Nungunungu
JF-Expert Member
- Feb 13, 2007
- 311
- 13
Kigoma mjini wapinzani hawapati
Kweli mkuu hili jimbo kalisahau hali ya CCM kule Mbeya ni ya kukatisha tamaa maana Chadema wanakunywa mpaka uji wa mgonjwaMbona mbeya mjini hujaliweka?
Mpesya anapumulia mashine kule
Red alert:Majimbo yote ya Dar, Siha ni baadhi tu ya majimbo ambayo huenda yakaangukia Chadema. Huko Siha kuna Injinia mmoja anaitwa Humphrey Tuni nasikia amemkalia pabaya Mhe. Aggrey Mwanri ila siwezi kuthibitisha maana huko sijafika taarifa hizo ni "hearsay"
jimbo la chalinze,bagamoyo,muheza,handeni, monduli,bagamoyo,lushoto,mwanga, same mashariki&magharibi,chamwino,dodoma mjini,simanjiro,rungwe mashariki&magharibi,kyela aaaaaaahhh jamani mbona yapo mengi mmeshindwa kuyataja?Wee kweli ni fanfa, yaani umeacha majimbo kibao kwa mfano anakotoka makamu mwenyekiti wa CHADEMA Mh. S. Arfi au humfahamu??? Sumbawanga mjini, Mbozi, Mbeya mjini, Kawe, na orodha inaendelea....
Nashukuru kwa kunisamehe. Sina maana kuwa ndo majimbo pekee bali kulingana na tathimini tuliyofanya. Tunahitaji tathimini kutoka kila pembe ya nchi na kazi hii huwezi fanya mtu mmoja au wawili. Hivyo naomba utujuze kwa yale ambayo hatujapata tathimini halisi.
Ninaafiki na hiyo tathmini kwa asilimia sitini hivi. Hesabu zangu zinaweka majimbo 81 kuwa yanaelekea Chadema na mengineyo 26 ni "too close to call"
Majimbo yote ya Dar, Siha ni baadhi tu ya majimbo ambayo huenda yakaangukia Chadema. Huko Siha kuna Injinia mmoja anaitwa Humphrey Tuni nasikia amemkalia pabaya Mhe. Aggrey Mwanri ila siwezi kuthibitisha maana huko sijafika taarifa hizo ni "hearsay"
Jimbo la 18. Ngorongoro sina uhakika kwa sababu taarifa nilizonazo mgombea wa Chadema pamoja alikuwa ni mbunge wa zamani wa hapo katika miaka ya 1985- 1990 Bw. Parkipuny wanasema hakubaliki sana wakidai kutokana na silika yake ambayo siwezi kuiandika humu kwa sababu ni hisia tu. Hata hivyo Parkipuny is very strong ukilinganisha na huyo mpinzani wake wa CCM ambaye anashutumiwa kwa kutotetea Mwarabu mwindaji kuondolewa Loliondo. Parkipuny anakumbukwa kwa kumwondoa Ole Saibul (marehemu sasa) kwa kile kilchoitwa kuwatekeleza wamasai wa ngorongoro. Hiyo "is a hot button campaign issue" kwenye tarafa ya ngorongoro ambako serikali imekusudia kuondoa kilimo cha bustani kwenye mbuga ya hifadhi. Wagombea wote wawili "they are busy assigning blame on the matter rather than assuming responsibility."
Yule mgombea wa CCM hapo Ngorongoro anaitwa Saningo Telele (an immediate) MP hakubaliki sana haswa kwenye kata yake ya ngorongoro wanadai he is " too snobbish and too weak" Kama hilo linatosha kumsarambatisha tutajua baada ya D-Day. Na huyu Parkipuny kama akiweza kuwashawishi kata ya Ngorongoro basi jimbo limekwenda Chadema maana huko kwenye kata nyinginezo "it is anybody's game"
Taadhari isije ikawa kama tasmini ya mwaka 2005 kusema upinzania utapata majimbo 100, na kuzomwea kote kina Hawa Ghasia na Makweta mwisho wake wakaja kushinda, naomba tusidanganyike na wingi wa watu kwenye mikutano ina bidii tuwahamasishe wajitokezo hiyo siku ya kupiga kura na wajitahidi kuzilinda ndio ushindi ytapatikana
Ahsante sana kwa kumtakia mema mtoto wa watu, najua unaonge kinyume!
WildCard Mkuu umenena CCM ni Mafia wa wizi wa kura!Hamuwafahamu CCM kwenye ballot box. Muulize Dr Mvungi aliyegombea Urais kwa tiketi ya NCCR mwaka ule. Hakuiona hata kura aloojipigia yeye mwenyewe pale Chuo.
Mimi huwa sihesabu vifaranga kwa kuangalia idadi ya mayai... napenda zaidi kulinda hayo mayai ili yaanguliwe yote... kwa kuhesabu vifaranga na tuna mwezi mzima wa kampeni ni ngumu sana
Cha maana ni kuendeleza kampeni ili mbunge sahihi (bila kujali chama) ashinde
hivi wanaoshabikia ccm ni watanzania?