Vifahamu vyeo vya askari polisi wa Tanzania na alama zake

GAZETI

JF-Expert Member
Feb 24, 2011
5,278
6,636
Kwa anayefahamu naomba msaada wa kujua ngazi ya vyeo vya polisi

Kwa mfano Inspekta ni yepi majukumu yake na anatambuliwa kwa nyota

au alama gani, Sajenti, Konstebo, Koplo n.k


Kwa faida yako sio unamwangalia kova alafu ujui yeye ni mtu wa ngapi kutoka kwenye renk za juu.
View attachment 91476

Inspekta Jenerali wa Polisi(IGP)

Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi(DIGP)

Kamishina wa Polisi(CP)

Naibu Kamishina wa Polisi(DCP)

Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi(SACP)

Kamishina Msaidizi wa Polisi(ACP)

Mrakibu Msaidizi Mwandamizi wa Polisi(SSP)

Mrakibu wa Polisi(SP)

Mrakibu Msaidizi wa Polisi(ASP)

Mkaguzi wa Polisi(Insp)

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi(A/Insp)

Sajini Meja wa polisi(rsm)

Stesheni Sajini wa Polisi(s/sgt)

Sajini wa Polisi(sgt)

Koplo wa Polisi(cpl)

Konstebo wa Polisi(pc)

8a8d151a0886ff4dcc25a1fe08d794d4.jpg
65386ba81990412e2647fdab84f15860.jpg
31a05dbc14896eb32d694a9fb68d51ca.jpg


Zaidi, soma:

Vyeo vya Jeshi la Polisi Tanzania kwa protocol
 
Kwa anayefahamu naomba msaada wa kujua ngazi ya vyeo vya polisi
Kwa mfano Inspekta ni yepi majukumu yake na anatambuliwa kwa nyota
au alama gani, Sajenti, Konstebo, Koplo n.k
Kama ni jeshi la polisi la Tanzania, basi angalia wikipedia, kwenye ukurasa wa police rank in UK, maana sisi ndio tumerithi uko.
 
Vipo vya kiutawala na vya kijeshi weye wataka vipi?.......mathalan IGP ni cha kiutawala wakati kijeshi ni kamishna wa polisi (CP)

Kijeshi
Commissioner of Police
Deputy Commissioner of Police
Senior Assistant Commissioner of Police
Assistant Commisisoner of Police
Senior Superintendent of Police
Superintendent of Police
Assistant Superintendent of Police
Inspector
Staff Sergeant
Sergeant
Corporal
Lance Corporal
Police Constable
 
Vipo vya kiutawala na vya kijeshi weye wataka vipi?.......mathalan IGP ni cha kiutawala wakati kijeshi ni kamishna wa polisi (CP)

Kijeshi
Commissioner of Police
Deputy Commissioner of Police
Senior Assistant Commissioner of Police
Assistant Commisisoner of Police
Senior Superintendent of Police
Superintendent of Police
Assistant Superintendent of Police

Inspector
Staff Sergeant
Sergeant
Corporal
Lance Corporal
Police Constable
Hapo umechanganya kidogo nadhani...
 
Hapo umechanganya kidogo nadhani...

Hapana shem,

Senior Superintendent of Police (SSP) hawa mara nyingi huwa ni OCDs,OCD/CIDs na nadra huwa RPCs
Superintendent of Police(SP)hawa mara nyingi huwa ni OCDs,OCD/CIDs
Assistant Superintendent of Police(ASP)hawa mara nyingi huwa ni OCSs
 
Ndata

Mwera

Kuruta

Njagu

TiGo

Nyigu

Afande Kidekeo

Mlinzi

Kachero Hadji

Ispekta Fogu

Mpelelezi

Usalama wa Taifa

Askari Kanzu

Fanya Fujo Uone

Nimeipenda hii,
Vipi Sajent Kitowela???
 
Naomba nielimishe hivi vyeo vya kiutawala zinakwendaje....maana kwingine nakuta OCD ndio mkuu wa kitua, na kwingine nakuta OCS etc.
 
Naomba nielimishe hivi vyeo vya kiutawala zinakwendaje....maana kwingine nakuta OCD ndio mkuu wa kitua, na kwingine nakuta OCS etc.

OCD hawezi kuwa mkuu wa kituo bali anaweza kuwa na ofisi ndani ya kituo. Mathalan Oysterbay Police Station pana OCS na OCD wa kinodnoni na ofisi pale....na RPC wa mkoa maalum nae yuko pale pia
 
Kwa Tanzania cheo cha juu ni IGP, Akifuatiwa na Makamishina, Halafu kuna madeputies. Then kuna Senior Assistant Commisioners.
 
Halafu ACP, SSP, SP,ASP, Inspector, Assistant Inspector, Rsm, Staff Sergent, Sergent na Koplo. Kama sijasaahu.
 
Hapana shem,

Senior Superintendent of Police (SSP) hawa mara nyingi huwa ni OCDs,OCD/CIDs na nadra huwa RPCs
Superintendent of Police(SP)hawa mara nyingi huwa ni OCDs,OCD/CIDs
Assistant Superintendent of Police(ASP)hawa mara nyingi huwa ni OCSs
Sawa lakini pia utegemeana na hadhi ya Kituo/Wilaya.
 
Kwa anayefahamu naomba msaada wa kujua ngazi ya vyeo vya polisi
Kwa mfano Inspekta ni yepi majukumu yake na anatambuliwa kwa nyota
au alama gani, Sajenti, Konstebo, Koplo n.k
Mkuu namjibu hapo kwenye nyekundu,
Unachnaganya.......hebu soma thread toka mwanzo....IGP,RPC,OCD na OCS ni vyeo vya kiutawala
Kuna Ngazi na majukumu, kwanza unapanda ngazi halafu unapewa majukumu kulingana na ngazi uliyonayo.
 
Camaraderie ameruka assistant inspector. Vinginevyo yupo sahihi kabisa.
Ni kweli ila cheo cha lens Corporal Hakuna Polisi. Halafu kuna RSM zamani walikuwa masajenti meja, lakini kwa sasa anakuwa mmoja tu katika kikosi.
 
Ni kweli ila cheo cha lens Corporal Hakuna Polisi. Halafu kuna RSM zamani walikuwa masajenti meja, lakini kwa sasa anakuwa mmoja tu katika kikosi.

Polisi hakuna RSM (Regimental Sergeant Major) kwa kuwa hakuna police regiment bali ni constabulary......Lance Corporal wapo
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom