"Huyu ndugu yangu Makamba ananishangaza sana. Lowassa anatoa wito kwa kuwa ameona tatizo, lakini yeye anapinga, akijifanya hawezi kukaa meza moja ya majadiliano na CHADEMA akiamini kuwa matumizi ya magari ya maji ya kuwasha ndilo suluhisho…bado watu watapigwa na kuwa sugu wakitoka wanaendelea kutafakari unyanyasaji huo!" alisema.
Alibainisha kuwa matumizi ya nguvu na polisi yataleta usugu kwa wananchi kama ilivyo kwa Wapalestina na Waisraeli ambao mara kwa mara wamekuwa na mapigano yanayosababisha vifo, uharibifu wa mali na wengine kukimbia makazi yao.