Elections 2010 Makamba akiri Dr Slaa ni tishio kwa Kikwete na CCM

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
301
"Dk. Slaa si tishio kwa CCM ila ni tishio kwa mtu binafsi…hawezi kuwa tishio kwa chama. Nani alikuwa maarufu kama Mrema. "Santuri mpya ikitoka itachezwa katika nyumba mbalimbali lakini baada ya muda watarudia ya zamani," alisema Makamba.

Dk. Slaa ni moto wa mabua ambao huzimika baada ya dakika tano kama alivyozimika Mrema. Mtu ambaye tunamuogopa…tunayeweza kusema kuwa ni tishio ni Lipumba, maana yeye alikuwa wa pili katika uchaguzi uliopita," alisema Makamba.

Wadadisi wa mambo wanaelezea hatua ya Makamba kulazimika kumuweka Lipumba juu ya Dk. Slaa, hasa wakati huu ambapo mgombea huyo wa CHADEMA anaonyesha dalili za kuungwa mkono, ni jitihada tu za chama hicho kujaribu kumshambulia yule wanayemhofia kuwa na nguvu zaidi katika kipindi hiki.
 
Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba amenukuliwa na vyombo vya habari kwamba Mgombea urais wa Chadema, Dr Wilbroad Slaa ni kama santuri (yaani record ya muziki) mpya tu ambayo so muda itakuja kuchakaa.

Kiongozi huyu msanii na propagandist mkubwa wa chama tawala ambaye kwake kusema yaliyo ya kweli ni mwiko anapaswa atambue kwamba ni bora azungumzie santuri ambayo tayari imeshachakaa – na siyo kujifanya mtabiri wa santuri itakayochakaa. Hataki kutambua kwamba santuri ambayo tayari imeshachakaa ni chama chake -- CCM – baada ya kukaa karibu miaka 50 madarakani.

Halafu kuchakaa kwake ni kuibaya sana kwani kumezuka unyan’gau wa hali ya juu ndani ya viongozi wake – kama vile tunavyoshuhudia hivi sasa wanavyogombania milo – hakuna tofauti na alivyokuwa akisema Mwl Nyerere kwamba ubepari ni unyama tu.

Wachunguzi wa mambo wanasema polepole CCM inajimaliza na huenda katika uchaguzi ujao (2015) wanaowania uongozi katika CCM wakatoleana bastola katika vikao au/na kujifyatulia risasi. Dalili zinaonekana kwani viongozi wakuu wa chama chenyewe hawawezi kujirekebisha au hata kujikemea kwa sababu kila mmoja wao yumo katika dimbwi la rushwa.

Hivi sasa wanatumia Takukuru kama onyesho kwa wananchi kwamba wanajirekebisha – mpango ambao ni kiini macho kwani taasisi hiyo imeingiliwa kisiasa na mtandao mmoja wa chama hicho.

Na kwa upande wake Takukuru imejikuta haina uhuru kamili katika mpango huu – na mfano ni namna afisa wake mmoja wa wa mkoa wa Kilimanjaro alivyoteremshwa cheo na kuhamishwa kwa sababu tu alimtia mbaroni DC mmoja kwa tuhuma za kugawa rushwa. Yale yale ya kulindana!

Kwa kifupi Makamba anapaswa kuangalia uchakavu mkubwa wa chama chake kabla ya kusemea chama kingine ambacho wananchi wanakiona kama ni mkombozi mkubwa kwao kutokana na machafu yanayoendelea katika CCM.


 
Jana niliona TBC walimpa airtime ya kutosha kumwaga upupu wake, kama hawamhofii kelele za nini?
 
Dk. Slaa ni moto wa mabua ambao huzimika baada ya dakika tano kama alivyozimika Mrema. Mtu ambaye tunamuogopa…tunayeweza kusema kuwa ni tishio ni Lipumba, maana yeye alikuwa wa pili katika uchaguzi uliopita,” alisema Makamba.

Chakujiuliza ni kama ameshaweza kufikiria athari zinazoweza kuletwa na moto wa mabua, shambani au kwenye makazi ya watu. Lakini kama walivyo wabinafsi wengi, huchelewi kukuta anafikiria mabua ya kwenye bustani yake pekee na kusahau kwamba moto huo huweza kuruka shamba hadi shamba, kitalo hadi kitalo na hata kufikia sehemu zenye mazao yaliyostawi na kuyateketeza pia!!
 
Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba amenukuliwa na vyombo vya habari kwamba Mgombea urais wa Chadema, Dr Wilbroad Slaa ni kama santuri (yaani record ya muziki) mpya tu ambayo so muda itakuja kuchakaa.

Kiongozi huyu msanii na propagandist mkubwa wa chama tawala ambaye kwake kusema yaliyo ya kweli ni mwiko anapaswa atambue kwamba ni bora azungumzie santuri ambayo tayari imeshachakaa – na siyo kujifanya mtabiri wa santuri itakayochakaa. Hataki kutambua kwamba santuri ambayo tayari imeshachakaa ni chama chake -- CCM – baada ya kukaa karibu miaka 50 madarakani.

Halafu kuchakaa kwake ni kuibaya sana kwani kumezuka unyan'gau wa hali ya juu ndani ya viongozi wake – kama vile tunavyoshuhudia hivi sasa wanavyogombania milo – hakuna tofauti na alivyokuwa akisema Mwl Nyerere kwamba ubepari ni unyama tu.

Wachunguzi wa mambo wanasema polepole CCM inajimaliza na huenda katika uchaguzi ujao (2015) wanaowania uongozi katika CCM wakatoleana bastola katika vikao au/na kujifyatulia risasi. Dalili zinaonekana kwani viongozi wakuu wa chama chenyewe hawawezi kujirekebisha au hata kujikemea kwa sababu kila mmoja wao yumo katika dimbwi la rushwa.

Hivi sasa wanatumia Takukuru kama onyesho kwa wananchi kwamba wanajirekebisha – mpango ambao ni kiini macho kwani taasisi hiyo imeingiliwa kisiasa na mtandao mmoja wa chama hicho.

Na kwa upande wake Takukuru imejikuta haina uhuru kamili katika mpango huu – na mfano ni namna afisa wake mmoja wa wa mkoa wa Kilimanjaro alivyoteremshwa cheo na kuhamishwa kwa sababu tu alimtia mbaroni DC mmoja kwa tuhuma za kugawa rushwa. Yale yale ya kulindana!

Kwa kifupi Makamba anapaswa kuangalia uchakavu mkubwa wa chama chake kabla ya kusemea chama kingine ambacho wananchi wanakiona kama ni mkombozi mkubwa kwao kutokana na machafu yanayoendelea katika CCM.



CCM sasa inapumua kwa nguvu ya vyombo vya dola tu -- pasipo hivyo ni kwishnei. Itafika mahala hata hivyo vyombo vya dola vitashindwa kukisanifu chama hicho. Mfano wa huyo DC ni onyesho tosha la kushindwa kwa Takukuru kuisanifu CCM.
 
CCM sasa inapumua kwa nguvu ya vyombo vya dola tu -- pasipo hivyo ni kwishnei.
Umenifurahisha sana CCM ilivyo sasa ni sawa na mtu nayepumua kwa msaada wa mashine maalum ya oxygen ikiondolewa tu hatunaye.

Kama ulivyosema CCM bila vyombo vya dola hakuna kitu hawana cha kuwaambia wananchi uongo wote wamemaliza.
 
CCM sasa inapumua kwa nguvu ya vyombo vya dola tu -- pasipo hivyo ni kwishnei.
Umenifurahisha sana CCM ilivyo sasa ni sawa na mtu nayepumua kwa msaada wa mashine maalum ya oxygen ikiondolewa tu hatunaye.

Kama ulivyosema CCM bila vyombo vya dola hakuna kitu hawana cha kuwaambia wananchi uongo wote wamemaliza.
 
"Dk. Slaa si tishio kwa CCM ila ni tishio kwa mtu binafsi…," alisema Makamba.
Huyo mtu binafsi anayetishiwa na Slaa ni nani?
 
Dk. Slaa ni moto wa mabua ambao huzimika baada ya dakika tano kama alivyozimika Mrema. Mtu ambaye tunamuogopa…tunayeweza kusema kuwa ni tishio ni Lipumba, maana yeye alikuwa wa pili katika uchaguzi uliopita," alisema Makamba.

No wonder MS,

Tunajua unavyokonda kama mnazi kwa mapenzi yako kwa JKM na CCM.
 
..Wanainama Wanainuka Wanaona Haya Haoooooooooo..!!
Kivumbi baada ya Oktoba 31...
 
Dk. Slaa ni moto wa mabua ambao huzimika baada ya dakika tano kama alivyozimika Mrema. Mtu ambaye tunamuogopa…tunayeweza kusema kuwa ni tishio ni Lipumba, maana yeye alikuwa wa pili katika uchaguzi uliopita," alisema Makamba.

Always " MIX WITH YOURS "
 
Kalinganisha vema kabisa...Moto wa mabua ni very efficient....haraka na kazi kubwa kwa mda mdogo...ndivyo JK atakvyong'olewa haraka na kwa uifanisi mkubwa....
Hivi Makamba na akili kweli? Anlinganisha Mrema na Dr. Slaa! Hivi kweli hawa IQ zao zinaweza linganishwa ? Mrema ilikuwa misifa na njaa iliyomtuma lakini Dr. Slaa yy ni uzalendo na mapenzi mema kwa nchi ndio vinamsukuma.
 
Dk. Slaa ni moto wa mabua ambao huzimika baada ya dakika tano kama alivyozimika Mrema. Mtu ambaye tunamuogopa…tunayeweza kusema kuwa ni tishio ni Lipumba, maana yeye alikuwa wa pili katika uchaguzi uliopita," alisema Makamba.

Bora moto wa mabua unaoivisha chakula kuliko ule wa nini sijui unaounguza chakula. Moto ni moto tu ilimradi kuna fuel kiasi gani, yaani, mabua - Dr. Slaa ni sawa na mabua millions na JK ni fungu moja la mkaa!!!!! Lipumba ni moto wa pumba - unafaa kuchomea viazi tu!!
 
Dk. Slaa ni moto wa mabua ambao huzimika baada ya dakika tano kama alivyozimika Mrema. Mtu ambaye tunamuogopa…tunayeweza kusema kuwa ni tishio ni Lipumba, maana yeye alikuwa wa pili katika uchaguzi uliopita,” alisema Makamba.

Wananchi wa bumbuli kama Dr. Slaa ni moto wa mabua basi kwa mantiki hiyo januari makamba ni moto wa karatasi, kwani januari hajawahi kuwa hata wa tatu
 
Kalinganisha vema kabisa...Moto wa mabua ni very efficient....haraka na kazi kubwa kwa mda mdogo...ndivyo JK atakvyong'olewa haraka na kwa uifanisi mkubwa....
Hivi Makamba na akili kweli? Anlinganisha Mrema na Dr. Slaa! Hivi kweli hawa IQ zao zinaweza linganishwa ? Mrema ilikuwa misifa na njaa iliyomtuma lakini Dr. Slaa yy ni uzalendo na mapenzi mema kwa nchi ndio vinamsukuma.

Kwani Makamba ana Elimu gani, usije kuta ni mwalimu wa UPE aliyekimbilia ukamisaa wa jeshi na kuambulia uluteni.
 
Makamba siyo mtu wa kumnukuu kwa vile amejaa wivu na chuki,yeye tangu azaliwe hajawahi kupata nafasi yoyote kwa kuchaguliwa na watu , yeye siku zote amekuwa akipata nafasi za kuteuliwa na wakubwa kwa vile ni bingwa wa kuwalamba miguu wakubwa, hivyo akiona mtu anayependwa na watu roho inamuuma sana. Hivi kumlinganisha Makamba na Dr Slaa ni sawa na kulinganisha panya buku na tembo,YM yuko chini saaaana, ndiyo maana matamshi yake ni ya kijiweni tu.
 
Back
Top Bottom