Majibu rasmi ya Mwanakijiji kwa Waziri Mkuu

Duh Pwida.. yaani ningepata hiyo link few days ago...ingesaidia kweli. Well.. I hope next time. Ila nashukuru I could use some information sometimes later.
 
Nikisoma makala ya mzee Mwanakijiji na jibu kutoka ofisi ya waziri mkuu, nashawishika kuamini jibu kutoka ofisi ya waziri mkuu. Kwa sababu moja ya msingi: Imeambatana na takwimu na element za utafiti. Takwimu na utafiti ni weakness kubwa ya postings za JF.

Vilevile hii hali ya kusingizia vitisho serikali inapotoa jibu la makala zetu inamomonyoa utashi wetu JF.

Mgonjwa wa Ukimwi;

"NO INVESTIGATION NO RIGHT TO SPEAK" Ben Mkapa, Nkurumah Hall, 1990's'

Mnatoa hoja mkijibiwa mwaanza kusema mnatishiwa maisha tuoeni hoja na ninyi zenye takwimu kama zilivyotolewa na Ofisi ya Waziri mkuu, au tuamini ilikuwa udaku kama ilivyokawaida ya JF?!!!

Ukitaka kuchafua tu serikali bila kuwa na hoja unatakiwa kujiunga na vyama vya siasa na katika hilo huna haja ya kujificha... unajitokeza kama Mtikila, Mrema and the like...
 
Kilitime, subiri majibu yangu mbona na wewe unakuwa kama ni mgumu kuelewa. Nikijibu ndio mje kuchambua majibu yangu na kuonesha udhaifu wake na makosa yake. Tunajadili haya ya Waziri Mkuu kwa vile wameshayatoa hadharani. Are you in a hurry?
 
Mzee Mwanakijiji,

Unajua inachekesha sana sisi waswahili kuwa wepesi kukubali vitu kwa sababu tu kuna takwimu fulani zilizojengwa na baadhi ya watu fulani...
Sidhani kama unayo haja ya kuweka utafiti wako hapa kuridhisha baadhi ya watu ambao wamependa kukubali takwimu za serikali na kuzikataa zile za Benki kuu kwa sababu ambazo hazifahamiki... Mh. Waziri mkuu kesha sema ndege inaruka!... ndege ya maendeleo yetu kama inaruka ina maana kuwa Tanzania sasa hivi kimaendeleo ipo safarini...na huwezi kurusha ndege ikiwa bado kuna dosari nyingi za kiufundi!...
Wote tunafahamu kwamba hii sii kweli hata kidogo kwa sababu maendeleo hayawezi kuja hata siku moja bila kuwepo miundombinu. Ni mapungufu ambayo serikali yenyewe imeyakubali na nadhani ktk fungu kubwa la mikopo yetu mwaka huu tumesisitizwa kujenga miundo mbinu. Hata anapozungumzia Macroeconomic fundamentals ambazo zilijengwa na Mkapa hazikuwa kwa minajiri ya kuondoa Umaskini, Ujinga ama Maradhi!..hakuna haja ya takwimu kuweza kuwakilisha swala hili kwani somo lenyewe halihusiani kabisa na vitu hivyo bali ni maandalizi ya nchi yetu kuingia ktk dunia ya Utandawazi na soko huria. Haya maandilizi yenyewe yamefanyika tukiwa tayari ndani ya ulimwengu wa Utandawazi na soko huria hali hizi macroeconomic fundamentals ni wajibu wa kila nchi ktk ku promote transparency na good governance hasa unapo jianika sokoni (international capital markets).
Kwa hiyo hadi sasa hivi hiyo ndege inayopaa sio ya kitaifa imeruka toka mbuga za migodi ambako hilo dege la Ki Canada Caribou huongoka bila abiria, kisha dege hili halikutengenezwa kwa ajili abiria bali mizigo!....Kweli mizigo inaondoka sana nchini kwa malipo ya njugu ambayo viongozi wetu wanayapigia makofi!

Mimi nadhani la muhimu hapa ni kuanzisha mada moja muhimu inayokusanya mawazo yetu kuhusu hao adui watatu yaani Umaskini, Ujinga na Maradhi!... Nini mtazamo wetu kwa sababu kila naposoma report za serikali huzidi kunipa hofu kama kweli serikali yetu inafahamu vizuri suluhisho la matatizo haya ktk mazingira yetu.
UMASKINI, UJINGA na MARADHI ni madhara ambayo tayari yameisha kuwa sugu ktk maendeleo ya wananchi. Kama nilivyosema toka huko awali ni kwamba sisi ni Wagonjwa tayari wa maradhi hayo matatu, inakuwaje leo tunatumia mbinu za nchi za magharibi ambao wao sii wagonjwa ila wanazitumia mbinu hizi kama kinga kuhakikisha hawapatwi na maradhi haya!..Chanjo za kinga hata siku moja haziwezi kuwa dawa kwa mgonjwa wa maradhi haya!
Waheshimiwa, adui zetu hawawezi kuondoka kwa kutafuta kinga ama kupunguzwa, tunachohitaji ni tiba kwa taifa zima!...Tanzania ni nchi maskini sii swala la baadhi ya watu, mikoa ama wilaya.
 
Nikisoma makala ya mzee Mwanakijiji na jibu kutoka ofisi ya waziri mkuu, nashawishika kuamini jibu kutoka ofisi ya waziri mkuu. Kwa sababu moja ya msingi: Imeambatana na takwimu na element za utafiti. Takwimu na utafiti ni weakness kubwa ya postings za JF.

Vilevile hii hali ya kusingizia vitisho serikali inapotoa jibu la makala zetu inamomonyoa utashi wetu JF.
Mgonjwa wa Ukimwi;

"NO INVESTIGATION NO RIGHT TO SPEAK" Ben Mkapa, Nkurumah Hall, 1990's'

Mnatoa hoja mkijibiwa mwaanza kusema mnatishiwa maisha tuoeni hoja na ninyi zenye takwimu kama zilivyotolewa na Ofisi ya Waziri mkuu, au tuamini ilikuwa udaku kama ilivyokawaida ya JF?!!!

Ukitaka kuchafua tu serikali bila kuwa na hoja unatakiwa kujiunga na vyama vya siasa na katika hilo huna haja ya kujificha... unajitokeza kama Mtikila, Mrema and the like...

Kwa hiyo MgonjwaUkimwi na Kilitime mmeona substance kwenye jibu la Waziri Mkuu kwa vile alitoa takwimu? Nikiwaambia kuwa takwimu alizotoa ndizo zilizozidi kuimarisha madai ya mwanakijiji mtakubali?

(1) Kwamba watanzania sasa hivi ni maskini sana kiasi kuwa mwananchi akipata Shs 1000 anaonekana kapiga hatua kubwa sana kufuta umaskini!

Waziri mkuu anadai kuwa serikali imetoa TSh 1bn kwa kila mkoa kupiga vita umaskini. Kwa mkoa wangu wa Tabora wenye idadi ya wakazi 1,717,908, kila mmoja atapata Sh 582.11 tu na hivyo kuondokana na umaskini!!. Je nawe unaamini kuwa TSh 600 kwa mwaka zinamwondolea mwananchi umaskini??

(2) Kwamba takwimu anazotoa kuhusu kilimo ni chini sana ya takwimu zilizotolewa mwaka 1975-76, yaani miaka 30 iliyopita, ambapo serikali ilitoa mbolea bure kwa wanachi wote, iliajiri mabwana shamba kwa kila kijiji Tanzania nzima, na mavuno ya chakula yalikuwa na tani millioni tano zaidi ya mahitaji ya nchi lakini sehemu kubwa ya mazao hayo ikaozea huko vijijini kwa vile hakukuwa na usafiri wa kuyawezesha kufikia sehemu nyingine za nchi ambako chakula kilikuwa kinahitajika. Kuwa Waziri mkuu angekumbushwa kuhusu ile kampeini ya "Kilimo cha Kufa na Kupona" na atuambie takwimu zake zinaingia wapi katika kampeini hiyo. Kama "Kilimo cha Kufa na Kupona" hatukusema ndege inaruka je yeye kaitoa wapi ndege hiyo?

(3)Kwamba kuongezeka kwa shule za sekondari 1,090 katika mwaka mmoja bila kusema ameongeza waalimu wangapi wa sekondari ni kudanganya umma. Shule siyo idadi ya wanafunzi waliowekwa kwenye majengo yasiyo kuwa na milango wala madirisha bila mwalimu. Lazima atuambie ameajiri waalimu wangapi ambao ni qualified kufundisha watoto wale na wana vifaa vya kufundisha. Kujibu swali hili sawasawa, tutahitaji statistics ambazo kwa bahati mbaya serikali haijazitoa, hata hivyo ninapenda kuangalia madai hayo kwa kuangalia statistics za mwaka 2005- 2006, halafu nitatumia bajeti ya 2005-2006-2007 kujibu madai hayo.

Mwaka 2005 kulikuwa na shule za sekondari za serikali 1,202 zikiwa na waalimu 11,313, mwaka 2006 kulikuwa na shule za sekondari 1,690 zenye waalimu 15,911, kwa hiyo kwa wastani kila shule ilikuwa na waalimu 29 katika miaka yote miwili. Ongezeko la shule lilikuwa asilimia 41 na ongezeko la waalimu pia lilikuwa asilimia 41. Hata hivyo, naomba nitahadharishe kuwa asilimia 13 ya waalimu kwa mwaka 2006 walikuwa ni wale wa grade A, B na C, wakati asilimia yao kwa mwaka wa 2005 ilikuwa ni 5 tu, kwa hiyo kuna ongezeko la haraka kwa waalimu wa grade hizi kutumika katika kufundisha sekondari (Nadhani wenzangu mnajua qualifications za mwalimu wa grade A, B na C na mahitaji ya qualifications za kufundisha sekondari.) Katika miaka hiyo miwili idadi ya wanafunzi wa sekondari iliongeeka kutoka 337034 hadi 462590 sawa na asilimia 37, idadi ya wanafunzi wanaoingia kidato cha kwanza iliongezeka kutoka 180,239 hadi 243,359sawa na asilimia 35. Bajeti ya kuendesha shule za sekondari ilikuwa ni kama ifuatavyo: mwaka 2005 serikali ilitenga Tsh 104,483m na mwaka 2006 ikatenga TShs 119,987m sawa na ongezeko la asilimia 14.8 tu, kwa hiyo katika mwaka 2006 kulikuwa na degradation katika quality ya elimu ya sekondari kwa wastani wa asilimia ya 63! Ni vizuri niseme kuwa katika bajeti hiyo ya 2006 kulikuwa na fungu la kujenga hizi sekondari anazozungmzuia waziri mkuu kwa hiyo degradation halisi ilikuwa ni zaidi ya asilimia 63 hizo, tukichukulia kuwa pesa zote zilitumika kama ilivyopangwa. Hapo ni mwaka 2006 kabla ndege haijapaa! Kwamba maongezeko ya majengo bila vifaa vya kufundishia hakuonyeshi chochote kuhusu quality ya elimu hiyo. Madhara ya degradation hii hayataonekana mpaka baada ya miaka mitatu au minne wakati watoto waliokuwa form 2 na form 1 watakapofanya mitihani yao ya form 4.

Sasa baada ya kuangalia miaka hiyo miwili, waziri mkuu katuambia kuwa mwaka huu wameongeza shule za sekondari 1,090 sawa na asilimia 64, na idadi ya watoto walioingia sekondari nayo imeongezeka kwa asilimia 65. Kwa wastani wa waalimu 29 kwa kila shule, ina maana kuwa serikali iliajiri waalimu wapya wapato 31,610 kwa mwaka huu tu!. Na kama serikali inataka kuhakikisha kuwa kiwango cha elimu kinabaki kile kile cha mwaka jana (ambacho kilikwisha telemka kwa zaidi ya asilimia 63), inatakiwa itumie angalau TSh 197,979m bila kuweka adjustment ya inflation. Hata hivyo kama sote tunavyofahamu, bajeti ya wizara ya elimu kwa mwaka huu ni TShs 265,679m na kati yake matumizi ya kawaida ni TSh 155,447m ambazo ni chini kabisa ya kiasi kinachotakiwa kutumika kwa matumizi ya kawaida ya elimu ya sekondari tu kulingana na maongezeko aliyosema waziri mkuu. Kwa jumla waziri mkuu hakutoa data za kuonyesha kama kweli elimu ya Tanzania inapaa angani na ndege yake.

(4) Kuhusu kupambana na maradhi waziri mkuu ametueleza idadi ya zahanati zilizojengwa, lakini hakutuambia kuwa walipeleka dawa za namna gani kwenye zahanati hizo ama ziliajiri waganga na manesi wangapi. Vipimo vya kawaida vya kuonyesha kuwa unapambana na maradhi ni kuonyesha jinsi gani serikali imezuia vifo vitokanavyo na maradhi yenye kutibika kirahisi. Ukiachilia mbali HIV/AIDS ambapo serikali imepata fedha nyingi sana kutoka kwa wahisani mbalimbali kama Clinton Foundation na Bill and Melinda Gates foundation, magonjwa ya kawaida kama yale yatokanayo na mlo duni na mazingira machafu yameendelea kuuwa watanzania kwa kasi sana. Takwimu za WHO zinaonyesha kuwa utapiamlo unaikabili asilimia 21.8% ya watanzania wote ambao wengi wamekondeana kwa kukosa lishea na asilimia 37.7% ya watoto wanaozaliwa wameshindwa kukua vizuri kutokana na kukosa lishe. Kwa jumla watanzania asilimia 22% inaishi bila kupata chakula cha msingi na asilimia 39% inaishi bila kupapa mahitaji ya msingi kama maji, malazi n.k. Yote hiyo inapunguza maisha ya watanzia kwa kasi sana na ndiyo mambo makubwa ambayo serikali inatakiwa ipambane nayo pamoja na kujenga zahanati. Waziri mkuu hakuyazungumzia, je rafiki zangu kweli mnaamini takwimu zake?
(5) Utafiti unaoaminika ni ule unaofanywa na independent organization. REDET ni organization ambayo imeshajulikana kuwa siyo indepndent sana inapokuwa inatafiti jambo linalokihusu chama cha CCM, linafanya kazi kwa kuipendelea CCM. Kwa hiyo kuna kila sababu ya kuhoji aina ya watu waliohojiwa na REDET hadi kufikia majumuisho kuwa asilimia 82 ya watanzania wameridhika na maisha wakati asilimia 39 ya watanzania hawapati mahitaji yao ya muhimu. Ijulikane kuwa hata wale ambao wanapata mahitaji ya muhimu hawawezi kuridhika na maisha kirahisi vile.

NYONGEZA: Nimefanya marekebisho kadhaa ya typing na clarification
 
hapa mie nnasema mkuu Kichuguu sina la kusema,

maana umeusuta uongo na kuubanisha ukweli hadharani, sasa ni kazi kwa marafiki zetu kusuka au kunyoa.

mijadala iko wazi tusubiri waziri mkuu atakuja na data zipi, pengine alikuwa anasikilizia upepo
 
Naona niongezee kuwa kama waziri mkuu alitaka kuonyesha jinsi gani serikali yake imepambana na maadui wa maendeleo angeonyesha jinsi walivyopambana na Umaskini, Ujinga, Magonjwa na Dhuluma. Inashangaza kuona kuwa serikali haitaki kuongea chochote kuhusu huyu adui wa maendeleo ajulikanaye kama Dhuluma. Dhuluma ina sura nyingi sana na mojawpao ni rushwa kama vile mikataba ya hovyo ya Richmond na upendeleo (nepotism) kama vile utoaji vyeo kwa wanamtandao bila kujali uwezo wao.
 
Katika yote yakiyoongelewa katika mada hii kilichonisikitisha wala sio majibu ya Waziri Mkuu..ninasikitishwa na wana jambo ambao wameamua kushambulia hoja iliyopelekea majibu hayo..

Huu ni uthibitisho tosha kuwa hao viongozi wetu wamefanikiwa kiasi kikubwa ku-shape akili za watanzania vile watakavyo..yaani kuwafanya waone kuwa kila kinachosemwa na serikali ni sahihi..hata wasomi wenye uwezo wa kuchambua mambo waridhike na statement za kiongozi bila kuuliza... Kwa maneno mengine seriakli ya CCM imefanikiwa kwa kiasi fulani kutuwekea uvivu wakufikiri..Kitendo cha kumkejeli Mwanakijiji..ati anaandika bila takwimu, au anaogopa nini wakati uandishi kautaka mwenyewe..kwangu naona kama its a plus to the CCM govt..wametuharibu akili kweli...wakiongea tu tunaanza kupigana wenyewe kwa wenyewe..baadae tutasema CCM wachawi.. Yes, ni wachawi to the extent kwamba wametujengea culture ya silence, hivyo kwamba anayethubutu kuongea basi tunamuona msaliti, tunawaaacha wasaliti tunauana wenyewe..What a sorry state of affairs

Tuseme hoja ya Mwanakijiji haina maana for lack of research/statistics; swali litakuwa, Why did they bother to respond, tena so vehemently?

Mwenye statistics azilete hapa JF zimsaidie Mwanakiji kujenga hoja; afterall its not a film show, kwamba sisi tukae tuangalie mtu mmoja akipigana na serikali hapo kwenye stage halafu tushangilie mshindi..kama mtu ana data/takwimu anazoona zinapingana au zinakubaliana na hoja aziweke hapa zisaidie kuboresha hoja, mambo ya kutishana, kudharauliana , kukujeliana hayafanani na msimamo wa JF

Ni mawazo yangu tu...
 
ndugu yangu mwendapole

nnategemea unaelewa kuwa mwenda pole hajitomi na mwiba.

mie sisikitishwi hata kidogo na wanayoipinga hoja ya mwanakijiji, maana nnaamini there is no motion without friction, hawa wanasaidia sana kutufanya na sisi gari letu la mapambano ya haki liengeze kasi.

pili ni upanuzi wa demokrasia inapnyesha jambo forums si ya upande mmoja.

pia huenda si kama wanampinga bali wanatoa changa moto na wakati huo huo kuchangia michango yao in another side, mie nnaweza kufikiri huwasilisha mawazo ya watu wa pili vipi wanaweza kufikiri.

kwa hiyo ndugu yangu usikate tamaa.
 
Mi naona asishambuliwe mtu. Hata wale wanaosema Mwanakijiji aandike kwa kutumia takwimu nadhani wanamtakia mema. Wanataka ajenge hoja kamili, yenye ushahidi wa kila aina. So I would take it as constructive criticism...
 
Darasa la Kichuguu ni shule tosha. Nafikiri EL anahitaji watu kama wewe mmsaidie mawazo kama anataka kuisaidia nchi badala ya kuibabaisha!!!
 
Naona niongezee kuwa kama waziri mkuu alitaka kuonyesha jinsi gani serikali yake imepambana na maadui wa maendeleo angeonyesha jinsi walivyopambana na Umaskini, Ujinga, Magonjwa na Dhuluma. Inashangaza kuona kuwa serikali haitaki kuongea chochote kuhusu huyu adui wa maendeleo ajulikanaye kama Dhuluma. Dhuluma ina sura nyingi sana na mojawpao ni rushwa kama vile mikataba ya hovyo ya Richmond na upendeleo (nepotism) kama vile utoaji vyeo kwa wanamtandao bila kujali uwezo wao.

Kichuguu, that #106 deserves to go as a rejoinder to the original Mkjj article.

People must understand, this is not mudslinging anybody. Leaders must earn their living. To do that, they must tell the truth.

The trend shown here, if it continues, will make these leaders think twice before they lie to the wananchi with their eyes open.

Consider the case of a Prof. MP from Rufiji who thinks Electricity is a priority in his constituency at this time!
 
Ushauri wa mwisho kwa MKJJ.

Ni matumaini yetu kwamba kwenye hizo hoja zako unazotayarisha,,, uta-heat point/hoja kuonyesha uintelectual wako... na sio na wewe kuishia kuibua hoja ambazo haziko ndani ya hoja ya WM. au kujibu vibweka vya ati umekimbia nchi etc.

Nia ni kusaidia nchi sio kuonyesha kwamba mnajua kuchonga sana au la!!! Na mwisho usijetumia ushabiki ndugu yangu we need to read facts... yakuunga mkono yaunge yakupinga ukipinge, wasiwasi wangu ni kuchagua scope ya maendeleo unayoyaongelea,,, na kuto-put Tanzania history in perspective.


Kila la Kheri.
 
Kilitime once again.. you are underestimating my intellectual abilitiy to understand the challenge at hand or for uknown reasons (or reasons known to you alone) you are hoping that my academic competence to write a strong, factual, and composed response will not meet JF's intellectual scrutiny and would fall short of a satisfying response. Let me assure you and others, I am up for the challenge and my response will prove to you (and other naysayers) that not only am I able to meet the challenge thrown to me, but I'm well qualified to exceed the expectation in so many ways! So would you just wait until my response is out?

Hata hivyo, siandiki kwa ajili ya wasomi or intellectuals... Hadi hivi sasa nimeshaandika majibu na yako tayari na kwa vile sasa Tanzania Daima wameamua wayachapishe Jumatano ijayo, basi nitatumia muda huu kurevise mambo fulani and as a matter of fact recent developments Bungeni yanaendelea kuthibitisha kuwa Tanzania bado haijaanza kupaa.

Ila ushauri wako wa kutokuwa na jazba nimeutilia maanani kwani my first draft ilikuwa inasomeka kama "Mtikila at the Dock".. so nitabadilisha lugha sehemu fulani fulani, but nitaiacha ili hata mtu ambaye hajapata nafasi ya kufanya mazoezi kisomi ataweza kusoma awe yuko Merelani, Kalenge, Boza, Ikwiriri au Kibanda Maiti.. I promise you it won't be an intellectual or academic paper, itakuwa something that would stimulate the mind and entertain the spirit while at the same time itakufanya utabasamu na kucheka kwa mantiki yake.. for at the end of day I don't want people to be depressed baada ya kusoma majibu yangu.
 
By the way, naomba usiwe ushauri wa mwisho.... majibu yangu mengi yanatokana na michango niliyoisoma humu.. so wengi mtaona mawazo yenu pia yakiwa ndani ya majibu hayo.
 
Katika yote yakiyoongelewa katika mada hii kilichonisikitisha wala sio majibu ya Waziri Mkuu..ninasikitishwa na wana jambo ambao wameamua kushambulia hoja iliyopelekea majibu hayo..

Huu ni uthibitisho tosha kuwa hao viongozi wetu wamefanikiwa kiasi kikubwa ku-shape akili za watanzania vile watakavyo..yaani kuwafanya waone kuwa kila kinachosemwa na serikali ni sahihi..hata wasomi wenye uwezo wa kuchambua mambo waridhike na statement za kiongozi bila kuuliza... Kwa maneno mengine seriakli ya CCM imefanikiwa kwa kiasi fulani kutuwekea uvivu wakufikiri..Kitendo cha kumkejeli Mwanakijiji..ati anaandika bila takwimu, au anaogopa nini wakati uandishi kautaka mwenyewe..kwangu naona kama its a plus to the CCM govt..wametuharibu akili kweli...wakiongea tu tunaanza kupigana wenyewe kwa wenyewe..baadae tutasema CCM wachawi.. Yes, ni wachawi to the extent kwamba wametujengea culture ya silence, hivyo kwamba anayethubutu kuongea basi tunamuona msaliti, tunawaaacha wasaliti tunauana wenyewe..What a sorry state of affairs

Tuseme hoja ya Mwanakijiji haina maana for lack of research/statistics; swali litakuwa, Why did they bother to respond, tena so vehemently?

Mwenye statistics azilete hapa JF zimsaidie Mwanakiji kujenga hoja; afterall its not a film show, kwamba sisi tukae tuangalie mtu mmoja akipigana na serikali hapo kwenye stage halafu tushangilie mshindi..kama mtu ana data/takwimu anazoona zinapingana au zinakubaliana na hoja aziweke hapa zisaidie kuboresha hoja, mambo ya kutishana, kudharauliana , kukujeliana hayafanani na msimamo wa JF

Ni mawazo yangu tu...

Aloo, unajua bado tunasubiri ngwe ya pili ya ile mada ya malalamiko uliyoanzisha juu ya ahadi hewa za Kikwete wakati wa uchaguzi??

Chondechonde tena safari ijayo tunataka na wewe utuwekee takwimu na vikolombwezo vinginevyo vya kutetea hoja zako, na siyo nadharia kavu na riwaya dizaini ya John Rutasingwa.
 
Aloo, unajua bado tunasubiri ngwe ya pili ya ile mada ya malalamiko uliyoanzisha juu ya ahadi hewa za Kikwete wakati wa uchaguzi??

Chondechonde tena safari ijayo tunataka na wewe utuwekee takwimu na vikolombwezo vinginevyo vya kutetea hoja zako, na siyo nadharia kavu na riwaya dizaini ya John Rutasingwa.

VRS,
Polepole kidogo. MKJJ ni mwanadamu- na ana uhuru wa kujibu Hoja na jinsi anavyooona- we learn as we do -and perfect as we go on! Kila mtu ana style yake kujibu mambo.
MKJJ audience sii ya wasomi tu- bali pia Watz wa kawaida wenye uchungu na wazalendo wanaojua kusoma!
Mimi nashauri tuwape moyo Watz wanojitolea to question the status quo in boldness as exemplified by MKJJ!
Hata hivyo MKJJ ni mtu mwuungana sana- hata majibu yake kwako na wengine ni ya kiuungwa! VRS umeangalia majibu na hoja za Dr.WHO?
Wote tujitahidi kujadiliana bila kuwa na jazba!
MKJJ mie binafsi pamoja na yote yanayoseama nadhani una kipaji- na nakuunga mkono!
MzalendoHalisi
 
Back
Top Bottom