Felixonfellix
JF-Expert Member
- Feb 16, 2010
- 1,672
- 182
Katika jimbo fulani kuna bango linalomnadi mbunge wa sehemu hiyo hivi: Baadhi ya misaada mbalimbali niliyotoa kwa wanajimbo langu binafsi:
- Nilisaidia upatikanaji wa majeneza pamoja na kusafirisha marehemu toka wilaya yangu waliopata ajali ya treni huko Dodoma na kushughulikia majeruhi kwa kuwawahisha hospitali ili kupata matibabu ya haraka.
- Nilifanikisha uletwaji wa mwili wa marehemu Mathias Kasoso toka Dar es Salaam. Nilisaidia sana uwezekano wa usafiri wa ndege pamoja na usafiri wa gari wa kutoka uwanja wa ndege kwenda alikozikwa.
- Nilitoa baiskeli kwa mlemavu wa .... yenye thamani ya Tsh. 60,000 na Sh. 00,000 kumnunulia mlemavu mwingine baiskeli ya gurudumu tatu.
- Nilimsaidia Mama mtu mzima kupata haki zake Dodoma zilizokuwa hatarini kupotea bure
- Nilimsaidia Salehe na rafiki yake (Sh. 40,000) nauli ya kutoka Dar es Salaam. Walikuwa wamekwama Dar es Salaam.
- Niliwasafirisha vijana wawili kutoka jimboni mwangu waliokwama Dar baada ya kudanganywa waende Dar es salaam wangepatiwa ajira.