Elections 2010 Makamba akiri Dr Slaa ni tishio kwa Kikwete na CCM

Huyo mzee hana strategy zozote, mmesahau wakati wa uchaguzi mdogo tarime? Aligaragazwa kisiasa.
 
Dk. Slaa ni moto wa mabua ambao huzimika baada ya dakika tano kama alivyozimika Mrema. Mtu ambaye tunamuogopa…tunayeweza kusema kuwa ni tishio ni Lipumba, maana yeye alikuwa wa pili katika uchaguzi uliopita,” alisema Makamba.

Profesa wa Pumba alikuwa tishio mwaka ulke, si mwaka huu ambako wengi wamekikimbia chama chake kwa sababu ya kauli zake za kutetea ufisadi alizotoa mwaka jana -- kuhusu mafisadi papa na pia kutete ununuzi wa mitambo chakavu ya Dowans. Hapo ndipo ilikuwa mwisho wa CUF -- kujitambulishja kwake na mafisadi. kama nasema uongo chunguzeni uswahiba mkubwa uliopo kati ya Ismail Jussa na Rostam Aziz. Uswahiba huu wa kifisadi ndiyo uliyomkimbiza Lwakatare kutoka CUF -- na kuna siku atakuja kuzungumzia kwa undani suala hilo.

Kwa hivyo kwa Makamba kumtetea Lipumba hivi sasa ni sababu wameshamteka -- amekuwa anawatetea katika ufisadi wao -- kitu ambacho Dr Slaa hawezi kamwe kukifanya. Malaria Sugu, inapaswa ufahamu kwamba CCM haiwezi kumtetea kiongozi wa upinzani hivi hivi tu, pasipo kufaidika na
ye.
 
Makamba siyo mtu wa kumnukuu kwa vile amejaa wivu na chuki,yeye tangu azaliwe hajawahi kupata nafasi yoyote kwa kuchaguliwa na watu , yeye siku zote amekuwa akipata nafasi za kuteuliwa na wakubwa kwa vile ni bingwa wa kuwalamba miguu wakubwa, hivyo akiona mtu anayependwa na watu roho inamuuma sana. Hivi kumlinganisha Makamba na Dr Slaa ni sawa na kulinganisha panya buku na tembo,YM yuko chini saaaana, ndiyo maana matamshi yake ni ya kijiweni tu.

Ningependa Dr Slaa mwenyewe ndiyo angemjibu Makamba namna hii. Lakini naamini kabisa kama kuna mdahalo kati ya Dr Slaa na YM, basi YM atapata tumbo la kuharisha kabla ya kuanza. YM ni mwanasiasa uchwara tu, anakweza kwa kujikombakomba tu kwa walio juu yake -- hana lolote!!!!!!!!!!!
 
Huyo mzee hana strategy zozote, mmesahau wakati wa uchaguzi mdogo tarime? Aligaragazwa kisiasa.

Ha ha -- umenikumbusha ya Tarime!! YM aliukimbia mji usiku na hakusikika hadi miezi miwili baadaye! Anachezea Waswahili wacheza bao wa kule Bumbuli, siyo wanaume wa Tarime!!!
 
Ningependa Dr Slaa mwenyewe ndiyo angemjibu Makamba namna hii. Lakini naamini kabisa kama kuna mdahalo kati ya Dr Slaa na YM, basi YM atapata tumbo la kuharisha kabla ya kuanza. YM ni mwanasiasa uchwara tu, anakweza kwa kujikombakomba tu kwa walio juu yake -- hana lolote!!!!!!!!!!!

Kazi yake kubwa ni kucheza ngoma ya TOT katika majukwaa ya CCM, kabla ya wanasiasa kuingia.
 
Dk. Slaa ni moto wa mabua ambao huzimika baada ya dakika tano kama alivyozimika Mrema. Mtu ambaye tunamuogopa…tunayeweza kusema kuwa ni tishio ni Lipumba, maana yeye alikuwa wa pili katika uchaguzi uliopita,” alisema Makamba.
Makamba kazungumza haya makusudi akijua anakianzisha baina ya CUF na Chadema kwa kuwaweka ulingoni Dr.Slaa na Lipumba. This is stage one ya CCM siku zote ni kugombanisha Upinzani..
 
Mimi naona huyu juha kasha mu endorse Lipumba, unless anamuhofia Dr. Slaa na anajaribu kui dilute kura ya upinzani kwa kuigawa kati ya Dr. Slaa na Dr. Lipumba (kitu ambacho huyu mtu siwezi kumfikiria kufikiria, kwa jinsi alivyo off the cuff, or could it be that Makamba is more calculating than the buffoon he is letting his image to portray ?)

Kwa hiyo unless anataka kuigawanya kura ya upinzani, hii ni bonge la endorsement kwa Lipumba. Katika nchi zinazotumia matangazo sana naweza kuona Lipumba akitumia kauli hii ya Makamba katika kampeni yake. "Hata wapinzani wetu wanakubali kwamba wanatuogopa".

The more I think about it, the more that theory of dividing the opposition makes sense. Unless Makamba is so nutty as to give generous endorsement freely to the opposition, why would he want to endorse Lipumba ?
 
Makamba is the bomb thrower for CCM. He is their attack dog....

And I kinda like it though...the opposition also need to have their own attack dog. You can't let CCM's apparatchiks swift boat you like that. You have to hit back and hit back twice as hard

Politics is rough and tumble.
 
MAKAMBA = CHEMICAL ALI a.k.a vuvuzela

wirq13.jpeg


Mkuu hii ibadilishe iwe "Comical" ndiyo itamfiti hasa; amekalia kuongea tu, mwisho wa siku chali. Makamba anajua kabisa kuwa wana uwezo wa kujitangaza wameshinda kwani Tume ya uchaguzi ni yote inaongozwa na makada wa CCM. Kinachowaumiza vichwa hasa ni pale Dr. Slaa atakapokuwa na wafuasi wengi kama ilivyokuwa kwa "Raila Odinga" hilo ndilo linalowatisha na wanataka kuhakikisha wanamfunga Dr. Slaa repelant ya wafuasi kwa kumuita kila neno baya kuanzia kwenye dini mpaka muziki.

Maana wanajua kabisa kuwa nguvu ya "mwanasiasa ni wafuasi" na kama wafuasi wakiwa wengi zaidi inakuwa ngumu kutekeleza wizi wa mchana wa kura, vinginevyo ujiandae for the worse.
 
"Dk. Slaa si tishio kwa CCM ila ni tishio kwa mtu binafsi…hawezi kuwa tishio kwa chama. Nani alikuwa maarufu kama Mrema. "Santuri mpya ikitoka itachezwa katika nyumba mbalimbali lakini baada ya muda watarudia ya zamani," alisema Makamba.

Dk. Slaa ni moto wa mabua ambao huzimika baada ya dakika tano kama alivyozimika Mrema. Mtu ambaye tunamuogopa…tunayeweza kusema kuwa ni tishio ni Lipumba, maana yeye alikuwa wa pili katika uchaguzi uliopita," alisema Makamba.

Wadadisi wa mambo wanaelezea hatua ya Makamba kulazimika kumuweka Lipumba juu ya Dk. Slaa, hasa wakati huu ambapo mgombea huyo wa CHADEMA anaonyesha dalili za kuungwa mkono, ni jitihada tu za chama hicho kujaribu kumshambulia yule wanayemhofia kuwa na nguvu zaidi katika kipindi hiki.

Hongera sana Makamba, kwenye ukweli uwongo hujitenga. Watanzania wekeni kumbukumbu ya maneno ya makamba. Dr Slaa na Chadema yatumieni kwa faida. Makamba amekiri kwa kinywa chake kwamba Dr. Slaa ni tishio kwa Kikwete. Dr Slaa yuko juu kuliko Kikwete, ni kama anga ilivyo juu kuliko nchi kavu. Makamba alishawahi kusema kuwa Kikwete ni maarufu kuliko CCM. Kwa kuwa Kikwete ni maarufu kuliko CCM, Makamba anakiri kuwa Dr. Slaa yupo juu kuliko Kikwete na CCM. Kwa hiyo Dr. Slaa ni tishio kwa Kikwete na CCM yote kwa sababu Kikwete ni maarufu kuliko CCM.
 
Huyu mzee ni kama kasuku tu ye ni kuropoka tu hata kama haelewi maana ya asikiacho. Mwacheni aende bumburi akagombee kwa ufisadi!
 
Kwa kukiri hadharani kupia TBC kuwa Dr Slaa ni tishio kwa Kikwete na siyo CCM, Makamba anakiri kuwa Dr. Slaa ni tishio kwa Kikwete na CCM. Hii ni kwa sababu Makamba akinukuu utafiti wa REDET aliwahi kusema kuwa Kikwete ni maarufu kuliko CCM. Ni wazi kuwa Dr Slaa ni tishio kwa Kikwete na CCM kwa sababu Dr. Slaa ameongoza nchi hii kama rais akiwa Bungeni. Dr. Slaa ndiye yeye pekee aliyeona mapungufu kwenye sheria ya uchaguzi ambayo Kikwete hakuona wala CCM hawakuona na akaisaini sheria kwa mbwembwe. Umesema vema Makamba, Dr. Slaa ni tishio kwa Kikwete na CCM, Dr Slaa anaipenda nchi hii kwa dhati. Watanzania tujiandikishe kupiga kura, rais wetu ni Dr. Slaa, CCM wamekiri wenyewe.
 
Ni kweli kuwa Dr. Slaa ni tishio, lakini mbona hii habari inaonekana kama haijakamilika? Haisemi Makamba alikiri hivyo lini, wapi na ilikuwaje hadi akakiri. Hebu tupe habari kamili.
 
Back
Top Bottom