Majina saba ya askari walio uwawa Sudan

attachment.php


Vifo hivi viwakumbushe wanajeshi wetu kwamba watanzania wote ni ndugu na kwamba sote ni mavumbi na mavumbini ni lazima tutarudi. Mateso wanayoyafanya wanajeshi kwa raia wa Mtwara ni ya kinyama!!! Si ya kiutu hata kidogo!!! Ni bahati mbaya kwamba jeshi letu linatumiwa vibaya na wanasiasa!!! Mungu aturehemu sote na roho za wanajeshi hawa zipumzike kwa amani!!

Kweli kabisa ndugu yangu. Askari wetu wamezoea kuwageuza wananchi ngoma kwa kuwapiga na kuwaua bila sababu. Pamoja na ruhusa waliyopewa na waziri mkuu wakumbuke kuwa nao ni binadamu, wananchi wanapoumia na kusoneneka kutokana na mateso wanayoyapata kutoka kwa askari na wao kama binadamu yanapowafika hayo machungu ni yale yale. Hata waziri mkuu naye pamoja na amri zake akumbuke kuwa na yeye ni binadamu na ana ndugu ambao asingependa wapigwe au wauawe bila hatia kama inavyotokea Mtwara na kama ilivyotokea Arusha, Iringa, Morogoro na Ruvuma. Waziri mkuu angekuwa hata na chembe ndogo ya aibu angeomba radhi kwa kutoa kauli ile yenye ukakasi. R.I.P wanajeshi wetu mliouawa bila hatia.
 
Hayo maneno uliyoandika hapo chini ni upumbavu na kukosa akili kuliko pitiliza.
Rest in peace askari wetu. Mmekufa kishujaa
Upumbavu gani alioandika? Hujawahi pelekwa kambini wewe ukaona
jinsi wanavyopiga na ukirudi breki ni hospitali na si nyumbani, makovu yangu
hayajafutika mpaka leo subiri siku nipige picha yangu na ya wenzangu niyaweke
hapa JF.
 
kwanza kuna msiba hapa tuwape POLE wanafamilia na wanajeshi wenzao.Hili la UISLAMU na Ukristo au Upagani wa wanajeshi ni akili ndogo kuwaza hivyo sasa. SAINT IVUGA Kwa nini uanzishe mjadala huo sasa?WEWE AKILI YAKO NA MIKONO YA KUANDIKA HAVIWASILIANI?
 
RIP mashujaa wetu. Mliobaki msife moyo kwani hiyo ni ajali tu ya kivita. Sasa ongezeni tahadhari kwa maana tunajifunza tokana na makosa.
Kwa mnaoshabikia kumbukeni waliokufa ni makaka, wadogo zetu, watoto na wajukuu zetu. Tuziweke itikadi pembeni na tuwafariji waliopoteza wapendwa wetu. Kama ni vyama hata huko Jeshini wapo wengi tu wanapenda mabadiliko kwani nao wanaguswa na matatizo yanayosababishwa na utawala mbovu hapa nyumbani, lakini tunapomkabili adui toka nje ya mipaka sote tu wamoja.
 
Nasikitika nahao waislam mauti yamewakuta katika mwezi mtukufu Wa ramadhani walitakiwa wafanye ibada

ibada ni muda wote siyo ramadhan tu. hulijui hilo. usilete udini hapa. wasikitikie wote waliouawa na kuwaombea kwa Mungu awapokee
 
Kuna ushahidi gani uliotumika kueleza jinsi walivyoshambuliwa..? au kuna walionusurika kufa...?
R.I.P our beloved Tanzanians.

Yes!wapo walionusurika kufa ila wana majeraha na wako hospitalini kwa mujibu wa taarifa.
 
Mungu awajaalie pumziko mahali pema. Natamani sana damu yao isipotee bure, isaidie kuleta amani waliyoifia
 
Hivi mkuu wameifia Tanzania
ama Sudan?Naomba kueleweshwa kwenye hili.Kuuliza si ujinga mkuu
wangu.

Aliyewapeleka Darfur ndio mwenye Maslahi yake binafsi. Muulizeni Membe na bosi wake maana wanapenda sana sifa za Kijinga
 
Mungu atupe nguvu wafiwa na hasa familia, JWTZ na watanzania wote kwa ujumla. Msiba ni wetu sote. Natamani wangepelekwa uwanja wa taifa ili tupate nafasi ya kwenda kutoa heshima za mwisho kwa mashujaa wetu hawa.
 
Very sad. Poleni sana familia, ndg na jamaa wote walioguswa na msiba huu mzito kwa namna moja au nyingine. Bila shaka JWTZ wameshawasiliana na familia za marehemu maana jana msemaji wa JWTZ alisema hawawezi kutaja majina ya marehemu mpaka wawasiliane na familia zao kwanza.
 
Back
Top Bottom