Majukumu ndani ya nyumba.

Jaguar

JF-Expert Member
Mar 6, 2011
3,438
1,026
Ndani ya nyumba,mume na mke wote mmeajiriwa na kila mmoja ana kazi yake.Inawezekana mshahara wa mume ukawa mkubwa kuliko wa mke au vice versa.Nimekuwa nikisikia akina mama wengi wakisema,mshahara wa mume ndo kila kitu,kuanzia matumizi madogo madogo ndani ya house mpaka yale makubwa ya kimaendeleo,mshahara wa mke hauhusiki,ana uhuru wa kuutumia atakavyo tena bila kuhojiwa.Hili swala limekaaje au ndo utamaduni wetu wa Tanzania?
 
mwanaume ndio kichwa cha nyumba_remember!,....hata hivyo kusaidiana muhimu
 
Huo utamaduni unatumika kwa baadhi,sioni tatizo kama mwanaume ana uwezo au ameridhia hilo lifanyike.Nafikiri si sahihi kumuachia majukumu ya kifedha mwanaume unless kama situation ya mume ni mtu kama Mengi na mke ni mwalimu wa primary,otherwise ushirikiano ni muhimu kutegemea na kipato....
 
Familia ni two way traffic,mnatengeneza budget na mnaiwezesha kwa pamoja kutokana na kilichopo.Km mama anategea na ana kipato hiyo ni policy yenu.
 
Familia ni two way traffic,mnatengeneza budget na mnaiwezesha kwa pamoja kutokana na kilichopo.Km mama anategea na ana kipato hiyo ni policy yenu.
Hayo maneno,kama mimi ndo kichwa cha nyumba inamaanisha ninajukumu la ku control everything in the house mpaka vipato vyetu sote wawili.
 
Baba katika nyumba....hatambuliki kwa jina bali kwa majukumu yake.Pia makubaliano katika nyumba ni jambo la watu wawili...sababu shughuli za kuendeleza familia hazina ''nembo'' kwamba hizi ni za mama hizi ni za baba.
 
Ndani ya nyumba,mume na mke wote mmeajiriwa na kila mmoja ana kazi yake.Inawezekana mshahara wa mume ukawa mkubwa kuliko wa mke au vice versa.Nimekuwa nikisikia akina mama wengi wakisema,mshahara wa mume ndo kila kitu,kuanzia matumizi madogo madogo ndani ya house mpaka yale makubwa ya kimaendeleo,mshahara wa mke hauhusiki,ana uhuru wa kuutumia atakavyo tena bila kuhojiwa.Hili swala limekaaje au ndo utamaduni wetu wa Tanzania?
Hapo kwenye bluu ni sahihi kabisa, otherwise unasaidiwa tu, Lakini mwisho wa siku zengwe likiibuka mnagawana mali sawa kwa sawa! upo hapo kaka? that is life.
 
Hapo kwenye bluu ni sahihi kabisa, otherwise unasaidiwa tu, Lakini mwisho wa siku zengwe likiibuka mnagawana mali sawa kwa sawa! upo hapo kaka? that is life.
Mkuu ni sahihi au ndivyo ilivyo?,mi naona si sahihi ila haikwepeki!
 
Haki zinakwenda pamoja na wajibu! Lazima kuwepo na balance kuhusu haya mambo mawili. Huwezi kuchukua moja ukaacha jingine.
 
Elia;1930233]Hapo kwenye bluu ni sahihi kabisa, otherwise unasaidiwa tu, Lakini mwisho wa siku zengwe likiibuka mnagawana mali sawa kwa sawa! upo hapo kaka? that is life.

Kama ni kusaidiwa utasaidiwa tu kaka haijalishi unatowa pesa ya kutosha au hapana. Ni wangapi wana kila kitu katika familia zao nikimaanisha mali lakini wanasaidiwa?

Zaidi mimi Naona ni makubaliano mlio nayo kwenye ndoa yenu. Kuna wengine wanapenda ushirikiano ikiwa na maana mke na mme mnaweka budget yenu na plan mlizo nazo. Na budget inakuwa na mapato na matumizi yenu. Ukikuta mke anasema kipato chake ni chake na cha mme ni chake mara nyingi haya masuala ya budget shirikishi hayapo. Mtakuwa mnabudget nini wakati budget member mmoja hatowi ushirikiano wa kuwezesha budget? Mara nyingi katika situation kama hii ambayo mme anakuwa ni kila kitu hata chumvi na nyanya na mke anacho kipato kunakuwa na matatizo hata kwenye projects wanazofanya.Nikiwa na maana unaweza kukuta baba anafanya mambo bila ushirikishwaji mzuri wa mke. Itaonekana pia kuwa hiki ni cha baba na hiki ni cha mama, chanzo cha ubinafsi katika ndoa.

Kushirikiana naona ni vema hata kama kipato cha mke ni kidogo ukilinganisha na cha mme.Kwa kuzingatia vipato vyenu mtajuwa kipi kiende wapi na kipi kibaki wapi. Na hii pia inasaidia kuwaweka karibu kama mambo yenu mnayafanya kwa pamoja.
 
Elia;1930233]Hapo kwenye bluu ni sahihi kabisa, otherwise unasaidiwa tu, Lakini mwisho wa siku zengwe likiibuka mnagawana mali sawa kwa sawa! upo hapo kaka? that is life.

Kama ni kusaidiwa utasaidiwa tu kaka haijalishi unatowa pesa ya kutosha au hapana. Ni wangapi wana kila kitu katika familia zao nikimaanisha mali lakini wanasaidiwa?

Zaidi mimi Naona ni makubaliano mlio nayo kwenye ndoa yenu. Kuna wengine wanapenda ushirikiano ikiwa na maana mke na mme mnaweka budget yenu na plan mlizo nazo. Na budget inakuwa na mapato na matumizi yenu. Ukikuta mke anasema kipato chake ni chake na cha mme ni chake mara nyingi haya masuala ya budget shirikishi hayapo. Mtakuwa mnabudget nini wakati budget member mmoja hatowi ushirikiano wa kuwezesha budget? Mara nyingi katika situation kama hii ambayo mme anakuwa ni kila kitu hata chumvi na nyanya na mke anacho kipato kunakuwa na matatizo hata kwenye projects wanazofanya.Nikiwa na maana unaweza kukuta baba anafanya mambo bila ushirikishwaji mzuri wa mke. Itaonekana pia kuwa hiki ni cha baba na hiki ni cha mama, chanzo cha ubinafsi katika ndoa.

Kushirikiana naona ni vema hata kama kipato cha mke ni kidogo ukilinganisha na cha mme.Kwa kuzingatia vipato vyenu mtajuwa kipi kiende wapi na kipi kibaki wapi. Na hii pia inasaidia kuwaweka karibu kama mambo yenu mnayafanya kwa pamoja.
Akhsante mkuu!
 
mwanaume anaweza kuwa na mashati manne na suruali nne na akaonekana smart kila siku .mwanamke sasa nguo mpya kila kukicha maurembo, ndio maana tunajikuta tunatumia vipesa vyetu kwa mambo kama hayo, ila kama unamshahara mkubwa si vibaya kusaidiana na mwenzako
 
Huo utamaduni unatumika kwa baadhi,sioni tatizo kama mwanaume ana uwezo au ameridhia hilo lifanyike.Nafikiri si sahihi kumuachia majukumu ya kifedha mwanaume unless kama situation ya mume ni mtu kama Mengi na mke ni mwalimu wa primary,otherwise ushirikiano ni muhimu kutegemea na kipato....

Hilo nalo neno asante Michelle.
 
Back
Top Bottom