazi zake kwa mujibu wa utaratibu ni muhimu wazee wakapewa nafasi ya kutoa mchango wao kwa taifa bila kuwa na ubaguzi wa aina yoyote.
Mimi nishatangaza sitagombea ubunge na itakapofika mwaka 2012, nitakuwa nimeitumikia CCM kwa miaka 30, hata nafasi hii ya ukatibu mkuu niliteuliwa na rais ambaye ni mwenyekiti wa chama, sasa maneno yanatoka wapi jamani?
Mwalimu J.K. Nyerere alisema hakuna shamba linalokosa mbuyu na hapa tunaona wazi umuhimu wa wazee katika kuongoza mambo na hakuna safari iliyo salama kama si busara za wazee, hao wanaowakana wazee hawana jipya ndani ya CCM, mbona CCM imeshinda huku wanaoongoza ni wazee? alisema Makamba.
na Bakari Kimwanga
Akizungumza na Tanzania Daima jana katika mahojiano maalumu, alisema sasa uzee wala ujana si sifa ndani ya CCM ila kinachotakiwa ni kupima utendaji kazi na si kuishia kulaumu bila kutoa njia ya nini kifanyike kwa makosa yanayojitokeza ndani ya CCM.
Februari 12 mwaka huu, Dk. Chrisant Mzindakaya, alisema baadhi ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamechoka, hawana upeo na mbinu za kutatua matatizo ya kiuchumi na kijamii.
Alisema ndani ya CCM kuna makundi mawili ya wazee, huku akilitaja kundi la kwanza ni lile ambalo limeombwa kutokana na busara zao na kubarikiwa na Kamati Kuu ya CCM na kundi la pili ni la wazee walioomba kugombea na wanachama wakawachagua katika mikutano ya uchaguzi.
Alisema wakati umefika kwa baadhi ya viongozi kungatuka na kuwaachia wenye mawazo mapya kuongoza.
Kutokana na kauli hiyo, Makamba alisema ili chama hicho kiweze kufanya kazi zake kwa mujibu wa utaratibu ni muhimu wazee wakapewa nafasi ya kutoa mchango wao kwa taifa bila kuwa na ubaguzi wa aina yoyote.
Mimi nishatangaza sitagombea ubunge na itakapofika mwaka 2012, nitakuwa nimeitumikia CCM kwa miaka 30, hata nafasi hii ya ukatibu mkuu niliteuliwa na rais ambaye ni mwenyekiti wa chama, sasa maneno yanatoka wapi jamani?
Mwalimu J.K. Nyerere alisema hakuna shamba linalokosa mbuyu na hapa tunaona wazi umuhimu wa wazee katika kuongoza mambo na hakuna safari iliyo salama kama si busara za wazee, hao wanaowakana wazee hawana jipya ndani ya CCM, mbona CCM imeshinda huku wanaoongoza ni wazee? alisema Makamba.