Majina yetu jamani

tatizo sisi wenyewe huwa tunapenda kujibadili majina, utakuta mtu wazazi wake wamempa jina kama BARAKA yeye akiwa mkubwa anajibadilisha na kujiita BRESSING. Sio vizuri inafaa tupende asili yetu.
 
Mziwanda (maana yake mtoto wa mwisho, wengine huita kitinda mimba) hii imekaa vizuri sana, unanikumbusha wakati ninasoma kulikuwa na stori nilihadithiwa na jamaa yangu, aliniambia alikuwa na jamaa yake alienda Ulaya kusoma, jamaa alikuwa anaitwa Daudi Ndege, sasa kwa kupenda kwake uzungu aliporudi nyumbani alianza kujiita Dav Bird, sasa jamaa zake wakashindwa kulitamka hilo jinale jipya na kuishia kulibadili kabisa na kumuita Davibade! Unajua haya majina ya kizungu hasa ya kiingerza ambayo watu wengi hupenda kujipachika ukitafsiri maana yake kwa kiswahili hakuna ataye penda tena kujiita. Mfano mwingine kuna yule jamaa anetoa simulizi zake katika kipindi cha sinto sahau, anajiita ROGERS, nimeambiwa eti jina lake halisi ni RAJABU, sasa hebu tazama kapoteza kabisa maana ya jina! Kisa Uzungu
 
Kwani hamna wazungu wanao ongea Kiswahili dada?
wapo baadhi wanaongea hicho kiswahili. lkn sijawahi kuona shule au chuo cha kizungu wanafundisha masomo yao kwa lugha ya kiswahili. Tanzania sasa hivi shule zote ni english tu kuanzia chekechea hadi chuo. shule pekee zilizobaki kufundisha lugha ya kiswahili ni shule za primary za serikali tu.
 
majina ya kizungu hamtaki, mbona kizungu mmeiga?

Majina, mavazi, lugha, dini ya kizungu na kiarabu vyote ni matokeo ya utumwa, ukoloni asilia na ukoloni mamboleo. Karne zile kabla ya utumwa na ukoloni ninauhakika hakukuwa na mwafrika hata mmoja mkristo wala muislam. Waafrika tulikua na majina, mavazi, dini, mila na desturi zetu wenyewe tofauti (si 'inferior') na za watu wengine duniani kote.

Changamoto iliyopo ni kufuta athari mbaya za utumwa na ukoloni na tuanze kuenzi historia, utamaduni na utambulisho wetu kama Waafrika. Kirahisi zaidi cha kuanza nacho ni majina. Kisha taratibu tutaachana na lugha, mavazi na dini zote za kigeni. Hivi ndo waasia wanavyofanya. Ndo maana wana uhuru na maendeleo kuliko sisi. Kwasababu wanajitambua.

Sisi tutaendelea tu kuwa tegemezi?

Hapana. Tuanze kubadilika. Tuanze na majina.
 
Mziwanda (maana yake mtoto wa mwisho, wengine huita kitinda mimba) hii imekaa vizuri sana, unanikumbusha wakati ninasoma kulikuwa na stori nilihadithiwa na jamaa yangu, aliniambia alikuwa na jamaa yake alienda Ulaya kusoma, jamaa alikuwa anaitwa Daudi Ndege, sasa kwa kupenda kwake uzungu aliporudi nyumbani alianza kujiita Dav Bird, sasa jamaa zake wakashindwa kulitamka hilo jinale jipya na kuishia kulibadili kabisa na kumuita Davibade! Unajua haya majina ya kizungu hasa ya kiingerza ambayo watu wengi hupenda kujipachika ukitafsiri maana yake kwa kiswahili hakuna ataye penda tena kujiita. Mfano mwingine kuna yule jamaa anetoa simulizi zake katika kipindi cha sinto sahau, anajiita ROGERS, nimeambiwa eti jina lake halisi ni RAJABU, sasa hebu tazama kapoteza kabisa maana ya jina! Kisa Uzungu

kweli mtu wangu. Ni mawazo mgando tuliyonayo hata baada ya kujitambua kielimu. Ni uhuru lkn wa bandia
 
Back
Top Bottom