Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Hapa nazungumzia zile ndoa zenye vurugu, maana naona Wa-Beijing wanataka kunishukia kama Mwewe awindapo vifaranga.
Kwa wale wanawake wanaoishi kwenye zile ndoa zenye vurugu zisizoisha, ambapo tendo la ndoa halifanyiki au hufanyika kwa nadra sana, na kwa njia ya ukimaliza funika, msidhani uwepo wa ndoa hiyo kama itaendelea kuwepo, unatokana na kuvumiliana kama mlivyoaminishwa na jamii……….. Maana kuna ndoa zenye vurugu kweli kweli, lakini wahusika wanashindwa kuivunja ndoa hiyo kutokana na sababu mbalimbali, kama sio watoto, basi Dini itakuwa ni sababu kubwa au kukomoana, kitu ambacho kwangu mimi naona ni ujinga tu.
Kwa wanaume wengi wanaoishi kwenye ndoa za aina hiyo, humalizia ashiki zao kwa Makahaba! Kwa kumalizia ashiki zao huko huamini kabisa kwamba itakuwa ngumu kufumaniwa na`wenzi wao, kwa sababu biashara ya ukahaba ni ya nipe ni nikupe na hakuna kujuana.
Kama wewe unadhani unamkomoa mumeo, basi mwenzio anakucheka kwa kijino pembe, kwani ashamaliza hamu yake huko atokako, anajua akifika nyumbani anajilalia zake.
Hebu fikiria, hivi kama makahaba wasingekuwepo, ndoa nyingi zilizo na vurugu zingekalika?……….. Mimi naamini zisingekalika na hata kuuana kungeongezeka. Nyie wenyewe ni mashahidi wa mauaji mengi yanayotokea huko vijijini na sababu kubwa inayotajwa ni ya wanandoa kunyimana unyumba. Na kutokana na ukosefu wa makahaba huko vijijini ukilinganisha na mijini, ndio sababu hali hiyo hutokea…………….
Kwa wale wanawake wanaoishi kwenye zile ndoa zenye vurugu zisizoisha, ambapo tendo la ndoa halifanyiki au hufanyika kwa nadra sana, na kwa njia ya ukimaliza funika, msidhani uwepo wa ndoa hiyo kama itaendelea kuwepo, unatokana na kuvumiliana kama mlivyoaminishwa na jamii……….. Maana kuna ndoa zenye vurugu kweli kweli, lakini wahusika wanashindwa kuivunja ndoa hiyo kutokana na sababu mbalimbali, kama sio watoto, basi Dini itakuwa ni sababu kubwa au kukomoana, kitu ambacho kwangu mimi naona ni ujinga tu.
Kwa wanaume wengi wanaoishi kwenye ndoa za aina hiyo, humalizia ashiki zao kwa Makahaba! Kwa kumalizia ashiki zao huko huamini kabisa kwamba itakuwa ngumu kufumaniwa na`wenzi wao, kwa sababu biashara ya ukahaba ni ya nipe ni nikupe na hakuna kujuana.
Kama wewe unadhani unamkomoa mumeo, basi mwenzio anakucheka kwa kijino pembe, kwani ashamaliza hamu yake huko atokako, anajua akifika nyumbani anajilalia zake.
Hebu fikiria, hivi kama makahaba wasingekuwepo, ndoa nyingi zilizo na vurugu zingekalika?……….. Mimi naamini zisingekalika na hata kuuana kungeongezeka. Nyie wenyewe ni mashahidi wa mauaji mengi yanayotokea huko vijijini na sababu kubwa inayotajwa ni ya wanandoa kunyimana unyumba. Na kutokana na ukosefu wa makahaba huko vijijini ukilinganisha na mijini, ndio sababu hali hiyo hutokea…………….