ndetichia
JF-Expert Member
- Mar 18, 2011
- 27,772
- 6,555
kumbe shehe yahya mwizi kweli alikuwa anapenda sana kusema rangi ya udhulungi..nimekuta haya majina kwenye Bibilia
kumbe shehe yahya mwizi kweli alikuwa anapenda sana kusema rangi ya udhulungi..nimekuta haya majina kwenye Bibilia
picha ya ninipicha tafadhari!
Kiswahili ni lugha ya Kibantu, na lugha (nyingi) za Kibantu, kwa asili, zinaelekea kuwa na maneno matatu tu yanayoeleza dhana ya rangi:
1. Rangi nyeupe,
2. Rangi nyeusi, na
3. Rangi nyekundu.
Kama unazungumza lugha mojawapo ya Kibantu, jaribu kutafuta majina ya rangi, na utakutana na maneno ya rangi hizi tatu tu.
Katika Kiswahili, maneno mengine yanayotaja rangi tumekuwa tukiyapata kwa: (i) kutohoa kutoka lugha nyingine, kama vile Kiarabu na Kiingereza, na (ii) kwa kutumia analojia, yaani, kufananisha rangi husika na ile ya kitu fulani (kama vile chungwa, kahawa, zambarau, majani, udongo, ugoro, damu ya mzee, n.k.).
Kwa maneno yenye asili ya Kibantu, utaona kuwa maneno hayo yanaoana vizuri na sarufi ya lugha ya Kiswahili kwani yanatokea kama vivumishi vya kawaida tu vya neno 'rangi' (tazama <rangi nyeupe>, <rangi nyeusi>, <rangi nyekundu>; linganisha na <rangi nzuri>, <rangi mbaya>, <rangi nyingi>).
Lakini kwa maneno yanayoeleza rangi ambayo yametoholewa au yanatumia utaratibu wa analojia, utaona kuwa tunahitaji kutumia kihusishi <ya> ili kuhusisha 'rangi fulani' na 'kitu fulani', kama vile:
4. Rangi ya bluu (na sio rangi bluu),
5. Rangi ya kijani (na sio rangi kijani),
6. Rangi ya zambarau (na sio rangi zambarau),
7. Rangi ya samawati (na sio rangi samawati) n.k.
Kwa wazungumzaji tulio wengi, kanuni hizi (za kutumia au kutotumia <ya>) tunazijua lakini hatujui kwamba tunazijua! Kwa wanaojifunza Kiswahili ukubwani, inawabidi wajifunze kanuni zote hizi. Utawasikia wengine wakisema <Hii nguo ina rangi ya nyekundu.>.
Hudhurungi ni Orange au rangi ya goldGreen - kijani
orange - hudhurungi (siyo grey)
grey - kijivu
yellow - manjano
white - nyeupe
gold - dhahabu
red - nyekundu
kuna rangi inaitwa "chanikiwiti" sikumbuki ni rangi gani kwa kizungu
Hudhurungi ni Orange au rangi ya gold
Purple = Zambarau (matunda ya mizambarau au mawengewenge)
sky blue = samawati/ blue bahari
brown = Hudhurungi/damu ya mzee/udongo
dark green - kijani kibichi
grey - kijivu
khaki = majani makavu
red rose = Waridi jekundu
yellow = njano
silver = fedha
black =nyeusi
mengine mmeenda sawasawa.. hudhurungi ndiyo pink.
Chanikiwiti = bright green