Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Majibu ya JK yamekwepa hoja!http://www.majira.co.tz/index.php?v...hoja-&format=pdf&option=com_content&Itemid=57 http://www.majira.co.tz/index.php?v...nt&print=1&page=&option=com_content&Itemid=57 http://www.majira.co.tz/index.php?o...ob2phLSZvcHRpb249Y29tX2NvbnRlbnQmSXRlbWlkPTU3 Thursday, 10 September 2009 17:14 *Beregu: Yalikuwa mepesi hayakukidhi haja za wananchi
*Aonesha wasiwasi baadhi ya maswali kuandaliwa
*Shekhe Issa: Napongeza Rais kukemea tishio la udini
*Hamad Rashid apongeza utaratibu wa papo kwa papo lakini...
*Slaa atetea waraka, Lipumba alia muafaka, Mrema apongeza
Na Waandishi wetu
BAADHI ya maswali aliyoulizwa Rais Jakaya Kikwete jana kwenye utaratibu mpya wa'Muulize Rais'kwa kupiga simu, kutuma barua pepe na kujibiwa moja kwa moja kupitia redio na televisheni hayakupata ufafanuzi wa kina kulingana na uzito wa masuala husika, kama ilivyotarajiwa na wengi, imedaiwa.
Masuala yanayodaiwa Rais hakuyatoa majibu fasaha ni pamoja na vita dhidi ya ufisadi, safari zake za nje na nyaraka zinazotolewa taasisi za dini, ambapo imedaiwa majibu yake yalikuwa mepesi na hayakukidhi haja ya wananchi.
Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (CKD), Profesa Mwesiga Baregu aliliambia gazeti hili jana kuwa wananchi wengi waliondoka na kiu kubwa ya majibu kutokana na maswali mengi aliyoulizwa Rais Kikwete kutofafanuliwa kwa kina.
Prof. Baregu ambaye ni mtaaluma wa masuala ya Sayansi ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, alisema majibu aliyotoa Rais Kikwete juu ya vita dhidi ya ufisadi hayalingani na uzito wa jambo hilo ambalo limechukua sehemu kubwa ya mijadala nchini takribani kipindi chote cha utawala wake.
"Suala la ufisadi hakulitolea majibu ya kuridhisha kulingana na uzito wake unavyostahili, mpaka sasa ni moja ya mambo ambayo yametuchukulia muda mrefu katika kuyajadili bila kupata majibu sahihi.
"Alizungumzia TAKUKURU tu kwa muda mrefu lakini ninavyojua mimi chombo hicho pia kiliwahi kutuhumiwa katika vita dhidi ya rushwa kuwa kinasafisha watu na hakifanyi kazi yake sawasawa, sidhani kama kuongelea chombo hicho pekee ilikuwa ndio jibu sahihi la swali lile juu ya vita vya ufisadi," alisema Prof. Baregu.
Akizungumzia safari za mara kwa mara ambazo Rais Kikwete amekuwa akizifanya nje ya nchi, Prof. Baregu, alisema huenda Rais hakuelewa mantiki ya muuliza swali hivyo kujikuta akijibu tofauti.
Alisema mantiki ya swali lile lilikuwa ni kutaka kujua umuhimu wa safari hizo ambapo muda mwingi Rais Kikwete amekuwa akitumia kuzunguka kuomba misaada kwa nchi tajiri kuisaidia Tanzania, badala ya 'kuiuza' nchi kwa kutumia maliasili zilizopo na kutafuta wawekezaji makini wanaoweza kusaidiana na serikali kuziendeleza.
"Swali lile nahisi lilimpiga chenga, safari zake hizo za nje badala ya kutuingizia nafikiri zimekuwa zikitu-cost (kutugharimu) zaidi, badala ya kutumia fursa hiyo kutambulisha rasilimali zetu ziendelezwe ili zitusaidie wananchi wote, amekuwa akienda kuomba misaada.
"Mbali ya kuwa unapoomba unajinyima uwezo wa kujitegemea, lakini pia hakuna nchi itakupatia kitu bure, hivyo swali halikueleweka, tutaendelea kuomba omba mpaka lini?" alihoji Prof. Baregu.
Huku akionekana kuwa na wasiwasi na utaratibu uliotumika kuwasiliana na Rais, akisema kuwa inawezekana baadhi ya maswali yalikuwa yameandaliwa mapema, Prof. Baregu alisema suala la nyaraka za taasisi za dini nalo pia halikupata majibu muafaka.
Alisema haoni mantiki ya majibu ya Rais Kikwete kuwa nyaraka hizo (waraka na Ilani ya Wakatoliki na Mwongozo wa Waislamu) zitaleta mgawanyo miongoni mwa wanajamii.
"Nafikiri nyaraka hizo kwa jinsi nilivyozisoma na kuzielewa zililenga kupata viongozi waadilifu, na kwa hakika viongozi wa dini wana wajibu wao katika jamii kuhakikisha kuwa maadili yanakuwepo, sasa vipi zilete matatizo.
"Ingawa pia viongozi wa dini walitakiwa kuunganisha nguvu zao za madai pamoja lakini kama taifa linalotaka kuwa na viongozi waadilifu basi Rais hakuwa na haja ya kuziogopa," alisema Prof. Baregu.
Kwa upande wake, Shekhe Mohamed Issa ambaye ni mwanazuoni na mchambuzi mahiri wa masuala ya dini, alisema wanashukuru kuwa hatimaye Rais Kikwete amezungumzia masuala hayo baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu.
Shekhe Issa, alisema Rais anastahili kupongezwa kwa hatua hiyo ya kuzungumzia hatari ambayo taifa linanyemelewa kwa kusukwasukwa na mambo ya kidini, lakini akahoji kwa nini hatua hiyo imekuja baada ya Waislam kutoa mwongozo wao?
"Waraka wa Wakatoliki umetolewa karibu miezi tisa nyuma, tunaamini kabisa Rais Kikwete alijua kwa kutumia njia zake za kupata habari, anajua mambo ya waraka toka Januari, lakini alikaa kimya.
"Lakini mara zote katika nchi hii hatari imekuwa inaonekana pale waislam wanapoamua ku-react (kujibu) katika msuala yao, hapo ndipo watu huanza kusema kuna hatari na hali hii imekuwepo toka awamu ya kwanza ya utawala wa nchi hii," alidai mwanazuoni huyo.
Akizungumzia kuhusu Waraka na Mwongozo, alisema kuwa kimsingi demokrasia inahusisha mambo mengi ikiwemo kusikiliza na kusimamia maoni yanayotolewa na makundi ya kijamii.
Alisema hakuna tatizo kwa makundi mbalimbali ya kijamii kama yale ya kidini, walemavu, wawindaji na mengine kutoa maoni na malalamiko yao kupigania haki au stahili yao, lakini itakuwa vibaya tu endapo kundi moja litatoa maelekezo ya kukandamiza maslahi ya makundi mengine.
"Mfano watu wenye ulemavu wa ngozi, wenye virusi vya UKIMWI, Wahadzabe wote wanahaki ya kutoa maoni yao jinsi wanavyohitaji kutimiziwa stahili zao ilmradi tu, wasikandamize maslahi ya makundi mengine.
"Hivyo hakukuwa na makosa kwa watu wa dini kutoa utashi wao kwa serikali au vyama vya siasa kuvionesha namna gani wanapaswa watendewe, ikiwa ni mojawapo ya michakato ya demokrasia.
"Ilani ya Wakatoliki na Mwongozo wetu haina shida, labda tatizo liko kwa ule Waraka wa Kichungaji ambao umeweka mambo ya kidini zaidi, hivyo sisi tunasisitiza tutamchagua yeyote yule bila kujali dini ilimradi atimize haki zetu za msingi," alisema.
Naye Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Bw. Hamad Rashid Mohamed amesema mbali na kuridhishwa na utaratibu mpya wa Rais Jakaya Kikwete kujibu maswali ya wananchi papo kwa papo kupitia vyombo vya habari amesikitishwa na kiongozi huyo kuwa kigeugeu katika suala la muafaka wa kisiasa visiwani Zanzibar.
Bw. Hamad alidai Rais Kikwete ndiye kikwazo kikubwa cha kupatikana muafaka visiwani Zanzibar kwani wakati akilihutubia Bunge alisema kuwa ajenda zote tano zilizokuwa zinazungumziwa baina ya CCM na CUF zimemalizika lakini baadaye alikuja na ajenda ya sita ya kupigakura ya maoni kwa wananchi.
"Rais Kikwete ni mwepesi wa kujua matatizo yanayojitokeza katika jamii lakini ni mzito wa kutoa majibu jambo ambalo ni hatari sana hasa kwa suala kama la muafaka visiwani zanzibar," alisema Bw. Rashid.
Alidai kuwa vyama vyote katika vikao vyake vilikubaliana kwa pamoja mambo yote yaliyokuwamo kwenye ajenda tano ambazo walijiwekea lakini cha kushangaza wakati wakielekea mwisho, Rais akaja na ajenda ya sita ya kupigakura za maoni kitendo ambacho hakiwezi kuleta suluhu kutokana na udhaifu uliopo kwenye chaguzi zote.
"Huwezi kuwa na 'double conflict' kwamba mazungumzo yamemalizika lakini unakuja na ajenda nyingine ya kura za maoni kwa madai kuwa kuna mabadiliko makubwa ya Katiba na utendaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar," alisema na kuongeza kuwa shughuli ya uchaguzi Zanzibar haiaminiki kwa nini ulete kura ya maoni?
Alisema dosari hiyo inaweza kuigharimu Zanzibar kwani wakatijitihada za muafaka zinaanza, aliahidi kufanyika kwa wiki tatu lakini cha kushangaza imechukua zaidi ya wiki 18 bila ufumbuzi.
Naye Mbunge wa Karatu, Dkt. Wilbroad Slaa (CHADEMA) alisema Rais Kikwete amepotosha kuhusu waraka uliotolewa na Kanisa Katoliki kuelimisha wanaumini wao namna ya kuchagua viongozi kwenye uchaguzi mkuu ujao mwakani kwa kueleza kuwa una hatari kwa mustakabali wa Taifa.
Dkt. Slaa ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CHADEMA, alidai Rais Kikwete alipaswa kusoma vizuri waraka huo na kuuelewa.
"Rais alitakiwa kuusoma vizuri waraka huo kabla hajalizungumzia suala hilo mbele ya wananchi ambao wengi wa waliousoma, wameonesha kuukubali,"alisema.
Alisema Rais Kikwete alipaswa kuwapongeza wanataaluma Wakatoliki kwa kundaa waraka huo kwani unalenga kutoa elimu kwa watanzania hususan katika kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu.
"Nitamshangaa mtu yeyote anayepinga waraka huu kwani haufundishi kuchagua kiongozi kutokana na dhehebu au dini anayotoka bali unafundisha jinsi ya kumpata kiongozi asiyejihusisha na rushwa na ubinafsi," alisema Dkt Slaa.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, alisema chama chake hakikuridhishwa na majibu ya Rais Kikwete kwani alipaswa kuelezea undani wa suala la muafaka wa CCM na CUF lakini hakufanya hivyo.
"Kwa kweli majibu aliyotoa hayajatufurahisha ... tumemwandikia barua zaidi ya nne kuhusu jambo hilo lakini hadi sasa hakuna hata moja iliyojibiwa," alisema Prof. Lipumba.
Kuhusu waraka wa Kanisa Katoliki, Prof. Lipumba, alisema wameshangazwa majibu ya Rais Kikwete kwani pamoja na malalamiko yote vipo vipengele umuhimu vyenye manufaa makubwa.
Akizungumzia ahadi ya Maisha Bora kwa kila Mtanzania kama Ilani ya Chama Cha Mapinduzi inavyoeleza, Prof. Lipumba alisema hali ya maisha inazidi kuwa ngumu siku hadi siku.
Alisema, Rais Kikwete anakosea kutumia kigezo cha huduma za jamii kama afya na elimu kwani idadi ya vifo vya kina mama wajawazito na watoto inaongezeka siku hadi siku.
Mwenyekiti wa Tanzania Labour (TLP) Bw. Augustino Mrema alisema kuwa, ufisadi uliokithiri nchini ndicho chanzo cha nyaraka zinazotolewa na madhehebu kwani watu wamechoshwa na hali hiyo.
Alisema wananchi wamechoshwa kuona watu wachache wanafaidi rasilimali za umma na wengine wakiumia kwa umasikini wa kutisha.
Hata hivyo, Bw. Mrema alimpongeza Rais Kikwete kwa jitihada zake za kupambana na mafisadi kwa kuwa ndiye rais wa kwanza kushughulikia kero hiyo na kumshauri kuongeza nguvu zaidi.Source: http://www.majira.co.tz/index.php?o...epa-hoja-&catid=34:kitaifa-tanzania&Itemid=57
*Aonesha wasiwasi baadhi ya maswali kuandaliwa
*Shekhe Issa: Napongeza Rais kukemea tishio la udini
*Hamad Rashid apongeza utaratibu wa papo kwa papo lakini...
*Slaa atetea waraka, Lipumba alia muafaka, Mrema apongeza
Na Waandishi wetu
BAADHI ya maswali aliyoulizwa Rais Jakaya Kikwete jana kwenye utaratibu mpya wa'Muulize Rais'kwa kupiga simu, kutuma barua pepe na kujibiwa moja kwa moja kupitia redio na televisheni hayakupata ufafanuzi wa kina kulingana na uzito wa masuala husika, kama ilivyotarajiwa na wengi, imedaiwa.
Masuala yanayodaiwa Rais hakuyatoa majibu fasaha ni pamoja na vita dhidi ya ufisadi, safari zake za nje na nyaraka zinazotolewa taasisi za dini, ambapo imedaiwa majibu yake yalikuwa mepesi na hayakukidhi haja ya wananchi.
Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (CKD), Profesa Mwesiga Baregu aliliambia gazeti hili jana kuwa wananchi wengi waliondoka na kiu kubwa ya majibu kutokana na maswali mengi aliyoulizwa Rais Kikwete kutofafanuliwa kwa kina.
Prof. Baregu ambaye ni mtaaluma wa masuala ya Sayansi ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, alisema majibu aliyotoa Rais Kikwete juu ya vita dhidi ya ufisadi hayalingani na uzito wa jambo hilo ambalo limechukua sehemu kubwa ya mijadala nchini takribani kipindi chote cha utawala wake.
"Suala la ufisadi hakulitolea majibu ya kuridhisha kulingana na uzito wake unavyostahili, mpaka sasa ni moja ya mambo ambayo yametuchukulia muda mrefu katika kuyajadili bila kupata majibu sahihi.
"Alizungumzia TAKUKURU tu kwa muda mrefu lakini ninavyojua mimi chombo hicho pia kiliwahi kutuhumiwa katika vita dhidi ya rushwa kuwa kinasafisha watu na hakifanyi kazi yake sawasawa, sidhani kama kuongelea chombo hicho pekee ilikuwa ndio jibu sahihi la swali lile juu ya vita vya ufisadi," alisema Prof. Baregu.
Akizungumzia safari za mara kwa mara ambazo Rais Kikwete amekuwa akizifanya nje ya nchi, Prof. Baregu, alisema huenda Rais hakuelewa mantiki ya muuliza swali hivyo kujikuta akijibu tofauti.
Alisema mantiki ya swali lile lilikuwa ni kutaka kujua umuhimu wa safari hizo ambapo muda mwingi Rais Kikwete amekuwa akitumia kuzunguka kuomba misaada kwa nchi tajiri kuisaidia Tanzania, badala ya 'kuiuza' nchi kwa kutumia maliasili zilizopo na kutafuta wawekezaji makini wanaoweza kusaidiana na serikali kuziendeleza.
"Swali lile nahisi lilimpiga chenga, safari zake hizo za nje badala ya kutuingizia nafikiri zimekuwa zikitu-cost (kutugharimu) zaidi, badala ya kutumia fursa hiyo kutambulisha rasilimali zetu ziendelezwe ili zitusaidie wananchi wote, amekuwa akienda kuomba misaada.
"Mbali ya kuwa unapoomba unajinyima uwezo wa kujitegemea, lakini pia hakuna nchi itakupatia kitu bure, hivyo swali halikueleweka, tutaendelea kuomba omba mpaka lini?" alihoji Prof. Baregu.
Huku akionekana kuwa na wasiwasi na utaratibu uliotumika kuwasiliana na Rais, akisema kuwa inawezekana baadhi ya maswali yalikuwa yameandaliwa mapema, Prof. Baregu alisema suala la nyaraka za taasisi za dini nalo pia halikupata majibu muafaka.
Alisema haoni mantiki ya majibu ya Rais Kikwete kuwa nyaraka hizo (waraka na Ilani ya Wakatoliki na Mwongozo wa Waislamu) zitaleta mgawanyo miongoni mwa wanajamii.
"Nafikiri nyaraka hizo kwa jinsi nilivyozisoma na kuzielewa zililenga kupata viongozi waadilifu, na kwa hakika viongozi wa dini wana wajibu wao katika jamii kuhakikisha kuwa maadili yanakuwepo, sasa vipi zilete matatizo.
"Ingawa pia viongozi wa dini walitakiwa kuunganisha nguvu zao za madai pamoja lakini kama taifa linalotaka kuwa na viongozi waadilifu basi Rais hakuwa na haja ya kuziogopa," alisema Prof. Baregu.
Kwa upande wake, Shekhe Mohamed Issa ambaye ni mwanazuoni na mchambuzi mahiri wa masuala ya dini, alisema wanashukuru kuwa hatimaye Rais Kikwete amezungumzia masuala hayo baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu.
Shekhe Issa, alisema Rais anastahili kupongezwa kwa hatua hiyo ya kuzungumzia hatari ambayo taifa linanyemelewa kwa kusukwasukwa na mambo ya kidini, lakini akahoji kwa nini hatua hiyo imekuja baada ya Waislam kutoa mwongozo wao?
"Waraka wa Wakatoliki umetolewa karibu miezi tisa nyuma, tunaamini kabisa Rais Kikwete alijua kwa kutumia njia zake za kupata habari, anajua mambo ya waraka toka Januari, lakini alikaa kimya.
"Lakini mara zote katika nchi hii hatari imekuwa inaonekana pale waislam wanapoamua ku-react (kujibu) katika msuala yao, hapo ndipo watu huanza kusema kuna hatari na hali hii imekuwepo toka awamu ya kwanza ya utawala wa nchi hii," alidai mwanazuoni huyo.
Akizungumzia kuhusu Waraka na Mwongozo, alisema kuwa kimsingi demokrasia inahusisha mambo mengi ikiwemo kusikiliza na kusimamia maoni yanayotolewa na makundi ya kijamii.
Alisema hakuna tatizo kwa makundi mbalimbali ya kijamii kama yale ya kidini, walemavu, wawindaji na mengine kutoa maoni na malalamiko yao kupigania haki au stahili yao, lakini itakuwa vibaya tu endapo kundi moja litatoa maelekezo ya kukandamiza maslahi ya makundi mengine.
"Mfano watu wenye ulemavu wa ngozi, wenye virusi vya UKIMWI, Wahadzabe wote wanahaki ya kutoa maoni yao jinsi wanavyohitaji kutimiziwa stahili zao ilmradi tu, wasikandamize maslahi ya makundi mengine.
"Hivyo hakukuwa na makosa kwa watu wa dini kutoa utashi wao kwa serikali au vyama vya siasa kuvionesha namna gani wanapaswa watendewe, ikiwa ni mojawapo ya michakato ya demokrasia.
"Ilani ya Wakatoliki na Mwongozo wetu haina shida, labda tatizo liko kwa ule Waraka wa Kichungaji ambao umeweka mambo ya kidini zaidi, hivyo sisi tunasisitiza tutamchagua yeyote yule bila kujali dini ilimradi atimize haki zetu za msingi," alisema.
Naye Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Bw. Hamad Rashid Mohamed amesema mbali na kuridhishwa na utaratibu mpya wa Rais Jakaya Kikwete kujibu maswali ya wananchi papo kwa papo kupitia vyombo vya habari amesikitishwa na kiongozi huyo kuwa kigeugeu katika suala la muafaka wa kisiasa visiwani Zanzibar.
Bw. Hamad alidai Rais Kikwete ndiye kikwazo kikubwa cha kupatikana muafaka visiwani Zanzibar kwani wakati akilihutubia Bunge alisema kuwa ajenda zote tano zilizokuwa zinazungumziwa baina ya CCM na CUF zimemalizika lakini baadaye alikuja na ajenda ya sita ya kupigakura ya maoni kwa wananchi.
"Rais Kikwete ni mwepesi wa kujua matatizo yanayojitokeza katika jamii lakini ni mzito wa kutoa majibu jambo ambalo ni hatari sana hasa kwa suala kama la muafaka visiwani zanzibar," alisema Bw. Rashid.
Alidai kuwa vyama vyote katika vikao vyake vilikubaliana kwa pamoja mambo yote yaliyokuwamo kwenye ajenda tano ambazo walijiwekea lakini cha kushangaza wakati wakielekea mwisho, Rais akaja na ajenda ya sita ya kupigakura za maoni kitendo ambacho hakiwezi kuleta suluhu kutokana na udhaifu uliopo kwenye chaguzi zote.
"Huwezi kuwa na 'double conflict' kwamba mazungumzo yamemalizika lakini unakuja na ajenda nyingine ya kura za maoni kwa madai kuwa kuna mabadiliko makubwa ya Katiba na utendaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar," alisema na kuongeza kuwa shughuli ya uchaguzi Zanzibar haiaminiki kwa nini ulete kura ya maoni?
Alisema dosari hiyo inaweza kuigharimu Zanzibar kwani wakatijitihada za muafaka zinaanza, aliahidi kufanyika kwa wiki tatu lakini cha kushangaza imechukua zaidi ya wiki 18 bila ufumbuzi.
Naye Mbunge wa Karatu, Dkt. Wilbroad Slaa (CHADEMA) alisema Rais Kikwete amepotosha kuhusu waraka uliotolewa na Kanisa Katoliki kuelimisha wanaumini wao namna ya kuchagua viongozi kwenye uchaguzi mkuu ujao mwakani kwa kueleza kuwa una hatari kwa mustakabali wa Taifa.
Dkt. Slaa ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CHADEMA, alidai Rais Kikwete alipaswa kusoma vizuri waraka huo na kuuelewa.
"Rais alitakiwa kuusoma vizuri waraka huo kabla hajalizungumzia suala hilo mbele ya wananchi ambao wengi wa waliousoma, wameonesha kuukubali,"alisema.
Alisema Rais Kikwete alipaswa kuwapongeza wanataaluma Wakatoliki kwa kundaa waraka huo kwani unalenga kutoa elimu kwa watanzania hususan katika kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu.
"Nitamshangaa mtu yeyote anayepinga waraka huu kwani haufundishi kuchagua kiongozi kutokana na dhehebu au dini anayotoka bali unafundisha jinsi ya kumpata kiongozi asiyejihusisha na rushwa na ubinafsi," alisema Dkt Slaa.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, alisema chama chake hakikuridhishwa na majibu ya Rais Kikwete kwani alipaswa kuelezea undani wa suala la muafaka wa CCM na CUF lakini hakufanya hivyo.
"Kwa kweli majibu aliyotoa hayajatufurahisha ... tumemwandikia barua zaidi ya nne kuhusu jambo hilo lakini hadi sasa hakuna hata moja iliyojibiwa," alisema Prof. Lipumba.
Kuhusu waraka wa Kanisa Katoliki, Prof. Lipumba, alisema wameshangazwa majibu ya Rais Kikwete kwani pamoja na malalamiko yote vipo vipengele umuhimu vyenye manufaa makubwa.
Akizungumzia ahadi ya Maisha Bora kwa kila Mtanzania kama Ilani ya Chama Cha Mapinduzi inavyoeleza, Prof. Lipumba alisema hali ya maisha inazidi kuwa ngumu siku hadi siku.
Alisema, Rais Kikwete anakosea kutumia kigezo cha huduma za jamii kama afya na elimu kwani idadi ya vifo vya kina mama wajawazito na watoto inaongezeka siku hadi siku.
Mwenyekiti wa Tanzania Labour (TLP) Bw. Augustino Mrema alisema kuwa, ufisadi uliokithiri nchini ndicho chanzo cha nyaraka zinazotolewa na madhehebu kwani watu wamechoshwa na hali hiyo.
Alisema wananchi wamechoshwa kuona watu wachache wanafaidi rasilimali za umma na wengine wakiumia kwa umasikini wa kutisha.
Hata hivyo, Bw. Mrema alimpongeza Rais Kikwete kwa jitihada zake za kupambana na mafisadi kwa kuwa ndiye rais wa kwanza kushughulikia kero hiyo na kumshauri kuongeza nguvu zaidi.Source: http://www.majira.co.tz/index.php?o...epa-hoja-&catid=34:kitaifa-tanzania&Itemid=57