Joss
JF-Expert Member
- May 28, 2009
- 765
- 191
Alikuwa anazungumza na wanaccm wa Arusha kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi.
Angalia kwenye nyekundu.....
BAADA ya kimya cha muda mrefu, katibu mkuu wa CCM, Yusuph Makamba ameibuka na kuwataka viongozi wa dini nchini kuacha kuwachagulia waumini wao wagombea kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Kwa muda mrefu tangu kampeni zianze, Makamba amekuwa kimya, akikataa kuzungumzia masuala ya kampeni za chama chake kwa maelezo kuwa yupo mapumzikoni mkoani Tanga.
Lakini jana, Makamba alikuwa na mkutano na wanachama wa CCM kwenye Kata ya Kaloleni mjini hapa jana na kuwambia kuwa katika siku za karibuni baadhi ya viongozi wa dini wamekuwa wakiwataka waumini wao kuchagua wagombea wa fulani jambo ambalo katibu huyo wa CCM alidai kuwa si haki.
"Kuna baadhi ya viongozi wa dini wamekuwa wakitoa maneno yanayoonyesha wanawachagulia waumini wao wagombea... naomba muanze kuwauliza ni wapi katika vitabu vyao vimewaeleza wawalazimishe kuwachagulia viongozi," alisema Makamba.
Katibu huyo, wa CCM bila kuwataja viongozi hao, huku akinukuu maneno ya vitabu vitakatifu vya Biblia na Quran, alisema kila mtu ana haki ya kumchagua kiongozi bora ambaye anamtaka na sio kuchaguliwa.
Kumekuwepo na tuhuma hizo za viongozi wa dini kuwashawishi waumini wao kuwachagua wagombea wanaowataka, lakini hadi sasa hakuna kiongozi wa dini aliyekemewa wala kuonywa kwa kosa la kuwatajia waumini wake jina la mgombea anayemtaka.
Hata hivyo, Makamba alisema viongozi bora ni wawale wanatokana CCM ambayo aliielezea kuwa ni chama chenye rekodi ya kuwasaidia wananchi katika kukabiliana na umasikini, ujenzi wa barabara na kuwawekea huduma muhimu.
"Waulizeni hao akina (mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Willibrod) Slaa na (mgombea urais kwa tiketi ya CUF, Prof Ibrahim) Lipumba je wamewahi kujenga barabara; je wamewahi hata kuwasaidia; lakini Kikwete leo ni sawa na mtu ambaye ametoka vitani. Ana jambo la kujivunia kwa kuwa katika miaka mitano kuna mengi amefanya," alisema Makamba.
Katika mkutano huo, Makamba aliwataka wakazi wa Arusha kujiepusha na siasa za udini na kuwataka kuchagua kiongozi bora bila kujali dini yake wala kabila lake.
"Nina jambo moja muhimu nataka kuwaambia... kuna hili la udini nawaomba muache udini chagueni viongozi bora kama Kikwete na Dk Batilda na madiwani wa CCM kwa kuwa wanawapenda na wataweza kuwasaidia," alisema Makamba.
Makamba katika mkutano huo, pia aliomba wanachama wa CCM wilayani Arusha kuvunja makundi na kumchagua mbunge aliyepitishwa na chama hicho, Batilda Buriani hata kama mwanzoni hakuwa katika kundi lao.
Makamba aliwaonya wanaccm kuwa hatawaeleka kama jimbo la Arusha likipotea hivyo ni wajibu wao kushikamana sasa na kuachana na upinzani ili CCM ishinde kiti cha urais, ubunge na nafasi nyingi za udiwani.
"Najua wapo hapa baadhi yetu wana mashati ya kijani lakini moyoni sio wenzetu, naowaomba kuanzia leo tushirikiane... Batilda apite kwa kuwa ushindi wake ni wetu sote CCM," alisema Makamba.
Angalia kwenye nyekundu.....
BAADA ya kimya cha muda mrefu, katibu mkuu wa CCM, Yusuph Makamba ameibuka na kuwataka viongozi wa dini nchini kuacha kuwachagulia waumini wao wagombea kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Kwa muda mrefu tangu kampeni zianze, Makamba amekuwa kimya, akikataa kuzungumzia masuala ya kampeni za chama chake kwa maelezo kuwa yupo mapumzikoni mkoani Tanga.
Lakini jana, Makamba alikuwa na mkutano na wanachama wa CCM kwenye Kata ya Kaloleni mjini hapa jana na kuwambia kuwa katika siku za karibuni baadhi ya viongozi wa dini wamekuwa wakiwataka waumini wao kuchagua wagombea wa fulani jambo ambalo katibu huyo wa CCM alidai kuwa si haki.
"Kuna baadhi ya viongozi wa dini wamekuwa wakitoa maneno yanayoonyesha wanawachagulia waumini wao wagombea... naomba muanze kuwauliza ni wapi katika vitabu vyao vimewaeleza wawalazimishe kuwachagulia viongozi," alisema Makamba.
Katibu huyo, wa CCM bila kuwataja viongozi hao, huku akinukuu maneno ya vitabu vitakatifu vya Biblia na Quran, alisema kila mtu ana haki ya kumchagua kiongozi bora ambaye anamtaka na sio kuchaguliwa.
Kumekuwepo na tuhuma hizo za viongozi wa dini kuwashawishi waumini wao kuwachagua wagombea wanaowataka, lakini hadi sasa hakuna kiongozi wa dini aliyekemewa wala kuonywa kwa kosa la kuwatajia waumini wake jina la mgombea anayemtaka.
Hata hivyo, Makamba alisema viongozi bora ni wawale wanatokana CCM ambayo aliielezea kuwa ni chama chenye rekodi ya kuwasaidia wananchi katika kukabiliana na umasikini, ujenzi wa barabara na kuwawekea huduma muhimu.
"Waulizeni hao akina (mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Willibrod) Slaa na (mgombea urais kwa tiketi ya CUF, Prof Ibrahim) Lipumba je wamewahi kujenga barabara; je wamewahi hata kuwasaidia; lakini Kikwete leo ni sawa na mtu ambaye ametoka vitani. Ana jambo la kujivunia kwa kuwa katika miaka mitano kuna mengi amefanya," alisema Makamba.
Katika mkutano huo, Makamba aliwataka wakazi wa Arusha kujiepusha na siasa za udini na kuwataka kuchagua kiongozi bora bila kujali dini yake wala kabila lake.
"Nina jambo moja muhimu nataka kuwaambia... kuna hili la udini nawaomba muache udini chagueni viongozi bora kama Kikwete na Dk Batilda na madiwani wa CCM kwa kuwa wanawapenda na wataweza kuwasaidia," alisema Makamba.
Makamba katika mkutano huo, pia aliomba wanachama wa CCM wilayani Arusha kuvunja makundi na kumchagua mbunge aliyepitishwa na chama hicho, Batilda Buriani hata kama mwanzoni hakuwa katika kundi lao.
Makamba aliwaonya wanaccm kuwa hatawaeleka kama jimbo la Arusha likipotea hivyo ni wajibu wao kushikamana sasa na kuachana na upinzani ili CCM ishinde kiti cha urais, ubunge na nafasi nyingi za udiwani.
"Najua wapo hapa baadhi yetu wana mashati ya kijani lakini moyoni sio wenzetu, naowaomba kuanzia leo tushirikiane... Batilda apite kwa kuwa ushindi wake ni wetu sote CCM," alisema Makamba.