democratic
JF-Expert Member
- Nov 21, 2011
- 1,642
- 295
Yule kibabu aliyepata kuwa katibu mkuu wa CCM Luten Yusuf Makamba ameibuka baada ya kimya cha mda mrefu na kuwaasa watanzania waache kufikiri kwamba wanaishi peponi kwa kulalamika kila siku kuwa maisha ni magumu na badala yake wafanye kazi kwa bidii kwani hata huko peponi nako kuna kazi.
Vilevile amewataka waache kumlalamikia Rais J.M.Kikwete kwamba kashindwa kuyafanya maisha yao kuwa bora,kwani hilo si jukumu la rais Kikwete bali ni jukumu la kila mwananchi kunyanyua maisha yake bila kuitegemea serikali au Rais J.M.Kikwete.Alipoulizwa ni kwa nini wakati wa kampeni rais Kikwete alitoa ahadi ya maisha bora kwa kila mtanzania wakati anafahamu kuwa huo sio wajibu wake.
Makamba alidai kuwa siasa ni mchezo na kila mchezo una mbinu na hiyo ilikuwa mbinu ya rais kikwete na chama chake ili aweze kuchaguliwa kwani hata ahadi alizokuwa anatoa Dk.Slaa ya mfuko wa cement kuwa 5000/=kwa mfuko haiwezekani bali ni mbinu ya mchezo wa siasa.
SOURCE;Gazeti la Jambo Leo ukurasa wa 4.
My take; Mzee umri unamtupa mkono vibaya mno kama kweli haamini kama kazi kubwa aliyonayo rais wa nchi ni kuboresha hali ya maisha ya watu wake.
Vilevile amewataka waache kumlalamikia Rais J.M.Kikwete kwamba kashindwa kuyafanya maisha yao kuwa bora,kwani hilo si jukumu la rais Kikwete bali ni jukumu la kila mwananchi kunyanyua maisha yake bila kuitegemea serikali au Rais J.M.Kikwete.Alipoulizwa ni kwa nini wakati wa kampeni rais Kikwete alitoa ahadi ya maisha bora kwa kila mtanzania wakati anafahamu kuwa huo sio wajibu wake.
Makamba alidai kuwa siasa ni mchezo na kila mchezo una mbinu na hiyo ilikuwa mbinu ya rais kikwete na chama chake ili aweze kuchaguliwa kwani hata ahadi alizokuwa anatoa Dk.Slaa ya mfuko wa cement kuwa 5000/=kwa mfuko haiwezekani bali ni mbinu ya mchezo wa siasa.
SOURCE;Gazeti la Jambo Leo ukurasa wa 4.
My take; Mzee umri unamtupa mkono vibaya mno kama kweli haamini kama kazi kubwa aliyonayo rais wa nchi ni kuboresha hali ya maisha ya watu wake.