Majumba ya sinema: kumbukumbu iliyopotea

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Majumba ya sinema: kumbukumbu iliyopotea Send to a friend
Thursday, 12 January 2012 12:53


Na Charles Kayoka
Mwananchi

Naanza kwa kumshukuru msomaji mmoja aliyenidokeza kuwa kuna mrembo mmoja ambaye bado anaishi jijini Dar es salaam, na alikuwa Miss Chagaland kabla ya uhuru. Na kuwa Wachaga walianza kufanya mashindano hayo mapema kabisa. Ninaahidi wasomaji kuwa panapo majaliwa nitamtafuta mama huyu, atuonjeshe historia kidogo. Leo tunazungumzia sinema.

Asubuhi na mapema siku moja wiki iliyopita nilikuwa nawahi miadi eneo la mjini kati hapa Dar-es-Salaam. Nikipita mtaa wa Nkrumah, macho yangu yalielekea juu, kuangalia jengo nililokuwa nikipenda kwenda kupata chai wakati fulani huko nyuma, Continental Hotel. Ghafla macho yangu yakakutana na kitu ambacho kilikuwa kimetoweka katika kumbukumbu yangu. Nacho ni neno NEW CHOX. Kibao kilichofubaa kwa rangi baada ya kutelekezwa miaka dahari kwani umuhimu wa jengo hilo kwa sasa haupo tena, nani anakwenda sinema siku hizi.
Watu wa Dar es salaam ukiwaona wakiingia New World Cinema pale Mwenge au majumba ya Mlimani City, wanaweza kudhani kuwa huu ni utamaduni mpya sana. Kabla na baada ya Uhuru kwenda Sinema ilikuwa ni jambo la kawaida na moja kitu kinachoweza kukuletea mapenzi na heshima kubwa kwa familia yako, rafiki au mpenzi wako, kwa wakati ule.
New Chox, itakumbukwa kwa filamu zake za kizungu, wakati huo nikiwa bado mdogo, kwenda kuona filamu ilikuwa ni jambo adhimu sana. Na siku mzazi wako akikuambia mnakwenda sinema ni sawa kuwa umahidiwa ufalme. Utaona siku haifiki, na wakati unachelewa. Kwa vijana waliozaliwa miaka ya 1980 hasa 1990 neno Jumba la Sinema, ni kama ruya. Lakini Tanzania yote ilikuwa na majumba ya sinema, ambako kila siku jioni na wikiendi watu walikwenda huko kuburudika. New Chox hapa Dar-es-Salaam ilikuwa ni moja ya majengo ya sinema.
Mtaa wa Jamhuri ulikuwa na majengo mawili ya sinema, Odeon, ambako sasa kuna DTV/Channel Ten. Avalon, ambako watu wa GNLD wamekuwa wakifanyia mikutano yao na baadaye watu wa madhehebu ya kilokole kufanyia ibada zao. Jengo hili linaangaliana na uwanja mkubwa yanakoegeshwa magari na ofisi za zamani ya Uhamiaji. Kulikuwa na jengo kubwa zaidi la sinema kule Msasani, likiitwa Drive-IN, ambako sasa pamejengwa jengo la ubalozi wa Marekani. Huko kulikuwa ni kwa watu matajiri zaidi, waliruhusiwa kuingia na magari yao kwenye ukumbi, watu wakikaa ndani ya magari na kuangalia filamu huku wakiburudika na vinywaji.
Empress ilikuwa mtaa wa Acacia (Samora au Independence avenues) jirani na ofisi za Maelezo, lakini sasa kunauzwa fenicha. Empire, ambayo ndiko kulikuwa ni kwa watu wenye fedha pia na picha za kifahari zaidi, ilikuwa kwenye jengo ambalo sasa ni makao makuu ya NMB. Nakumbuka nilienda kuona filamu ya Dracula, iliyochezwa na Christopher Lee, na wengi wa watazamaji ambao walikuwa waoga hawakuiangalia filamu hii, ikimwonyesha Dracula akinyonya watu damu na kuambukiza tabia hii kila aliyemdonoa kwa jino lake.
Lakini walala hoi tulikuwa na mahali pengine pia pa kwanda, Amana Social Hall. Pale Ilala. Sasa hivi ni kituo cha burudani na taasisi za mafunzo, lakini awali ilikuwa pia ni mahali tukienda kungalia sinema wikiendi na siku za sikukuu. Lakini majumba haya ya jamii- Community Social halls, yalikuwa kila mahali. Pale Kata ya Kingo Morogoro tulikuwa nalo. Na zaidi ya sinema palikuwa ni mahali pa kuchezezea muziki wa dansi na aina nyingine ya shughuli za kijamii. Bado lipo hadi leo.

Dar-es-Salaam haukuwa mji pekee wenye majumba ya Sinema. Nakumbuka kule kwetu Morogoro mjini, palikuwa na Shani Cinema na baadaye Sapna. Sapna, njia ya kwendi kituo cha reli, ndipo nilipoiona kwa mara ya kwanza filamu ya Disco Dancer – ikimchezesha msanii mkongwe sasa-Mithum Chakrabotty - na pia wanamuziki wa Afrika Kusini Soul Brothers, wakati ule tuliwaita tu kwa jina la Makurukunyi- matamshi potofu ya moja ya wimbo wao.

Kila Makao makuu ya mkoa yalikuwa na jengo lake la filamu, na mengi yalikuwa yakiendeshwa na wafanyabiashara wa asili ya India. Kwa hiyo sio jambo geni kuwaona bado wanashika dau kwenye tasnia ya filamu hadi leo. Naambiwa kule Lindi pale kwenye Ukumbi wa unaoitwa Y2K kwa sasa ndipo palikuwa na jengo kubwa la filamu likialika watazamaji kutoka mikoa yote ya kusini, hadi Songea!
Ilikuwa ni jambo la kawaida miaka hiyo kabla ya kuanguka tasnia ya sinema ilikuwa ukinunua gazeti, hasa siku za Jumatano, Ijuma, Jumamosi na Jumapili, kufungua kurasa za burudani kutafuta ni sinema ipi inaonyeshwa wapi, na wakati huo Wahindi walikuwa wakichuana sana na wacheza filamu kutoka Marekani na Uingereza.
Sasa hivi utamaduni huu umekwisha kwa mikoani. Majengo ya sinema yamekuwa nyumba za ibada, maduka au yamefungwa, au kubomolewa na majengo mengine kusimamishwa badala yake. Lakini cha muhimu zaidi ni kufikiria namna ya kuweka kumbukumbu, kuwa hapo zamani tulikuwa na majengo ya sinema. Tungeteua jambo moja tu ya majengo haya na kuweka kumbukumbu zetu hapo. Kuiona ile nembo ya New Chox kumenikumbusha mengi kuhusiana na burudani hapa nchini!
utaliiupdate@gmail.com This e-mail address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it , 0766959349



 


 
Last edited by a moderator:
Mkuu, BAK umenirusha mbali sana kuhusu hayo majengo ya Film ya zamani, ukianzia na Drive-In Cinema hadi New Chox. Nakumbuka dogo mmoja akijisifu kuwa alienda kuangalia picha NEWI CHOKS (New Chox).

Ni juzijuzi tu nilikuja kuelewa kuwa jamaa wengi waliokuwa wanacheza film na Bruce Lee kama Chuck Norris, Karim Abdul Jabbal na wengine wengi, walikuwa ni wanafunzi wake aliokuwa akiwafundisha Kung-Fu.

Enter the Dragon, hiyo clip umeweka juu, nafikiri ni moja ya SCENE zinazoheshimika sana na zitakumbukwa kwa siku nyingi zijazo maana aliyefikiria kuweka vioo ili vitengeneze reflections kibao, kwa kweli alicheza sana k-akili.

Ngoja na mie nikumbushe tulivyoangalia kwenye hayo majumba.....

Man from Africa (Michael Walker), Yellow:Black...Emanuelle, Disco Dancer, Love in Goa, na nyingine nyingi kutoka USA.....




Bibie Nazia Hassan (RIP) kutoka Pakistan na kibao cha Aap Jaisa Koi


Huo wimbo juu, ulikuwa mara nyingi ukifuatana radioni na kibao cha Night Fever by Bee Gees.

 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
...Sound track ya Saturday Night Fever bado inapendwa sana mpaka hii leo.
 
Kuna jumba moja lilikuja mwishoni, jumba ambalo ndio lilikuwa jumba lenye uwezo wa kuingiza watu wengi sana... Likijulikana kwa jina la Star Light.


Kiukweli hii ni kumbukumbu nzuri na ya kuuzunisha, maana enzi hizo kweli ilikuwa jambo la tunu sana kwa mtoto au hata mtu mzima kupelekwa sinema.


Kwanza halikuwa jambo rahisi kwa mtu tu asiye na ubavu kupata tiketi, haswa filamu ikiwa ni mpya na waigizaji wakiwa ni maarufu.


Nakumbuka walanguzi wa tikiti za sinema walikuwa wakimaliza kulangua pale New Chox sinema, walikuwa wakikimbilia Avalon Cinema, alafu sasa tikiti zilikuwa zikiuzwa nusu, kisha zilizobakia wale Wahindi wakiwapa watu wao na kuziuza kwa bei ya juu.


Pale Empire nako wakimaliza kuuza, walikuwa wakienda Empress... Ila jumba ambalo vijana wengi wakilipenda ni jumba la Empire kwa sababu walikuwa wakionyesha sinema nyingi za hollywood, na waendeshaji walikuwa na tabia ya kuongeza sauti haswa wakati wa mapigano, ili kuwakoleza watizamaji.


Majumba ya Cameo na Odeon haswa yalikuwa maarufu kwa sinema za Kihindi, wakifuatiwa na New Chox Cinema na Avalon na Empress alafu ndio Empire. Kule Drive inn Cinema wakazi wa Msasani wengi walikuwa wakijazana nje ya ukuta na kutazama sinema japokuwa hawakuweza kusikia sauti lakini wengi wakiridhika na hiyo hali. Niliwahi kumtembelea ndugu yangu mmoja akiishi maeneo ya Msasani, akanipa ofa bubu ya kwenda kutazama sinema, ah ah ah ah, akanipeleka Drive inn, kufika tukakaa nje ya ukuta na kununu karanga na juice, tukatafuta tofali na box chakavu kisha tukaa kuangalia movie... Sikumwambia kitu maana nilikuwa nikimuheshimu, mwenyewe nilishazoe kwenye majumba yetu ya kawaida, kama ukishindwa kununua tikiti basi unafanya kila njia kupenya au unampa pesa kidogo mwangalizi wa tikiti na kukuingiza ndani, ila kama jumba limejaa, basi unakaa kwenye ngazi za kutokea nje... Ah ah ah ah, ama kweli siku hazigandi.


Vijana wa leo wanaweza kushangaa wakisikia kuwa hata wimbo wa Taifa ulikuwa ukipigwa kabla ya onyesho, ila baadae sana ikaja kuondolewa kwa sababu ilisemekana kuwa hakukuwa na heshima, sababu wengine walikuwa ni walevi na hawakuwa wakisimama wima pale wimbo wa Taifa unapopigwa.


Hii biashara ya siema ilikuwaja kuanza kudorora vilipoanza vituo vya TV na kushamili kwa biashara ya video na maktaba za kukodisha video. Wengi walikuja kupendelea kukodisha kanda za video kuliko kwenda kwenye majumba ya filamu kwa sababu kwanza ilikuwa ghali kwa mtu mwenye familia, kugharamia watu zaidi ya wanne, pili filamu zenyewe nyingi zilikuwa baadae zikirudiwa rudiwa, nadhani shirika la filam Tanzania lilikuja kufirisika na kushindwa tena kuagiza filam mpya.


Haya majumba siku za mwisho mwisho walikuwa wakionyesha filamu mbili mpaka tatu kwa malipo ya kutazama filam moja, yaani ilikuwa ni kukesha, maana zilikuwa zikianza usiku.


Nakumbuka filam moja ya kihindi ilitamba sana katikati ya mwa miaka ya 70 na mwanzoni mwa miaka ya 80, filam yenyewe ilitoka mwaka 1975. Ilitwa Sholay, hii filam wahindi wa bongo walichapisha mpaka fulana zake na kuziuza...!

Hii ni moja ya scene, kutoka filam ya Sholay, ikielezea kuwa urafiki wao hautaisha mpaka kifo kiwatenganishe... Huu ni mwimbo wa gwiji wa utunzi wa nyimbo za kihindi enzi hizo akijulikana kwa jina la Kishore Kumar (rip). Enzi hizo kama filam ya Kihindi aikuwa na back singer ya Kishore au Mama gwiji la nyimbo za Kihindi kwa mahadhi yote Lata Mangeshkar, basi hiyo filam ina walakini, au ni kutoka vichochoroni... Hawa Magwiji wawili ndio walikuwa wakinogesha filam nyingi za Kihindi kwa utunzi ulio mahiri na sauti zao tamu. Na hata kwenye filam hii ya Sholay Kishore Kumar na Lata Mangeshkar, wameinogesha kwa umahiri wao mkubwa.


Angalia iki kipande kutoka filam ya sholay, Yeh Dosti Mtunzi Kishore Kumar



Yeh Dosti Sad Scene



Yeh Dosti with Lyrics Translation


MALE 1
(Yeh dosti hum nahin todenge
We will not break this friendship


Todenge dam magar tera saath na chhodenge) 2
I may break my strength, but I will not leave your side


MALE 2
Ae meri jeet teri jeet, teri haar meri haar
Oh, my victory is your victory, your loss is my loss


Sun ae mere yaar
Listen, oh my friend


MALE 1
Tera gham mera gham, meri jaan teri jaan
Your pain is my pain, my life is your life


Aisa apna pyaar
That is how our love is


MALE 2
Jaan pe bhi khelenge, tere liye le lenge
I will even risk my life, for you I will


MALE 1
Jaan pe bhi khelenge, tere liye le lenge
I will even risk my life, for you I will


BOTH
Sab se dushmani
Become enemies with everyone


MALE 1
Yeh dosti hum nahin todenge
We will not break this friendship


MALE 2
Todenge dam magar
I may break my strength


BOTH
Tera saath na chhodenge
But I will not leave your side


MALE 1
Logon ko aate hain do nazar hum magar
People see two of us, but


Dekho do nahin
Look, we are not two


MALE 2
Arre ho judaa ya khafa ae khuda hai dua
Oh, that we be separated or angry, oh God I pray


Aisa ho nahin
That this may not happen


MALE 1
Khaana peena saath hai
We will eat and drink together


MALE 2
Marna jeena saath hai
We will die and live together


MALE 1
Khaana peena saath hai
We will eat and drink together


Marna jeena saath hai
We will die and eat together


BOTH
Saari zindagi
For our entire lives


(Yeh dosti hum nahin todenge
We will not break this friendship


Todenge dam magar tera saath na chhodenge) 2
I may break my strength, but I will not leave your side



Haa Jab Tak Hai Jaan Sholay mtunzi ni Lata Mangeshkar



--FEMALE--
Oh, oh oh oh, oh oh oh oh
(Haan, jab tak hai jaan jaane jahan


Yes, as long as I have life, oh lover
Main naachoongi) - 4


I will dance


(Pyaar kabhi bhi marta nahin
Love never dies


Maut se bhi yeh darrta nahin) - 2
It doesn't even fear death


Lut jaayenge, mit jaayenge, mar jaayenge hum
We will be robbed, ruined, and we will die


Zinda rahegi hamaari daastaan
But our story will stay alive


O haan, jab tak hai jaan jaane jahan
Oh yes, as long as I have life, oh lover


Main naachoongi
I will dance


Toot jaaye paayal to kya
If my anklet breaks, so what?


Paaon ho jaaye ghaayal to kya) - 2
If my legs become wounded, so what?


Dil diya hai dil liya hai, pyaar kiya hai to
Having given my heart, taken a heart, fallen in love, so


Dena padega mohabbat ka imtehaan
I have to give love's test


O haan jab tak hai jaan jaane jahan
Oh yes, as long as I have life, oh lover


Main naachoongi - 4
I will dance


(Yeh nazar jhuk sakti nahin
These eyes cannot be cast down


Yeh zubaan ruk sakti nahin) - 2
This voice cannot be stopped


Main kahoongi gham sahoongi chup rahoongi kya
I will speak, I will bear pain, why should I stay silent?


Bebas hoon lekin nahin main bezubaan
I am out of control but I am not speechless


O haan jab tak hai jaan jaane jahan
Oh yes, as long as I have life, oh lover


Main naachoongi
I will dance


Haan jab tak hai jaan jaane jahan
Yes, as long as I have life, oh lover


Main naachoongi - 5
I will dance


Waigizaji wakuuu kwenye filam hii ni Amitabh Bachchan,marehemu Amjad Khan, Dharmendra, Sanjeev Kumar, na Hema Malini, . Wengi walioona ile filam watamkumbuka Mzee Amjad Khan, au kubwa la maadui, ambaye alikuwa akikionea kijiji jilani na makao yake ya ujambazi, kijiji kilichokuwa kikiongozwa na Askali afisa mstaafu ambaye alikuwa amekatwa mikono na jambazi huyu, na karibia familia yake yote kuuliwa na Mzee mwenyewe Amjad Khan akienda kwa jina la Gabbar Singh... Yaani kwenye hii filam wanakijiji wakisikia tu jina Gabbar Singh, basi ni sawa na kusikia kuwa kuna Tsunami inakuja, ni hofu kwa kwenda mbele, kwa ufupi alitisha kwa ukatili wake na haswa ukizingatia kuwa ana mfuasi wake mwenye shabaha kupita wote kwa jina la Sambha... Mtaani ilikuwa si ajabu kumsikia kijana akitania kwa kuita Halioooo Sambhaaaa, yaani kwenye filam Mzee mzima Gabbar akipoiti na kuita hivyo ujue kinacho fuata ni shaba.


Huyu mzee Mstaafu "Thakur Sahib" jina halisi Sanjeev ****, aliomba msaada kwa wahalifu wawili wazoefu, waliokuwa jela kwa ahadi ya kuwalipa Rs 20,000, pamoja na zawaidi ya Rs 50,000, (Rs 1=Tshs 31) kama watafanikiwa kumkamata au hata kumuua jambazi Gabbar Singh, kwa sababu askari kutoka serikali walikwisha shindwa kumkamata ilikuwa ni sawa na suicide mission... So Mstaafu akamua kuwasiliana na hawa waalifu Amitabh Bachchan akijulikana kwa jina la Jai Dev, a.k.a Jai, Dharmendra ambaye alitumia jina Veeru, walikuwa marafiki wa kufa na kuzikana.

Enzi ya hayo majumba kwenda kuangalia filamu kama Dracula, ilikuwa issue, wengi walikuwa wakitishika kuiangalia hiyo filamu, lakini siku hizi kutokana na utaalam na watu kuzoea kuangalia move zenye special effect nyingi, imeifanya movie kama dracula istishe tena... Yaani kwa kizazi cha dot comu, hii filam itawa bore tu.
 
Last edited by a moderator:
Mwanza kulikuwa na TIVOLI nakumbuka ndipo nilipooona filamu ya Bruce Lee - Enter the Dragon show ya midnight. Pia kulikuwa na LIBERTY CINEMA
 
Tanga kulikuwa na Majestic Cinema, Regal, Novelty na Tanga Cinema.

Ilianza kufa tanga cinema, ikafuata novelty, baadae Regal na mwisho majestic. Hapo Majestic ndipo niliiona Commando ya Arnold Swarzneggar kwa mara ya kwanza, ilikuwa ni mwaka 1990, mzee alinipa pesa nikaone hiyo cinema kama pongezi kwa kufaulu mtihani wa darasa la saba. Ni katika movie hiyo nilijua kuna kitu kinaitwa flying boat...yaani aina ya ndege inayotua baharini na kuondokea baharini...sikuwa nimewahi hata kufikiri hicho kitu maana siku hizo tukiaminishwa ndege(siyo hedikopta) haiwezi kutua kwenye vumbi(seuze majini) kwani italipuka pia mafuta yake tuliambiwa yalitokana na mafuta ya korosho.

Kwa wale waliowahi kuiona Kaalia au Andhaa Kanoon(filamu za Amitabh), hizo niliziona Regal Cinema kule uhindini, sasa ni ukumbi nadhani na pale jirani kuna tax consultancy firm inaitwa shebrilla.

Hizo zilikuwa siku...ukijua leo kuna mchezo wa redio saa tatu na nusu usiku hubanduki redioni uwasikie marehemu Kipara, Rajab Hatia, Hamisi Tajiri, Zena Dilip, Ally Keto......

Ah........kweli siku hazigandi!!!!
 
Mkuu Naona DSM Jenga la Cameo Ulilisahau Ndio lilikuwa karibu sana na Home Sie Tulikuwa tunaingia kule wanaporushia Picha Hawa jamaa nadhani walikuwa walikuwa wanaitwa Director japo kulikuwa na kelele lakini tulikuwa tuna enjoy huku tukipigwa na upepo mkali tunatizama hadi mikanda inapokuwa inaunganishwa kila unapoisha...

Movie ya Kihindi Ikifika Mapumziko inaandikwa INTERMISSION. Mnatoka nje kula Bisi Pipi Big G, good Gud
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom