Majina ya wauza Madawa ya Kulevya: Kikwete anayo!

Mtz umenena JK anayo majina hayo siku nyingi toka kipindi cha marehemu Amina Chifupa,tatizo la jk ni lielile siku zote nikutojiamini,wala rushwa wakubwa hivyo hivyo hana uwezo nao,ndio wafadhiri wakubwa wa ccm.

Wauza madawa ya kulevya ndio wenye nchi,kwa hiyo hakuna wanaloweza kufanywa.After all hiyo ni moja ya agenda zao,kuwafanya vijana wetu wawe mandondocha and therefore easy to govern and manipulate,
 
Kwani hatuwezi kuwataja humu?

hii nchi ya longolongo tu,kila mtu anambwayambwaya kuhusu madawa ya kulevya! Vijana tupo nao mtaa wanaumia tu na madawa,soko linakua tu! Kitengo cha madawa ni rahisi sana kufuatilia hili,kutokea mtumiaji wa mwisho kupanda mpaka kumpata papa wao mkubwa! ila ndio hivo kila mtu anaangalia maisha yake,akipigwa mtu risasi kisa amefuatilia hili soo nani wa kumlinda??

hatuna usalama wa taifa,labda usalama wa matumbo...
 
names labda kikisha kipindi alichowapa wajirekebishe wasipojirekebisha atawataja
lini
kila mtu anaogopa kufa kwa kuuwawa na wauza unga,hata mkulu wa nchi anatetea unga wake,

longolongo hizi zimeanza 2006 na hakuna kitakachofanyika na mkulu ataondoka ktk kiti hakuna kitakachofanyika

subirini mtaona
 
Jina lake limo? Kama limo hamtomsikia akisema chochote. Kuwepo sio lazima liandikwe Jakaya Mrisho Kikwete linaweza likawemo kwa namna nyingine.

Majina ya vigogo ninayo-JK

03 Oct 2006
By Mwandishi Wetu


Rais Jakaya Kikwete, amekiri kupokea majina ya vigogo wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya na kwamba majina hayo yanafanyiwa kazi na watendaji wake.

Rais Kikwete aliyasema hayo jana alipokuwa akizungumza na taifa kupitia kwa wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari Ikulu jijini Dar es Salaam.

Alikuwa akijibu swali kutoka mmoja wa wahariri aliyetaka kujua iwapo amepokea waraka wenye majina ya vigogo wanaodaiwa kujihusisha na dawa za kulevya.

Bila kufafanua, Rais Kikwete alijibu, “waraka nimeupata na nimewapa wahusika na wanaufanyia kazi.” Inadaiwa kwamba, katika waraka huo ulioandikwa na kikundi kimoja cha wananchi, kimetaja majina ya vigogo zaidi ya 100 wanaodaiwa kujihusisha na biashara ya ama kuingiza nchini dawa za kulevya au kuwa mawakala wa dawa hizo au wauzaji.

Kwa mujibu wa waraka huo, baadhi ya wafanyabiashara waliotajwa ni wa kutoka mikoa ya Tanga, Mbeya, Dodoma, Kigoma, Arusha, Iringa, Manyara, Kilimanjaro, Dar es Salaam na Zanzibar wamedaiwa kuhusika na biashara hiyo.

Aidha, katika waraka huo, umetaja baadhi ya hoteli Jijini Dar es Salaam, kutumiwa kama vituo maalum vya kukutanisha wafanyabiashara wa dawa hizo, kwa ukanda wa Nchi za Afrika Mashariki na Kati.

Kazi ya kuandaa taarifa hiyo yenye kurasa 12, ilifanywa na Shirika moja linalopigania haki na Usawa na Mazingira katika Jamii la Jijini Dar es Salaam.

Imeelezwa kwamba, taarifa hiyo ya siri, ilikabidhiwa kwa Rais Kikwete kupitia kwa Waziri wa Usalama wa Raia, Bw. Bakari Mwapachu.

Katika taarifa hiyo, yamo baadhi ya majina ya wabunge, wafanyabiashara maarufu, maofisa wa idara nyeti za serikali kama vile Mamlaka ya Mapato Nchini, Benki Kuu (BoT) na maofisa wakuu waandamizi wa Jeshi la Polisi, pamoja na watendaji wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Nchini.

Viwanja vilivyotajwa kwenye waraka huo ni Dar es Salaam, Kilimanjaro (KIA), Zanzibar (Karume Aiport), Tanga, Arusha na Mbeya.

Mbali na viwanja vya ndege, waraka huo umetaja wafanyabiashara hao kuzitumia Bandari za Dar es Salaam, Tanga, Zanzibar na fukwe za Bagamoyo kuingiza shehena kubwa za dawa hizo.

Taarifa hiyo pia imetaja majina na namba za magari ya watu yanayotumika kusafirisha dawa hizo na kusambaza kwa walengwa jijini Dar es Salaam.

Pia majina ya kampuni za ndege zinazotumiwa na watuhumiwa hao kuingiza dawa, huku wengine wakitumia mikataba ya usafirishaji wa vifaa vya hospitali pamoja na matairi ya magari.

* SOURCE: Nipashe
 
Tazama kauli ya kiongozi wa taasisi ya kupambana na rushwa(TAKUKURU) ya Dk,Hosea "Mkuu alininiambia hapendi kuona kesi za viongozi wakuu wastafu zikipelekwa mahakamani,na kusema tuwaheshimu viongozi waliopita"Ni ukiri wa Dk.Hosea alipo kuwa akihojiwa na jasusi wa kimarekani.Sasa kwa kauli kama hizo hakuna haja ya watanzania kuamini kuna haja ya kweli kwa serikali ya kikwete kupambana na rushwa ndiyo maana wakina Rostam,Chenge,Kikwete,Sumaye,Karamagi nawengine wengi wanajiamini kwani baba yao ndiye mlinzi wao.
 
Back
Top Bottom