Majina ya Asili ya Kitazania na maana zake

kidadari

JF-Expert Member
Jul 26, 2012
8,647
9,574
Kutokana na mabadiliko ya maisha pamoja na utandawazi Mila na desturi hasa majina ya asili ya kitanzania yanazidi kupotea! nimeona ni vizur kuanzisha Uzi huu ili tuweke kumbukumbu vizuri za Maana ya majina yetu kwa ajili ya kizazi kijacho. Naanza na majina ya Kichagga halafu members wataongezea kutokana na asili yao.
1. Elisonguo-Mungu tangulia
2.Eliambuya- Mungu angalia
3.Ruaichi/Rwaichi- Mungu unajua
4.Ndenengo/Ndeinengo- Nilipewa
5.Pendaeli- Mungu ni Pendo
6. Oforo- Baraka.
7.Ndewihirio moo- Nilirudishiwa uhai( watoto waliopata tabu wakati wa kuzaliwa)
8.Ndetaramo- Nilisaidiwa
9. kisie( Masika)
10.Haika/Aika- Asante
11. Manka- mtoto wa pili( wa kike)
Wadau tuendee kuongeza majina ya asili ya makabila yetu na maana zake kwa ajili ya kizazi kijacho.

NB: hayo ndo majina yenye asili ya kichagga. majina kama Masawe, Mushi, Tillya, Laswai , Lyimo na Mtei ni majina ya ukoo Mara nyingi hayana maana!
 
12.Kyalow...mtu mzito au tajiri
13.Ling'anyi...Likubwa
14.Ibanya......
 
Kutokana na mabadiliko ya maisha pamoja na utandawazi Mila na desturi hasa majina ya asili ya kitanzania yanazidi kupotea! nimeona ni vizur kuanzisha Uzi huu ili tuweke kumbukumbu vizuri za Maana ya majina yetu kwa ajili ya kizazi kijacho. Naanza na majina ya Kichagga halafu members wataongezea kutokana na asili yao.
1. Elisonguo-Mungu tangulia
2.Eliambuya- Mungu angalia
3.Ruaichi/Rwaichi- Mungu unajua
4.Ndenengo/Ndeinengo- Nilipewa
5.Pendaeli- Mungu ni Pendo
6. Oforo- Baraka.
7.Ndewihirio moo- Nilirudishiwa uhai( watoto waliopata tabu wakati wa kuzaliwa)
8.Ndetaramo- Nilisaidiwa
9. kisie( Masika)
10.Haika/Aika- Asante
11. Manka- mtoto wa pili( wa kike)
Wadau tuendee kuongeza majina ya asili ya makabila yetu na maana zake kwa ajili ya kizazi kijacho.

NB: hayo ndo majina yenye asili ya kichagga. majina kama Masawe, Mushi, Tillya, Laswai , Lyimo na Mtei ni majina ya ukoo Mara nyingi hayana maana!
mkuu nini maana ya haya majina ya kichaga Ndetirima, Ndesangia, Ndesamburo, Ndesanjo na kwa nini majina mengi ya kichaga yanaanzana na kitangulishi Nde- ?
 
Kutokana na mabadiliko ya maisha pamoja na utandawazi Mila na desturi hasa majina ya asili ya kitanzania yanazidi kupotea! nimeona ni vizur kuanzisha Uzi huu ili tuweke kumbukumbu vizuri za Maana ya majina yetu kwa ajili ya kizazi kijacho. Naanza na majina ya Kichagga halafu members wataongezea kutokana na asili yao.
1. Elisonguo-Mungu tangulia
2.Eliambuya- Mungu angalia
3.Ruaichi/Rwaichi- Mungu unajua
4.Ndenengo/Ndeinengo- Nilipewa
5.Pendaeli- Mungu ni Pendo
6. Oforo- Baraka.
7.Ndewihirio moo- Nilirudishiwa uhai( watoto waliopata tabu wakati wa kuzaliwa)
8.Ndetaramo- Nilisaidiwa
9. kisie( Masika)
10.Haika/Aika- Asante
11. Manka- mtoto wa pili( wa kike)
Wadau tuendee kuongeza majina ya asili ya makabila yetu na maana zake kwa ajili ya kizazi kijacho.

NB: hayo ndo majina yenye asili ya kichagga. majina kama Masawe, Mushi, Tillya, Laswai , Lyimo na Mtei ni majina ya ukoo Mara nyingi hayana maana!
No 3. Nimepata kusikia kuwa ni pumzi ya Mungu...cc Ruachi band inayoongozwa na Godwini Ombeni
 
mkuu nini maana ya haya majina ya kichaga Ndetirima, Ndesangia, Ndesamburo, Ndesanjo na kwa nini majina mengi ya kichaga yanaanzana na kitangulishi Nde- ?
Majina mengi yanaanza na Nde ikimaanisha kipindi kilichopita mfano NDE-sanjo maana yake nilioshwa! na hii hutokana na matukio yaliyotokea wakati wa kuzaliwa!
Ndetirima- NILISUBIRI hii inaweza kuwa wakati wa kuzaliwa hakukuwa na mkunga karibu hivyo mama akasubiri mapaka mkungwa atafutwe aje.. kumzalisha!
.Ndesamburo- Mwenye Baraka. Mengine maana zake cjazipata mkuu
 
No 3. Nimepata kusikia kuwa ni pumzi ya Mungu...cc Ruachi band inayoongozwa na Godwini Ombeni
kwa kichaga Rua/Ruwa au Eli linamaanisha Mungu, na AICHI maana yake ni anajua....... Ruaichi means Mungu anajua.
 
Mboni-Jicho
Kigenda-Wamwendo
Mainda-Maringo
Nenkondo-Ndio jambo
Mhina-Mwanafunzi
Kiaga-Ahadi
Kajembe-Jembe

Mkoa wa Tanga.
 
Back
Top Bottom