OMUSILANGA
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 384
- 227
Ndiyo wakuu! Leo hii mji wa geita na viunga vyake umezizima kwa mkutano mkubwa ulio ongozwa na Mb Wenje wa jimbo la Nyamagana, kamanda Mawazo,diwani wa zamani wa kata ya Sombetini-Arusha alie hamia cdm ktk harakati za Vua gamba,vaa gwanda na Kamanda Rogerz, katibu wa cdm wilaya ya geita. Katika mkutano huo ambao ki msingi ulikuwa ni uzinduzi rasmi wa M4C Mkoani geita ,jumla ya wanachama wapatao 60 wamejiunga na cdm. Katika kutimilika kwa kauli ya "mjinga akijitambua ,mwerevu upo matatani "wananchi wengi wanaume kwa wanawake, wazee kwa vijana wameitikia ujumbe wa M4C ambapo hili limethibitishwa na msafara mrefu wa baiskeli,pikipiki na magari ulio kuwa unaongozwa na Kamanda Mawazo kuelekea kwenye uwanja wa mkutano. Mbali na kutoa ujumbe wa M4C, Mbunge kivuli wa jimbo la geita, Kamanda Rogerz ametoa matamko mazito sana kwa mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa wa geita dhidi ya shughuli zao za ukada wa ccm ambazo zimekuwa hazina tija kwa wananchi wa geita na taifa kwa ujumla. Baada ya mkutano huo Kamanda Rogerz ameitwa polisi na OCD geita. Mpaka sasa hivi hatujui kama atawekwa selo ama ata achiwa. Zaidi tutazidi kujuzana yatakayo jili. Naomba kuwasilisha.