BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,009
Makamba afiwa na mtoto
Mwandishi Wetu
Daily News; Sunday,October 26, 2008 @00:03
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yussuf Makamba, amefiwa na mtoto wake wa kiume, Kimweri Yussuf Makamba. Taarifa ya Ofisi ya Makao Makuu ya CCM Dodoma jana kwa vyombo vya habari, ilieleza kuwa kutokana na msiba huo, Makamba aliondoka Dodoma jana mchana kwenda kijijini Mahezangulu wilayani Lushoto Mkoa wa Tanga kwa ajili ya taratibu za maziko.
Kwa mujibu wa maelezo ya Mheshimiwa Makamba, mtoto wake huyo amefariki ghafla jana asubuhi huko kijijini kwake Mahezangulu Lushoto mkoani Tanga, ilisema taarifa ya CCM. Kuhusu mazishi, taarifa hiyo ilisema yanatarajiwa kufanyika leo alasiri Bumbuli, Tamota, Lushoto.
Mwandishi Wetu
Daily News; Sunday,October 26, 2008 @00:03
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yussuf Makamba, amefiwa na mtoto wake wa kiume, Kimweri Yussuf Makamba. Taarifa ya Ofisi ya Makao Makuu ya CCM Dodoma jana kwa vyombo vya habari, ilieleza kuwa kutokana na msiba huo, Makamba aliondoka Dodoma jana mchana kwenda kijijini Mahezangulu wilayani Lushoto Mkoa wa Tanga kwa ajili ya taratibu za maziko.
Kwa mujibu wa maelezo ya Mheshimiwa Makamba, mtoto wake huyo amefariki ghafla jana asubuhi huko kijijini kwake Mahezangulu Lushoto mkoani Tanga, ilisema taarifa ya CCM. Kuhusu mazishi, taarifa hiyo ilisema yanatarajiwa kufanyika leo alasiri Bumbuli, Tamota, Lushoto.