Nimemsikiliza Dr Kawambwa waziri mwenye dhamana ya kusimamia elimu nchini kwenye serikali hii ya JK nimesikitika sana na mwisho kubaini kabisa hastahili uwaziri. Anaeleza wamelazimika kutoa maswali ya kuchagua mitihani ya masomo yote kwa sababu ya kurahisisha usahihishaji wa mitihani wakiwa na lengo la kupunguza ghalama kwani watoto wanaofanya mitihani hiyo kwa sasa ni wengi tofauti na tulipopata uhuru, sababu ya pili ni kuwahisha zoezi ili waende zao sekondari. Waziri huyu ipo siku atafuta maswali ya kujieleza hata sekondari kwa sababu hizo hizo ikiwemo kuwawahisha kuingia zao kidato cha tano, na baadae kuwawahisha vyuo vya elimu ya juu na wale wa vyuo vikuu kuwawahisha kwenye ajira. Kwani kote idadi imeongezeka ukilinganisha na kipindi baada tu ya kupata uhuru.